Msisitizo wa somo hili ni kujifunza kuwa na mahusiano ya ngazi ya juu kabisa na Mungu wetu katika msingi wa upendo.
Kumpenda Mungu kuna
kuwa ni nguzo au msingi wa mahusiano yako na Mungu wako.
Marko 12 : 30 –
“nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa
akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.”
Mungu anataka tumpende kwa kiwango cha juu sana kuliko kitu
chochote.
Ndio maana kaweka amri ya kumpenda, japo ilitakiwa hii iwe
ni tabia ya kawaida kwa watoto wa Mungu.
-
Somo hili litakusaidia kujua namna ya kumpenda
Mungu katika kiwango anachokitaka Mungu.
-
Kiwango anachotaka Mungu tumpende si nusu wala
robotatu bali ni kwa nguvu zote, akili zote, moyo wote, na roho yote.
Hapa hatuongelei swala la Mungu kumpenda mwanadamu bali
tunaongelea mwanadamu kumpenda Mungu.
-
Kuna tofauti kubwa sana kati ya Mungu kumpenda
mwanadamu na mwanadamu kumpenda Mungu.
-
Unaweza ukawa unamtumikia Mungu lakini ukawa
humpendi huyo Mungu unayemtumikia.
-
Kumtumikia Mungu haimanishi kwamba ndiyo
unampenda. Unaweza ukawa ni mtumishi wa Mungu mkubwa tu lakini ukawa humpendi
Mungu unayemtumikia.
-
Vita kubwa ambayo shetani anaileta kwa watu wa
Mungu si pale wanapomtumikia Mungu bali ni pale wanapoamua kumpenda Mungu
wanayemtumikia. Uwe na uhakika shetani atakupiga vita ambavyo hukutegemea.
Wafilipi 3 : 8 – Nayahesabu
mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu
Bwana wangu …
-
Mtume Paulo anatuambia juu ya kumpenda kwake
Yesu kulivyokuwa katika namna ambayo ilimfanya ayahesabu mambo yote kuwa hayana
faida kuliko kumpata Yesu.
-
Alimpenda Yesu kwa kila kitu alichokuwa nacho;
moyo wake, mwili wake, nguvu zake, akili zake, vyote vilimpenda Yesu.
Biblia inamaanisha nini inaposema “mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako
wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote”?
NB: Kupenda ni
kuthamini, ni kujali, n.k
Inamaanisha:
i.
Mshirikishe
Mungu kwanza katika kila ufanyalo (kutengeneza ushirika imara na Mungu)
Mithali 19 : 21 – Mna hila nyingi moyoni mwa mtu, bali shauri la
Bwana ndilo litakalo simama. (Hila maana yake ni mipango, shauri maana yake ni
kusudi au mapenzi ya Mungu)
Mathayo 6 : 33 – Bali utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake …
Maana yake katika kila unachofanya
ni lazima utafute kujua kama jambo hilo ni kwa ajili ya mapenzi ya Mungu na si
kwa mapenzi ya kwako binafsi. Kabla hakijawa cha kwako ni lazima kiwe cha Mungu
kwanza.
Uzito wa hii pointi upo kwenye
neno “kwanza”. Tafsiri yake
ni kwamba; kuna watu wanafanya maamuzi juu ya mambo Fulani kwenye maishi yao na
wanakuja kumjulisha Mungu juu ya kile walichokwisha kukiamua na si kuomba Mungu
awasaidie kufanya maamuzi.
-
Mfano:
unaweza ukawa umemuona mtu ukampenda na ukataka kumuoa lakini unakuja kumuomba Mungu
akusaidie umpate mtu huyo ili umuoe. Tangu ulipoanza kutafuta mwenza wako
hukumshirikisha Mungu ili akusaidie umpate mtu sahihi kwa ajili yako lakini
ulipomuona Fulani ndipo ukaenda kwa Mungu ukihitaji akupatie huyo.
-
Hapo hujamshirikisha Mungu kwanza bali umefanya
maamuzi yako kwanza.
-
Kilichoanza si Mungu kwanza bali ni maamuzi yako
kwanza.
