Lengo la somo hili ni kukusaidia kujua na kuzitumia sheria mbalimbali za ulimwengu wa kiroho.
Mashitaka ni neno la kisheria,
lenye maana ya kutuhumiwa kufanya kosa Fulani.
Hati ni maelezo halali au kopi yanayoelezea
makosa aliyofanya mtu, na huwa yanatumiwa kama ushahidi kwenye baraza la
maamuzi (mahakama). Lengo likiwa ni kukuondolea uhalali wa kupokea haki zako
unazostahili kuzipata kutoka kwa Mungu.
Kumbuka, kila aliyeokoka ana “package”
yake kutoka kwa Mungu. Ile tu kwamba ameokoka kunampa Mungu uhalali wa
kukuhudumia kwa ukaribu zaidi.
-
Sasa hati ya mashtaka inaondoa huo uhalali wa
wewe kupokea haki zako kutoka kwa Bwana.
Wakolosai 2 : 14 - 15
“akiisha kuifuta ile hati
iliyoandikwa ya kutushtaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu, akaiondoa
isiwepo tena, akaigongomea msalabani”
-
Biblia inaelezea kitu kinachoitwa hati ya
mashtaka kwamba ina uadui kwetu kwa sababu lengo ni kukuzuia usipate
unachostahili kukipata kutoka kwa Mungu ambaye ni Baba yako.
-
Kinachofuta hati ya mashtaka si msalaba bali ni
damu ya Yesu iliyomwagika msalabani. Wakolosai
1 : 20
MAMBO MATATU YA MUHIMU YA KUFAHAMU
KWANZA
A.
Kuna sheria
zinazotawala katika ulimwengu wa kiroho
Kuna sheria zinazotawala katika
ulimwengu wa roho ambazo ni lazima mtu wa rohoni uzifahamu. Hizo sheria
zinafanya kazi katika ulimwengu wa roho na aliyeziweka ni Mungu mwenyewe.
Sheria ni
taratibu na kanuni zilizowekwa mahali Fulani au katika mazingira Fulani ili
kutoa muongozo wa mwenendo wa mahali husika, ikiwemo kuonyesha haki na wajibu
wa kila anayehusika na mazingira hayo au mahali hapo.
-
Ni Mungu mwenyewe kaziweka hizo sheria lakini
pia yeye mwenyewe anazifuata hawezi kuzivunja.
-
Kuna mambo ambayo itakuwa ni vigumu kuyapata
hata kama umeokoka kwa sababu ni lazima ufuate sheria za kiroho kuyapata.
Zipo sheria nyingi katika
ulimwengu wa kiroho zinazofanya kazi lakini mojawapo ni kwamba “Mungu hana ushirika
na dhambi”. Isaya 59 : 1 - 2
-
Tafsiri yake ni kwamba mtu atendaye dhambi hana
ushirika na Mungu, kwa hiyo hawezi akapokea chochote kutoka kwa Mungu.
Zipo sheria nyingi sana, baadhi ya hizo ni:
i.
Sheria ya dhambi na mauti – Warumi 8 : 1 – 2 & Warumi
6 : 23
ii.
Sheria ya uzima – Warumi 8 : 1 – 2 & Yohana
11 : 25 – 26
iii.
Kuna sheria zinazohusu uchumi au mafanikio – Yeremia 29 : 7, 11
iv.
Kuna sheria zinazohusu utawala wa kimaeneo kwa
nguvu ya fedha. Luka 19 : 11 – 27 –
kuna uhusiano uliopo kati ya kuwa na mali nyingi inayopelekea kuwa na nguvu ya
utawala au ushawishi katika utawala uliopo.
v.
Sheria ya kurithi. Waebrania 9 : 16 – 17
B.
Kila tendo
analolitenda mwanadamu linarekodiwa katika nyaraka zilizopo katika ulimwengu wa
roho
Inawezekana ikawa ni matendo mema
au mabaya, yote yanarekodiwa.
-
Matendo mema yanaleta thawabu bali matendo
mabaya yanaleta adhabu.
-
Baadhi ya maeneo yanakotunzwa kumbukumbu za
matendo ya watu ni kama vile:
i.
Aridhi/nchi na mbingu – Yeremia 22 : 29 – 30 & Kumb
30 : 19
Katika ulimwengu wa kiroho ardhi ina uwezo wa kutunza
kumbukumbu, inasikia n.k
ii.
