DARASA LA WANAOUKULIA WOKOVU
19/03/2023
Mungu
ameweka vigezo na masharti juu ya kila anayetaka kumfuata Yesu Kristo
-
Ili uwe
mwanafunzi waYesu Kristo ni lazima ufuate vigezo na msharti aliyoyaweka
1.
Kujikana
mwenyewe na kujitwika msalaba wako
Luka 9 : 23 – 26
Mathayo 10 : 34 – 39
Luka 14 : 25 – 33
Mistari hiyo
hapo juu inaelezea sifa ya mtu atakaye kumfuata Kristo ya kwamba ni lazima
ajikane mwenyewe na aubebe msalaba wake ndipo amfuate Yesu.
-
Kujikana mwenyewe
ni kufanya maamuzi ya kuachana na yake mambo ambayo yatakuzuia ushindwe
kumfuata Yesu kwa uaminifu.
-
Yanaweza
yakawa ni mambo mabaya au yakawa ni mambo yanayoweza yakachukua nafasi ya Mungu
ndani ya moyo wako.
-
Mungu
anapoona kuna jambo ambalo linaweza likachukua nafasi yake ndani ya moyo wako
basi huwa anakuambia mapema kwamba uachane na jambo hilo.
-
Ndio maana
kwenye hiyo mistari hapo juu inaonyesha wazi kwamba Yule asiyemchukia baba yake
aua mama yake au mke wake au familia yake basi huyo hastahili kuwa mfuasi wa
Yesu. Maana yake ni kwamba watu hao unaweza ukawaweka moyoni nao ukawasikiliza
wao sana kuliko kumsikiliza Mungu.
-
Mfano: Mungu
anaweza akakuagiza uende ukahubiri mahali fulani, lakini mzazi wako akakukataza
usiende kuhubiri kutokana na hatari anayohisi inaweza ikatokea juu yako
utakapokwenda. Hivyo ikapelekea wewe kumsikiliza sana mzazi wako badala ya
kumsikiliza Mungu aliyekutuma kazi hiyo.
Si watu
wengi sana wanajua kwamba watu wako wa karibu wanaweza wakakuzuia usiwe
mkamilifu mbele za Bwana. Ndio maana anasema katika ile Mathayo 10 : 36 – na adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake.
-
Hapa
anaongelea adui ambao wanamkwamisha mtu kuwa mwanafunzi mwaminifu wa Yesu Kristo.
-
Anachomaanisha
hapa si kwamba ukawachukie watu wa familia yako kwa sababu wao ni wabaya bali
anakupa taadhari ya kwamba watu wanaoweza kukukwamisha wewe usiwe mwanafunzi wa
Yesu kwa ukaribu kabisa ni watu wa nyumbani mwako.
-
Familia yako
au ndugu zako hawatakiwi kuchukua nafasi ya Mungu ndani ya moyo wako.
-
Mungu
anachotaka ni kwamba akiwa anasema na wewe uwe unasikia na kutii, badala ya
kuwa unasikia na sauti ya ndugu zako wakikuamulia kuifuata sauti ya Mungu au
uipuuzie.
-
Huo ndio
unaitwa msalaba wako, kwa maana hutokuwa unapata ushirikiano mzuri na watu wa
familia yako au ndugu zako kwa sababu wataona kila wanachokushauri kinyume na
yale maagizo ya Mungu huwa hawafanikiwi.
Msalaba
tafsiri yake ni mateso au adha au shida. Hivyo kujitwika msalaba wako maana
yake ni kukubali kuyabeba mateso yatakayotokea wakati wewe ni mwanafunzi wa
Yesu.
Baadhi ya
mateso au shida hizo ni kama
-
Kuchukiwa na
kukataliwa na ndugu
-
Kutengwa na
familia
-
Kutopata
msaada kutoka kwa watu ambao ungefikiri wangekusaidia wakati wa uhitaji. n.k
Yote hayo
unaweza ukayajumuisha katika sentensi moja nayo ni : kupiga gharama ya wokovu
Biblia
inatuambia katika kile kitabu cha Luka
14 : 28 -32 ya kwamba mtu akitaka kujenga mnara ni sharti apige gharama
kwanza kabla hajaanza kujenga ili ajue ataweza kujenga au hatoweza kukamilisha
ujenzi huo.
Na vivyo
hivyo katika kuwa mwanafunzi wa Yesu ni lazima upige gharama kwanza na kujua
kwamba unatakiwa kuacha hata vile vitu ulivyokuwa ukivipenda hapo mwanzo ili
visije vikakufanya ukashindwa kuwa mwanafunzi mwaminifu wa Yesu Kristo.
Wengi
tunataka kuingia kwenye wokovu na mambo yetu ya kale (tabia za zamani) ambayo
hayatufaidii kitu tena.
Biblia
inaseam kuwa itamfadia nini mtu akiupata ulimwengu wote na kupa hasara ya nafsi
yake? Itakufaidia nini wewe kuupata utajiri wote na mali zote halafu roho yako
ikaenda kuangamizwa katika jehanamu ya moto?
Hivyo ni
lazima kupiga gharama na kujua kuwa kuna mambo ya kuachana nayo hata kama kwa
nje tunaona yanatusaidia na yanapendeza.
Biblia
inasema katika kile kitabu cha 1 Yohana
2 : 15 – 17 “mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”
-
Ili umpende
Kristo na uwe mwanafunzi wake mzuri ni lazima usiipende dunia wala mambo ya
duniani.
2.
Kutokupenda
mali zaidi ya kumpenda Yesu Kristo.
Mtu ambaye
anapenda fedha au mali zaidi ya kumpenda Yesu hafai kuwa mfuasi wa Yesu.
Mathayo 6 : 24
Mathayo 19 : 16 – 22
Biblia
inasema mtu hawezi akatumikia mabwana wawili (Mungu na mali)
Nataka uone
jambo fulani hapa: kwa nini Biblia inasema mabwana wawili ikiwa inamjumuisha
mali sawasawa na “bwana”?
-
Jibu lake ni
kwamba Mungu akiingia ndani yako, wewe unakuwa mtumishi wa Mungu, lakini pia na
mali ikiingia moyoni mwako, unakuwa mtumishi wa hiyo mali. Kwa hiyo mali nayo
inakuwa ni bwana wako.
-
Ndio maana
Yesu anasema huwezi ukatumikia mabwana wawili kwa sababu wote watataka ufanye
kile wanachokuambia.
-
Katika
ulmwengu wa roho, fedha au mali ni kiumbe kinachoweza kukutumikisha kama
utakipa nafsi moyoni mwako kikutawale.
Kwa hiyo ni
lazima ujue namna ya kuepukana na tamaa za mali ili usiwe mtumwa wa mali na
badala yake uwe mtumwa wa Kristo.
Mali
zilimfanya yule kijana ashindwe kumfuata Yesu.
-
Ndani yake
kupenda mali kulizidi kumpenda Yesu hivyo akaamua afuate mali kuliko kumfuata
Yesu.
Ziko sifa
nyingi za mtu anayetakiwa amfuate Kristo, lakini kwa leo tutajifunza hizo mbili
tu.
Ubarikiwe.
No comments:
Post a Comment