Kwa kumshirikisha Mungu kwanza
katika kila unachofanya, kunampa Mungu kuwa na nafasi ya kwanza moyoni mwako. Kuwa
na ushirika na Mungu ni jambo la muhimu kupita tunavyofikiri.
ii.
Bila
msaada wa Mungu huwezi kufanya jambo lolote kama ikupasavyo kufanya.
Mithali 3 : 5 , 6 – Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala
usizitegemee akili zako mwenyewe.
-
Maana yake ni kwamba mwanadamu ameumbwa katika
Namna ambayo hawezi akafanikiwa pasipo kupata msaada wa Mungu.
-
Akili yako kuna mahali itafika itashindwa
kukusaidia. Kinachotakiwa ni wewe kuwekeza akili yako yote kwa Mungu.
-
Neno “kutumaini” maana yake ni kutarajia, au
kutegemea
iii.
Muda
au mali au mwili wako ulio nao si wako kwa ajili yako bali ni kwa ajili ya
Bwana
Warumi 12 : 1,2 – Itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu
ya kumpendeza Bwana …
Mithali 3 : 9 – 10 – Mheshimu Bwana kwa mali yako na kwa malimbuko
yako yote …
Zaburi 24 : 1 – Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na
wote wakaao ndani yake.
-
Ni muhimu kuelewa kwamba kila kitu alichonacho
mwanadamu ni mali ya Mungu. Hata mwili na pumzi uliyonayo si ya kwako bali ni
ya Mungu.
-
Kwa hiyo unaweza ukavitumia vitu hivyo vyote
alivyokupa Mungu kwa ajili ya Mungu.
-
Wakolosai
1 : 16 – vitu vyote viliumbwa kwa ajili yake na kwa njia yake
-
Unapotoa muda wako kwa ajili ya Mungu inaonyesha
kwamba unampenda Mungu
-
Unapotoa mali zako kwa ajili ya Mungu inaonyesha
kuwa unampenda Mungu n.k
iv.
Kwa hiyo, kumpenda Mungu ni mfumo tulioumbiwa nao ili tuwe
nao, lakini kwa sababu ya dhambi kuingia ulimwenguni tukapoteza hiyo tabia ya
kumpenda Mungu na badala yake tukaipenda dunia.
1 Yohana 2 : 15 - 17
-
Dhambi ilichofanya ndani ya moyo wa mtu si tu kuondoa
tabia ya kupenda bali ilibadilisha kipaumbele cha kupenda. Badala ya mtu
kumpenda Mungu akaanza kuipenda dunia.
-
Vita kubwa aliyonayo shetani juu ya watu a Mungu
ni kuhakikisha watu wa Mungu hawampendi Mungu wao wanayemtumikia.
-
Japokuwa kwa nje tunaona wanamtumikia Mungu
lakini ukweli ni kwamba hawampendi Mungu wanayemtumikia.
Mathayo 15 : 8 – 9
-
Watu hawa wanamheshimu Mungu kwa midomo yao
lakini mioyo yao iko mbali na Mungu wanayemheshimu.
-
Hakuna mahali kwenye Biblia inaposema mpende
Bwana Mungu wako kwa midomo yako yote bali imesema umpende Bwana Mungu kwa moyo
wako wote.
-
Sasa kwenye hii mistari inaonyesha kwamba mioyo
ya watu iko mbali na Mungu wao, japo kwa midomo yao wanaonekana kama
wanamtumikia Mungu. Tafsiri yake ni kwamba hawampendi Mungu wao kwa mioyo yao
yote japo wanamtumikia.
-
Na zaidi sana ni kwamba, kule kumpenda Mungu
kuliko pungua ndani yao kunapelekea kutokumsikiliza tena na badala yake
wakaanza kusikiliza sauti za wanadamu wenzao wasisikilize sauti ya Mungu.
VIASHIRIA (INDICATORS) VINAVYOONYESHA KAMA MTU ANAMPENDA MUNGU WAKE KWA
KIWANGO KINACHOHITAJI
i.
Kushika
na kufuata maagizo na maelekezo anayopewa na Mungu (utii wa Neno la Mungu).
Yohana 14 : 15- mkinipenda mtazishika amri zangu.