Vitabu vya mbinguni – Ufunuo 20 : 12
Kwa hiyo, kila tendo afanyalo
mwanadamu linaandikwa mahali.
-
Matokeo ya makosa uliyoyafanya yakaandikwa
kwenye kumbukumbu za kiroho huwa yanaweza yakakupata wewe tu au hata uzao wako
baada yako.
-
Makosa au dhambi zilizotendwa na mtu halafu
adhabu yake ikapita mpaka kwa watoto wake huwa yanaitwa “uovu”. Uovu ni dhambi
ambayo hujafanya wewe lakini kwako imepita kama adhabu.
-
Hivyo Mungu anaweza akapatiliza uovu wa baba kwa
watoto wake hata kizazi cha tatu na cha nne. Na pia anaweza akaachilia rehema
zake vizazi baada ya vizazi. Kutoka 20 :
5 - 6
C.
Katika
ulimwengu wa kiroho kuna mahakama.
Mahakama ni eneo ambalo hukumu
mbalimbali zinatolewa kulingana na sheria zilizopo.
-
Kuna kuwa na upande wa mshitakiwa na upande wa
mshitaki, na kuna kuwa na hakimu.
-
Mungu ndiye anayesimama kama Hakimu, Zaburi 7 : 11 & Zaburi 9 : 8. Mtu anasimama upande wa
mshitakiwa na Shetani anasimama kama mshitaki. 1 Petro 5 : 8 & Ufu 12 :
10
-
Shetani huwa anachukua hati iliyoandikwa makosa
yako halafu anakwenda kukushitaki mbele za Mungu.
-
Lengo la Shetani kukushitaki mbele za Mungu ni
ili akuondolee uhalali wakupokea haki zako kutoka kwa Mungu.
-
Mashitaka yanaweza kukuondolea uhalali huo wa
kupokea haki zako. Haki ni chochote unachostahili kukipata kutoka kwa Mungu.
Inawezekana ikawa ni afya njema, maisha ya mafanikio, elimu bora, mafanikio
katika biashara au kazi, utumishi mwema n.k.
-
Mungu anaposimama kama hakimu huwa hayupo upande
wako bali huwa anasikiliza hoja zenye nguvu ili atoe maamuzi (atoe hukumu). Isaya 41 : 21 & Isaya 43 : 26
NB: Sasa tambua kwamba, ili Shetani aweze kukuzuia usifanikiwe
katika mambo yako huwa anaangalia sheria inayompa uhalali wa kukutesa ndipo
anakutesa. Huwa anatafuta kama kuna kosa au uovu uliopo kwenye maisha yako ili
kwa kupitia kosa hilo ndipo akutese. Lakini pia hata kama akikosa huwa anaweza
kukutengenezea mazingira ya kumkosea Mungu ili yeye apate kitu cha kukushitakia
mbele za Mungu.
-
Lengo lake ni kukuangusha tu.
Shetani akipata uhalali mahali,
huwezi kumuondoa usipoondoa kwanza ule uhalali wa yeye kukaa hapo.
Mfano: Marko 5 : 1 – 17
-
Ulishawahi kuona Yesu anakemea pepo halafu pepo
linakataa kutoka?
-
Yesu alikemea pepo litoke wakati lile pepo
limepata uhalali wa kukaa katika lile eneo ndio maana pepo likamwambia Yesu
nakuapisha kwa Mungu usinitese, na pia lilimwambia kuwa asiwapeleke mbali na
mipaka ya nchi ile. Kwa sababu wanaikalia ile nchi kihalali. Na wale watu
hawakumkaribisha Yesu bali walimsihi aondoke mipakani mwao.
-
Hii inaonyesha kuwa kuna mambo hawa watu wa ule
mji waliyafanya yakawapa yale mapepo kibali na uhalali wa kukaa kwenye eneo lao
hivyo hawawezi kutoka kama huo uhalali haujaondolewa.
-
Vivyo hivyo na hata wenye familia yako kama
mapepo yanakaa kihalali basi huwezi kuyakemea mpaka ufute kwanza huo uhalali
walionao ndipo uwakemee watoke.
