Somo hili litakusaidia kujua mambo ya msingi ya kufanya kabla hujaamua kwenda mbele za Mungu
Zaburi 24 : 3 – 6
-
Ni nani atakayepanda katika mlima wa Bwana? Ni
nani atakayesimama katika patakatifu pake?
-
Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe
-
Asiyeinua nafsi yake kwa ubatili, wala hakuapa
kwa hila.
-
Atapokea Baraka kwa Bwana na haki kwa Mungu wa
wokovu wake
-
Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, wakutafutao
uso wako, ee Mungu wa Yakobo
Katika mistari hii tunaona kwamba kuna sifa za mtu
astahiliye kwenda mbele za Mungu au kusimama patakatifu pa Mungu
Na hivyo vigezo ni kama ifuatavyo:-
1)
Mtu aliye
na mikono safi
Biblia inatueleza kwamba kigezo kimojawapo cha kumwona Mungu
ni kuwa na mikono safi.
Na hapa ni muhimu ukajifunza kuangalia jambo kutokea rohoni
kwanza kuja mwilini.
-
Anaposema mikono safi hamaanishi usafi wa mikono
kwa namna ya nje bali usafi wa mikono kwa jinsi ya rohoni.
-
Hapa Biblia inatuonyesha kwamba katika ulimwengu
wa kiroho, mikono inaweza ikawa safi au michafu kulingana na kilichofanywa na
hiyo mikono.
-
Kwa lugha nyingine ni kwamba ulimwengu war oho
unaweka rekodi ya kila kinachofanyika duniani na hasa zaidi kinachohusisha
mikono ya mtu.
-
Mikono yako ikishiriki katika kutenda uovu basi
ulimwengu wa roho utajua na utaweka kumbukumbu, na hivyo hivyo ukitenda mema.
-
Na kwa sababu hiyo tunapata kutambua hali za
kiroho za mikono yetu.
Hili si somo jepesi sana na wala si jipya lakini tunamuomba
Mungu kwa njia ya Roho mtakatifu atusaidie akili zetu tuelewe na tupate kile
alichokikusudia Mungu tukipate.
Nataka
tuone baadhi ya mifano kwenye Bblia inayoonyesha hali za kiroho za mikono yetu:
Mfano 1. 1 Nyakati 22 : 8, & 1 Nyakati 28
: 3 (Mikono kujaa damu)
-
Mfalme Daudi aliambiwa na Mungu kwamba
hatomjengea Mungu hekalu kwa sababu mikono yake imejaa damu kwa kuwa amekuwa
mtu wa vita vingi.
Isaya 1 : 15 – Nanyi mkunjuapo mikono yenu nitaficha macho yangu
nisiwaone, naam mwombapo maombi mengi sitasikia maana mikono yenu imejaa damu.
-
Biblia inatuonyesha jambo la ajabu hapa kwamba
unapokwenda kwenye vita na ukamwaga damu, basi hiyo damu inabaki katika mikono
yako katika ulimwengu wa kiroho.
-
Na kama hujajua namna ya kushughulika na hali
hiyo basi mikono yako itabaki katika hali hiyo siku zote na itakunyima kumuona
Mungu kwa kiwango kinachotakiwa. Maana yake ni kwamba Mungu kujifunua kwako
kunaweza kukazuiliwa kwa sababu ya hali ya kiroho ya mikono yako ambayo imejaa
damu.
-
Mungu alikataa kuwasikiliza waombaji si kwa
sababu waombaji wanaomba vibaya bali ni kwa sababu wamekwenda mbele za Mungu
angali mikono yao imejaa damu.
-
Pia Mungu alikataa Daudi asimjengee Nyumba
(hekalu)si kwababu mahusiano kati ya Daudi na Mungu wake yalikuwa si mazuri
bali ni kwa sababu Daudi alikuwa na mikono iliyojaa damu kwa sababu ya vita
alivyopigana.
-
Na ukiangalia Daudi alikuwa na nia njema kabisa
ya kujenga nyumba ya Mungu lakini kilichomkosesha kibali mbele za Mungu ni
mikono yake yenye damu.
-
Kilichokwamisha majibu ya maombi ya hawa watu si
kutokuwa na imani, wala maombi yao kuzuiliwa na mkuu wa anga, n.k bali ilikuwa
ni mikono yao iliyokuwa imejaa damu ndio ilimfanya Mungu aache kuwasikiliza na
kuwajibu.
Mithali 6 : 16 – 18
Katika vitu saba anavyovichukia
Bwana kimojawapo ni mikono imwagayo damu isiyo na hatia.
Mfano 2. Yeremia 44 : 8, Yeremia 25 : 14,
& Zaburi 18 : 20, 24 – 26 (Mikono inaweza ikabeba adhabu au baraka)
Biblia inasema Mungu atawalipa kwa kadiri ya matendo yao na
kwa kadiri ya kazi ya mikono yao. Na mahali pengine inasema, Bwana amenilipa
sawasawa na usafi wa mikono yangu.
-
Kilichobebwa kwenye mikono yako kinaweza
kikaathiri hali yako katika ulimwengu wa kimwili. Kwa sababu kama iliyobebwa ni
adhabu basi adhabu hiyo itadhihirika mwilini na kama kilichobebwa ni Baraka
basi Baraka hiyo itadhihirika mwilini.