1 Samweli 15 : 22 – kutii ni bora kuliko dhabihu
Kusikiliza maagizo ya Mungu ni
kiashiria kikubwa sana cha kuonyesha kama mtu anampenda Mungu au hampendi.
-
Kwa sababu ukimpenda Mungu basi utamsikiliza na
kufuata Neno lake.
-
Zaburi
119 : 11 – moyoni mwangu nimeliweka neno lako nisije nikakutenda dhambi.
-
Hajasema kwamba moyoni unaweka huduma au unaweka
watu au wazazi bali amesema kuwa ameweka neno la Mungu maana yake Mungu atakapokuwa
anazungumza naye basi atasikia na kutii.
-
Mfano, mtu unayempenda utamsikiliza.
ii.
Ushirika
na Mungu wake unazidi kuimarika (intimacy fellowship with God)
Yohana 14 : 15, 16 – 17
-
Hiki ni kiashiri kinachoonyesha kukua kwa
ushirika baina yako na Mungu wako
-
Ushirika maana yake ni kuungana,au kuwa na
umoja, au kuwa na mahusiano ya ndani zaidi.
-
Watu wenye ushirika mmoja wana tabia ya kuwa na
mawasiliano ya karibu katika namna ambayo hadhi ya mahusiano yao ikipungua basi
watajua kuwa mahusiano yao yamepungua, na yanahitaji kurekebishwa.
Kutoka 33 : 15 – Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue
kutoka hapa
-
Musa alikuwa anajua kabisa kwamba ameanza safari
ya kuwatoa waisrael utumwani akiwa na mahusiano mazuri na Mungu, lakini sasa
inafika mahali Mungu anaamua kumtuma malaika wake badala ya Yeye mwenyewe
kwenda pamoja na Musa
-
Na hiyo ilikuwa inamaana kuwa hadhi ya mahusiano
baina ya Mungu na Musa ilikuwa imeshuka.
-
Huwezi ukaanza safari na Mungu halafu umalize na
malaika. Katika ulimwengu wa roho, hilo ni gap kubwa sana
iii.
Kiwango
cha kuwapenda watu wanaomzunguka kitaongezeka.
1 Yohana 4 : 20 – mtu akisema nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu
yake, ni mwongo.
-
Kumpenda Mungu ndani yako kutaachilia msukumo na
tabia ya kuwapenda wengine bila kujali wanamwabudu Mungu unayemwabudu au la.
-
Kosa moja ambalo wapendwa wengi huwa tunalifanya
na huwa tunadhani ni kawaida ni kuwa na uhusiano mzuri na wapendwa wenzetu tu,
lakini hao wengine hata kusalimiana nao huwa hatusalimiani.
Mathayo 5 : 43 – 47 – mkiwapenda wanaowapenda ninyi tu mwapata
thawabu gani, tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada?
-
Ni muhimu kujua kwamba kipimo cha kumpenda Mungu
kinapimwa kwa kuangalia kiwango chako cha kuwapenda wengine. Kwa sababu huwezi
kumpenda Mungu usiyemuona halafu mtu unayemuona humpendi.
-
Ndio maana Biblia inasema mpende jirani yako
kama nafsi yako.
-
Na jambo la ajabu ni kwamba na Mungu ameweka
hata kipimo cha msamaha kitokane na kipimo cha sisi kuwasamehe wengine. Mathayo 6 : 12, 14
NB: Kwa hiyo mtu akija akikuambia kwamba kumpenda Mungu ni
kuwachukia watu wengine basi anakudanganya.
-
Ni kweli unaweza usichangamane nao katika
shughuli zao lakini haimaanishi uwachukie.
-
Kwa sababu Biblia inatutaadharisha kutokushirikiana
nao katika dhambi wala kuwafuata lakini tunatakiwa kuwapenda, kuwaombea na
kutafuta kuwa na amani na wao.
iv.
Utoaji
Kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda, mtatwaa sadaka
kwake
Kutoka 25 : 1 - 2
Kutoka 35 : 5
-
Hakuna upendo usiokuwa na msukumo wa kutoa.
-
Kipindi kile wana wa Israel walikuwa wanasafiri
na hawakua na makazi ya kudumu, na Mungu alkuwa akiwtembelea na kuondoka.