-
Watu wengi huwa tunakimbilia kuyakemea mapepo
yatoke ndani ya mtu bila kujua hayo mapepo yameingiaje. Ni vizuri ukajua kwanza
mlango walio ingilia ndipo utajua namna ya kuomba.
NB: Kwa hiyo, unapokwenda mbele za Mungu ambaye ndiye hakimu,
kujitetea kwako ndiko kutakupa haki yako.
-
Lakini huwezi ukajitetea mwenyewe bila kuwa na
msaada wa Yesu kwa sababu Yesu ndiye anayesimama kama wakili na mwombezi wetu
kwenye mahakama ya kiroho. Waebrania 7 :
24 - 25
-
Yesu anachofanya huwa ni anakuja na ushahidi wa
damu yake ambayo imemwagika msalabani ikafuta hati inayotushitaki katika jambo
lolote lile.
-
Kwa lugha nyingine ni kwamba Yesu anasema hati
aliyonayo shetani ni hati “fake”
bali ile hati “orijino” ilishafutwa
msalabani kwa damu ya Yesu.
-
Wewe mwenyewe huwezi ukajitetea ukamshinda
shetani kwa sababu yeye shetani anajua sheria za ulimwengu wa kiroho zaidi ya
unavyojua na huwa anatumia udhaifu wa kutokujua sheria ili kukutesa. lakini pia
shetani huwa anatumia hila au udanganyifu kukutesa maana yake anaweza akakutesa
kwa kutumia hati feki.
-
Yesu pekee ndiye wakili mwaminifu na ndiye anayetuombea
kwa sababu ya upendo wake kwetu hataki mtu yeyote ateswe na nguvu za giza. Yeye
ndiye aliye kufa msalabani kwa ajili yetu kwa hiyo ana upendo wa kweli na watu
wake.
Damu ya Yesu pekee ndiyo inayoweza kufuta uhalali wa shetani kutawala
maisha yako. Ina uwezo wa kufuta mashitaka yote ambayo shetani anayapeleka kwa
Mungu juu yako. Ina uwezo wa kufuta kumbukumbu zote zilizoandikwa kukuhusu wewe
ambazo zimebeba adhabu katika ulimwengu wa roho.
Damu ya Yesu ilipomwagika pale
msalabani ilifanya kazi nyingi sana sio tu kutuosha dhambi zetu bali pia kufuta
hati zinazotushitaki. Kwa hiyo usiangalie upande mmoja tu wa kazi ya Damu ya
Yesu bali uiangalie kwa mapana yake ndipo utaona kazi zilizofanywa kwa damu ya
Yesu.
Kumbuka kwamba, Mungu anasimama
kama hakimu, kwa hiyo mtu usipojua namna ya kuitumia damu ya Yesu ili kufuta
mashitaka juu yako basi ujue utaendelea kuonewa na nguvu za giza sana.
-
Biblia inasema “eleza mambo yako upate kupewa haki
yako” Isaya 43 : 26
-
Maana yake usipoeleza mambo yako na usipojua
namna ya kujitetea basi hutopata haki yako.
Katika mahakama
za kawaida hapa duniani, si kila anayehukumiwa ni mtenda kosa bali kuna ambao
walishindwa kujitetea ikapelekea kukosa haki zao.
-
Ushahidi wa anayekushitaki unaweza ukakushinda
kujitetea kwako wewe unayeshitakiwa, hivyo ikapelekea kukosa haki uliyostahili
kuipata.
Namna ya kushughulikia kuondoa umiliki halali wa shetani juu ya kile
unachokiombea katika maisha yako.
i.
Omba toba kwa Mungu juu ya nafsi yako.
ii.
Omba toba juu ya kosa lililompa shetani nafasi
ya kuja na kumiliki kwenye maisha yako kihalali.
iii.
Halafu tumia damu ya Yesu kufuta uhalali huo wa
shetani wa kukumiliki
iv.
Vunja na haribu kazi zote za shetani zilizopitia
kwenye mlango huo aliopitia kuingia kwenye maisha yako.
v.
Mkaribishe Roho mtakatifu ayatawale maisha yako.
Luka 11 : 24 – 27
NB: Mlango anaopitia shetani kuingia kwenye maisha yako unaweza
ukawa ni maneno ya kinywa chako, matendo yako (dhambi) au maovu (dhambi
zilizotendwa na wazazi wako au vizazi kabla yako).
No comments:
Post a Comment