Hesabu 13 : 1 – 2,
25, 27 – 33; 14 : 1 – 11
Safari ya Wana wa Israeli ilikuwa ni safari ya kutoka nchi
moja kwenda nchi nyingine, ilikuwa ni safari ya kutoka hali Fulani ya maisha
(hali ya umasikini na utumwa) na kwenda kwenye hali nyingine nzuri zaidi ya
maisha (hali ya utajiri na heshima na uhuru).
Japo bado unaweza ukaitafsiri safari ya wana wa Israeli kama
safari kwenda mbinguni kwa sababu ina mambo yanayofanana na yanayotusaidia
kwenye safari yetu ya kwenda mbinguni.
Kila hatua waliyokuwa wanaipitia kwenye safari ile ilikuwa
ina umuhimu mkubwa sana mbele za Mungu na kwenye maisha yao kwa sababu ilikuwa
inaamua waendelee na safari au wasiendelee.
Kuna mambo waliyokuwa wanayafanya amabayo yaliwakwamisha
katika safari yao kiasi kwamba waliweza kukaa eneo moja kwa muda mrefu kama
adhabu.
-
Na hivyo ndivyo ilivyo kwenye maisha yetu jinsi
ambavyo kuna mambo tunaweza kuyafanya lakini yakapelekea kukwama tusivuke au
tusiendelee mbele, na kuna mambo mengine yanaweza yakatufanya tusonge mbele.
Katika hii mistari tuliyoisoma inaeleza habari ya wapelelezi
walivyokwenda na kurudi kuipeleleza nchi yao ya ahadi. Lakini cha ajabu ni
kwamba taarifa waliyoileta haikuwa nzuri kwao
Sasa haya mambo manne ni mambo ambayo huwa pia yanatokea sana
kwenye maisha yetu ya kila siku na pengine yanatukwamisha kutokuendelea mbele
MAMBO
YALIYOJITOKEZA HAPO:
1. Taarifa iliyoletwa na wapelelezi ilikuwa ni
moja lakini tafsiri ya hiyo taarifa zilikuwa tofauti
Wale watu waliokwenda kuipeleleza nchi walikuwa ni watu 12,
kumi kati yao walitafsiri kuwa ile ni nchi ambayo ina watu walio hodari kuliko
Waisraeli hivyo hawataweza kupigana nao na kuwashinda.
-
Na kwa sababu hiyo wakatafsiri kuwa ni nchi inayowala
watu wake.
-
Ni kweli kwamba ile nchi ilikuwa na watu warefu
walioitwa majitu (Wanefili au wana wa Anaki), ni kweli ile nchi ilikuwa na
maboma makubwa na maadui zao walikuwa wanakaa kwenye milima amabapo si rahisi
sana kuwashinda kwenye vita.
-
Lakini kati yao wapo watu wawili waliotafsiri kuwa
hata kama hao watu wana nguvu kuwashinda wao bado Israeli wanaweza kuwashinda.
-
Na hii ndio changamoto watu wengi tuliyonayo pale
ambapo tunakabiliana na mazingira magumu huwa tunawahi kutafsiri kushindwa,
tunaona ukubwa wa tatizo kabla ya kuona mpenyo wa Kimungu wa kutusaidia kuvuka
hapo.
-
Kwenye safari ya maisha yapo mambo mengi tunakutana
nayo na tunashindwa kuyavuka kutokana na vile tunavyoyatafsiri.
-
Ukishindwa kutafsiri jambo matokeo yake ni kufanya
sawasawa na vile ulivyotafsiri.
-
Kama ulitasiri kuwa mazingira ya kufanya biashara
kwamba ni magumu hutapata faida basi ni kweli hutoifanya hiyo biashara lakini
ukitafsiri kuwa mazingira ni magumu lakini bado utapata faida basi utafanikiwa.
-
Na ndio maana tunatakiwa tuwe makini na kila habari
tunayoletewa, kwa sababu shida haiku kwenye habari unayoletewa bali iko kwenye
tafsiri ya hiyo habari.
-
Isaya 53 :
1 – Nani aliyesadiki habari tuliyoileta, mkono wa Bwana amefunuliwa nani?.
Hii maana yake ni kwamba mkono wa Bwana anafunuliwa Yule aliyeamini habari za
Bwana alizoletewa.
-
Ni muhimu sana kupima kila jambo kwa jicho la rohoni
ilikuona kilichobebwa katika kila habari unayoletewa.
-
Katikati ya mazingira magumu wakina Kalebu na Yoshua
waliona ushindi wakati wale wengine wote kumi waliona kushindwa. Katikati ya
giza nene wao waliona nuru ikiwazukia.
NB: Chukulia mfanao unataka kuanzisha biashara, kigezo
kimojawapo ni lazima upate taarifa za kutosha juu ya hiyo biashara kama itakupa
faida au la, pia kama soko lake linapatikana kwenye mazingira unayotaka
uianzishe, na mambo mengine ya muhimu. Lakini unapokea taarifa kwamba biashara
katika eneo hilo ni ngumu hutopata faida lakini ndani yako Mungu ndiye
aliyekuambia kwamba nenda kaanzishe biashara eneo hilo. Unachotakiwa ni
kumwamini Mungu na sio mazingira unayoyaona.
2. Tafsiri ya jinsi walivyojiona nafsi zao
mbele ya adui zao.