Lakini alipotaka kuketi katikati yao alitoa utaratibu wa nini kifanyike ili
uwepo wake uwe pamoja nao.
-
Ndipo akasema kila mtu ambaye moyo wake wampa
kupenda, mtatwaa kwake sadaka.
-
Angalia lile neno “kila mtu ambaye moyo wake
wampa kupenda”, kupenda nini? Kupenda uwepo wa Mungu ukae kwake.
-
Hii haikuwa sadaka ya kawaida bali ilikuwa ni
sadaka ya kuuleta uwepo wa Mungu ukae katikati ya wana wa Israel.
Yohana 3 : 16 – kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata
akamtoa mwana wake wa pekee ….
-
Mungu mwenyewe anatufundisha kuwa watoaji, kwa
jinsi alivyomtoa Mwana wake wa pekee.
-
Ni kanuni ya kiroho kwamba kupenda kunaendana na
kutoa
-
Huwezi ukatoa kama hupendi.
-
Utoaji wa kumpenda Mungu hutoangalia kama unacho
au huna. Utakuwa radhi kutoa vyote ulivyonavyo kwa sababu tu unampenda Mungu.
-
Swala la utoaji kwako halitakuwa swala gumu,
maana kuna watu wanapotoa sadaka huwa wanaumia mioyo yao sana kana kwamba
wanapoteza, na wengine wanatoa tu ili mradi wabarikiwe lakini si kwa sababu
wanapenda kutoa.
Hebu tuone mifano
kadhaa ya watu wanaomtumikia Mungu bila kumpenda Mungu wanayemtumikia.
Mfano 1: Mathayo 7 :
21 – 23
Si kila mtu aniambiaye Bwana Bwana atakayeingia katika
ufalme wa mbinguni …
-
Hawa watu walikuwa wanamtumikia Mungu, na cha kushangaza
zaidi ni kwamba hata ishara na maajabu vilitendeka kupitia mikono yao, lakini
Mungu aliwaambia kuwa siwajui ninyi. Maana yake walikuwa wanamtumikia Mungu
bila kuwa na ushirika na Mungu wanayemtumikia.
-
Ni sawa na kutokee wakala “fake” wa kuuza simu
za kampuni Fulani ambayo inatengeneza simu halali lakini anayeziuza hizo simu
halali si wakala halisi wa hiyo kampuni. Kwa hiyo simu zinazouzwa ni halali, na
kampuni inayotengeneza hizo simu ni halali, lakini wakala ni “fake”. Hivyo
kampuni haimtambui wakala anayeuza simu hizo japokuwa simu zinazouzwa na huyo
wakala ni simu halali za hiyo kampuni.
NB: Mungu anawapenda watu wote. Lakini wale watu wanaompenda Mungu
ndiyo hao ambao Mungu anawajua.
Mfano 2: 1 Samweli 15: 23
Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe
…
-
Mfalme Sauli aliambiwa na Mungu kwamba nenda
kawapige Waamaleki wote wala usiache hai kiumbe chochote, lakini yeye hakuua
wanyama walionona, akawaleta ili kuwatoa sadaka kwa Mungu.
-
Alienda kinyume na maagizo aliyopewa na Mungu
wake, akafanya aliyoyaona yeye kuwa ni mazuri. Hakujua kuwa “utii ni bora
kuliko sadaka”. Kumtii Mungu ni muhimu zaidi kuliko kutoa sadaka asiyokuambia
uitoe.
-
Hii inamaanisha kwamba, mfalme Sauli hakutimiza
ule mstari unaosema kwamba “Mkinipenda mtazishika amri zangu”. Kwa Sauli huo
mstari haukuwepo.
-
Kwa hiyo alikuwa ni mtu anayemtumikia Mungu
lakini yuko mbali na Mungu wake. Hana ushirika naye, hasikilizi neno lake n.k.
NB: Ni maombi
yangu kwako kwamba umfahamu Mungu zaidi na zaidi na zaidi ili uishi kama
apendavyo yeye na si kama upendavyo wewe.
-
Ukae katika Neno lake
-
Uyafanye yale yanayompendeza
-
Na umzalie Mungu matunda kwa kila kai njema
ndani yako.
No comments:
Post a Comment