MUNGU ANVYOTUMIA AKIBA YA MAOMBI YAKO KUKULETEA MSAADA KWENYE MAISHA YAKO

 Lengo la somo: kukuwekea msukumo ndani yako wa kuendelea kuomba bila kukata tamaa ili kujiongezea akiba zaidi ya maombi mbele za Mungu.

 

Utangulizi:

Mbele za Mungu hakuna maombi ya watakatifu yanayopotea.

-          Mahitaji yako au majibu ya maombi yako yanategemea kiwango cha maombi unachokiachilia ili kushughulikia mahitaji hayo. Kama hitaji lako ni kubwa na linahitaji kiwango kikubwa cha maombi basi ujue ukiomba kwa kiwango kidogo hakitaweza kutengeneza majibu ya maombi hayo,

-          Lakini pia unapokuwa ni muombaji wa mara kwa mara basi ujue kuwa unajiwekea akiba ya maombi yatakayoweza kukusaidia wakati wa uhitaji.

Matendo 10 : 1 – (4) – 8

-          Hizi ni habari za mtu mmoja aliyeitwa Kornelio, alikuwa ni kamanda wa jeshi la Kirumi lakini alikuwa ni mcha Mungu maana yake alikuwa na hofu ya Mungu ndani yake pamoja na nyumba yake yote.

-          Kitu cha pekee kumuhusu huyu mtu ni kwamba alikuwa anawapa watu sadaka nyingi na pia alikuwa ni muombaji. Biblia inasema siku moja malaika wa Bwana alimtokea akamwambia kuwa sadaka zako na sala zako zimefika mbele za Mungu na kuwa ukumbusho. Na baada ya hapo akaambiwa akamlete mtume Petro aje amwambie Neno la Bwana.

Nataka uone jambo hapa: kilichomsukuma Mungu kutuma malaika kwenda kwa Kornelio ni kwa sababu ya akiba ya sadaka pampja na maombi yake mbele za Mungu.

Kwa leo tuangalie kile kipengele cha akiba ya maombi ambayo yamekuwa ni ukumbusho mbele za Mungu.

-          Biblia inaonyesha wazi kabisa kwamba mtu anaweza akawa ana akiba ya maombi mbele za Mungu na Mungu akaitumia hiyo akiba kwa ajili ya kumletea mtu huyo mssada pale atakapokuwa anauhitaji.

-          Hapa kwenye hii story hatuoni kama huyu Kornelio alimuomba Mungu ampe msaada lakini kwa sababu sala zake zimekuwa ni ukumbusho maana yake akiba yake ya maombi ilikuwa inadai mbele za Mungu kuwa huyu apewe msaada hivyo ilimbidi Mungu amletee msaada.

 

Hebu tuangalie mistari ifuatayo inaelezea jambo la ukumbusho wa maombi yetu mbele za Mungu.

Ø  Ufunuo 5 : 8 – vitasa vilivyojaa manukato ambayo ni maombi ya watakatifu

Mbinguni, maombi yetu huwa yanapimwa, na pia huwa yanakuwa ni manukato kwa Mungu maana yake yanaleta harufu nzuri kwa Mungu mpaka yanamfanya akumbuke haja za kila mtu aliyekuwa anaomba hayo maombi yaliyokuwa manukato.

Kwa hiyo kila akisikia harufu nzuri ya yale manukato basi anakumbuka haja za watakatifu wake walioomba.

Ø  Isaya 43 : 26 – Unikumbushe na tuhojiane, eleza mambo yako upate kupewa haki yako

Ø  Isaya 62 : 6 – 7 – Ninyi wenye kumkumbusha Bwana msikae kimya wala msimwache akakaa kimya

Ni tabia ya Mungu kutaka kukumbushwa juu ya haja zetu tulizomuomba mbele zake.

-          Haimaanishi kuwa Mungu amesahau bali anachotaka Mungu ni kuona uhitaji tulionao juu ya kile tunachomuomba.

-          Ile kwamba tunaombea jambo Fulani mara kwa mara inaonyeha ni kwa jinsi gani tunahitaji Mungu atusaidie katika jambo hilo.

-          Kwa mfano, fikiria una mtoto ambaye ni mwanafunzi na anadaiwa ada ya shule, sasa anakuja kukuambia wewe mzazi wake. Kutoa hiyo hela ya ada kunategemea na jinsi mtoto huyo atakavyokuambia, mwingine atakavyokuambia utaona kuna haja ya kumpa hapo hapo au utaona haina uharaka sana wa kuitoa hiyo ada hapo hapo. Ndivyo na kwa Mungu wetu kulivyo.

-          Unaweza ukawa unahitaji Mungu akufanyie jambo Fulani lakini ukawa hauko serious katika kumuomba Mungu, kwa hiyo Mungu naye akachelewa kukufanyia jambo hilo.

-          Ule u-serious unaokuwa nao kwenye maombi ndio unaomfanya Mungu akuhudumie kwa haraka. (lakini kila jambo ni kama linaendana na makusudi ya Mungu).

 

¨      Hivyo unapoomba mara kwa mara unakuwa unamkumbusha Mungu juu ya haja zako ulizo nazo lakini utakapopita kwenye shida ambayo itakufanya ushindwe kuomba ikupasdavyo basi yale maombi ambayo yapo kama akiba yatasimama kama ukumbusho mbele za Bwana kwa ajili yako. Na Mungu atakuletea msaada wa kukuvusha katika hali uliyonayo kwa sababu ya akiba hiyo ya maombi.

Na ukumbuke ya kwamba hatuachi kuomba kwa sababu jambo Fulani tumeliombea kwa muda mrefu au kwa sababu tumechoka kuomba bali ni kwa sababu Mungu ametenda kama tulivyomuomba au kwa sababu amani ya Kristo ndani yako imekusukuma kuliachilia jambo hilo kwa shukrani kwa njia ya imani kuwa Mungu atatenda kwa wakati wake kama apendavyo Yeye mwenyewe.

Kwa hiyo usione shida kuendelea kumkumbusha Mungu juu ya mahitaji yako mbele zake.

 

v  Kuna mazingira unaweza ukapitia kwenye maisha yako ambayo ni magumu na yakakufanya hata ushindwe kuomba. Sasa kama ulikuwa ni muombaji kipindi cha nyuma basi ujue kwamba Mungu huwa anaweza kutumia akiba ya maombi yako kuja kukusaidia katika hali hiyo unayoipitia.

Waefeso 6 : 13 – angalia lile neon analosema “mpate kushindani siku ya uovu”

-          Siku ya uovu maana yake ni siku za shida au za hatari au siku zenye changamoto kwa mwanadamu.

-          Na kila mtu anazo siku za uovu, maana yake kila mtu kuna siku atapitia kwenye shida Fulani ambayo atahitaji Mungu amsaidie hata kama yeye atashindwa kuomba. Sasa Mungu atakusaidia endapo tu kama wewe ulikuwa ni muombaji maana yake ataangalia kwenye akiba yako ya maombi kama kuna kitu cha kukusaidia au la.

Uko upendeleo kwa watoto wa Mungu (watakatifu) kwa sababu maombi yao huwa hayapotei bali yanabaki kama ukumbusho kwa Mungu.

No comments:

Post a Comment

Katika maisha yako usisikilize watu wanasema nini bali msikilize Mungu anasema nini, kwa sababu watu hawajui ni nini ambacho Mungu amekupang...