Hawa watu kumi wanasema walijiona nafsi zao kama mapanzi na
ndivyo wao walivyowaona wao hivyo.
-
Hapa Biblia inatuonyesha kuwa watu hawa walijiona kwa
kujilinganisha na mapanzi, wakaenda mbali zaidi kwa kufiri na wale watu
waliwaona hivyo.
-
Swali la kujiuliza ni kuwa, nani aliwaambia kuwa watu
wale wanawaona wao kuwa kama mapanzi?
-
Kujiona kama mapanzi mbele ya wale watu ni sawa na
kujilinganisha uwezo wao kana kwamba panzi anapigana na mtu.
-
Walijiona kama si kitu kabisa, kana kwamba hawana
uwezo wowote.
-
Biblia inasema kuwa ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo
alivyo (Mithali 23 : 7). Maana yake
ni kuwa ukijiona wewe ni hodari na shujaa basi utakuwa ni shujaa kweli bali
ukijona wewe ni mnyonge na mdhaifu basi utakuwa ni mnyonge na mdhaifu kweli.
-
Kumbuka kuwa nguvu ya utendaji inatoka ndani mwako,
inategemea tu kile kiwango unachoamua kukiachilia ili kifanye kazi.
-
Na katika jambo hili la watu wanavyojiona nafsini mwao
kumesababisha wakwame maeneo mengi sana bila ya kujua nini cha kufanya.
-
Inawezekana kwamba muda mwingi umekuwa ni mtu wa
kusema mimi siwezi tu mimi siwezi tu kwenye kila kitu, na kweli umekuwa huwezi.
Na hii si kwa sababu huna uwezo bali ni kwa sababu umejijengea fikra hizo
kwamba huwezi.
-
Na jambo baya zaidi ni kwamba macho yanapoona jambo
yanapeleka taarifa kwenye ubongo wako na ubongo wako unatoa tafsiri. Sasa kama
ubongo wako utatoa tafsiri kwamba jambo Fulani huwezi basi mwili wako wote
unapokea amri kwamba jambo Fulani huwezi, hivyo inapelekea kushindwa kufanya
mambo mengi tu ambayo kimsingi yapo chini ya uwezo wako lakini akili yako
imekataa kuwa huwezi kuyafanya.
-
Mfano mmojawapo ni kwamba wanafunzi wengi wanafeli
kwenye masomo yao si kwa sababu hawana akili bali ni kwa sababu wanajiona kuwa
hawawezi kufaulu mitihani yao wakijilinganisha na wanafunzi wengine wenye akili
kupita wao.
3. Jinsi hofu ilivyoshinda imani yao kinyume
na Mungu wao (maana yake hofu iliondoa imani ndani yao)
Kumbuka imani ni kuwa na uhakika wa kile unachokitarajia
hivyo hofu inaondoa huo uhakika na kwa sababu hiyo Hofu ni adui mkubwa wa
imani.
-
Ndani mwako ukiwa na hofu basi imani inapungua au
inakufa kabisa, unakuwa huna imani tena.
-
Wale wana wa Israeli waliposikia habari ile waliingiwa
na hofu kubwa sana kiasi kwamba si tu ilishusha imano yao kwa Mungu wao bali
pia kilifisha kabisa imani yao kwa Mungu. Ikapelekea waamue kurudi Misri.
-
Hofu iliingia ndani mwao kwa sababu waliona tatizo ni
kubwa kuliko Mungu wao anaeweza kuwaokoa na tatizo
-
4. Kutokutambua
kuwa Ahadi za Bwana ni hakika na kweli
Mungu aliwaahidi kuwa atawatoa kwenye nyumba ya utumwa na
kuwapeleka kwenye nchi ijaayo maziwa na asali, na kweli nchi ya Kaanani ilikuwa
ni nchi ijaayao maziwa na asali.
-
Wapelelezi wote walithibitisha jambo hilo
-
Nataka tufahamu kwamba Mungu akiahidi anatekeleza kwa
sababu Mungu si mwanadamu hata aseme uongo – Hesabu 23 : 19/ 1 Samweli 15 : 29/ Tito 1 : 2
-
Mungu hawezi kusema uongo na wala hana kigeugeu maana
yake ni kwamba akisema amesema.
-
Zaburi 138
: 2 – Mungu ameikuza ahadi yake kuliko jina lake.
-
Inapofika mahali unatilia mashaka ahadi za Mungu maana
yake unawaza kwamba anaweza akasema uongo.
Ahadi inaleta tumaini au subira. Na
ndani ya tumaini kuna uvumilivu. Na uvumilivu unaleta utulivu rohoni. Kwa hiyo
hata kama kuna mazingira magumu yoyote utakayopitia bado hayataweza kuondoa ule
utulivu ndani yako kwa sababu una uhakika na ahadi za Mungu kwamba ni kweli
zitatimia.
Lakini pia tufahamu kuwa ahadi za
Mungu zina kanuni zake (terms and conditions).
-
Fahamu ya kwamba ili Mungu attimize ahadi yake huwa
anafuatilia vigezo vya hiyo ahadi aliyokuahidia.
Mifano,
-
Mtu akinitumikia Baba atamheshimu – Yohana 12 : 26
-
Utakaposikiliza
sauti ya Bwana na kufuata maagizo yake basi utabarikiwa – Kumb 28 : 1 -14
No comments:
Post a Comment