Baadhi ya mambo yanayohusu mikono
yako ambayo chanzo chake ni rohoni lakini yanatokea mwilini
a. Mikono inaweza ikadhoofika au ikatiwa nguvu
Yeremia 38 : 4 –
Mikono kudhoofika
Waamuzi 7 : 11 –
Mikono kutiwa nguvu
NB: Kibiblia anapoongelea mikono anamaanisha utendaji kazi.
Kwa hiyo utendaji kazi wako unaweza ukadhoofika au ukatiwa nguvu.
-
Mikono yako inaweza ikadhoofishwa au ikatiwa
nguvu kutokana na maneno unayosikia.
-
Kwa tafsiri nyingine ni kwamba ni muhimu
kuchunga na kuchuja kila unachokisikia kinachokuhusu kwa sababu kinaweza
kikaathiri utendaji kazi wako.
-
Watu wengi wameacha huduma na vipaji vyao kwa
sababu walisikia maneno juu ya huduma zao na yakadhoofisha huduma hizo.
-
Maneno yanaweza yasiharibu moyo wako lakini yanaweza
yakadhoofidha mikono yako kiasi kwamba ukashindwa kufanya uliokusudia kufanya.
-
Wapendwa wengi tunakumbuka kulinda mioyo yetu tu
kwa sababu tunalinda imani zetu lakini tunasahau kulinda na mikono yetu
isidhoofishwe.
Ezra 6 : 22 –
Mungu akawafurahisha kwa kumgeuza moyo mfalme wa Ashuru awaelekee ili awatie
nguvu mikono yao katika kazi hiyo ya nyumba ya Mungu .
-
Kwa hiyo Mungu anaweza akaachilia mazingira
yatakayotia nguvu mikono yako ili uifanye kazi yake.
b. Mikono ya mtu inaweza ikataabika
Ezekiel 7 : 27 –
mikono ya watu wa nchi itataabika.
Kutaabika maana yake ni kuhangaika pasipo kuzalisha matunda
yaliyokusudiwa.
-
Mfano wa mtu au watu ambao mikono yao inataabika
ni pale unapofanya biashara kwa juhudi na bidii kubwa tu lakini mwisho wa siku
huoni faidi uliyoikusudia.
c. Mikono inaweza ikawa na hila.
Isaya 25 : 11
Hila ni mashauri au makusudio au nia.
Mathayo 5 : 30 na
Mathayo 18 : 8
2)
Mtu aliye
na moyo mweupe
Kigezo kingine cha kuweza kumwona Mungu ni kuwa na moyo
mweupe au moyo safi.
Kama kuna moyo mweupe au safi basi pia kuna moyo mchafu.
Mathayo 5 : 8 –
heri wenye moyo safi maana hao watamuona Bwana
-
Biblia kwenye mistari hii haijaelezea habari ya
kumwona Bwana baada ya kufa bali imeelezea habari ya kumuona Mungu kabla ya
kufa maana yake katika ulimwengu huu wa mwili.
-
Moyo safi unakupa credit ya kumuona Mungu.
Marko 7 : 20 – 23 haya ni baadhi ya mambo ambayo yanaweza
yakachafua moyo wa mtu na yakamzuia asimwone Bwana.
Mithali 6 : 16 – 19 baadhi ya vitu asivyovipenda Bwana ni pamoja na
moyo uwazao mawazo mabaya.
-
Na ndio maana Biblia inatutaka tulinde sana
mioyo yetu kwa sababu inaweza ikatukwamisha tusimuone Mungu.
-
Kuna mambo hatutaweza kuyapata kutoka kwa Mungu
kwa sababu tu mioyo yetu haiko safi.
3)
Mtu
asiyejiinua nafsi yake kwa ubatili.
Ubatili maana yake ni uongo.
Kujiinua nafsi yako maana yake ni kujiona bora zaidi kupita
wengine. Ni kujihesabia haki.
Ezekieli 28 : 1 – 2,
6 – 8, 17 – moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako.
Luka 18 : 10 – 14
ukijikweza utashushwa na ukijishusha utakwezwa.
Kuna aina nyingi za kujiinua:
i.
Kuna wanaojiinua kwa sababu ya uzuri au hali
nzuri ya maisha waliyonayo
ii.
Pia kuna wanaojiinua kwa sababu ya utakatifu/
uchaji walionao.
Lakini kujiinua kote huku bado
Mungu anapakataa. Maana yake ni kwamba Mungu anahitaji unyenyekevu.
4)
Mtu
asiyeapa kwa hila
Neno linatukataza kuapa kwa namna yoyote ile, ila linatutaka
ndio yetu iwe Ndio na siyo yetu iwe Siyo.
Mathayo 5 : 33 – 37
Usiape kabisa.
Hesabu 30 : 2 –
kiapo kinaweza kikafunga nafsi yako.
Kumb 23 : 21 – 22
NB: DAMU YA YESU NDIO JIBU LA CHANGAMOTO ZOTE HIZO
Waebrania 10 : 19 –
22
-
Kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu
kwa damu ya Yesu ….
-
Damu ya Yesu pekee ndio inayotustahilisha
kuingia mbele za Mungu na kumweleza Mungu haja za mioyo yetu.
No comments:
Post a Comment