Luka 15 : 11 – 32
Hii ni habari inayoonyesha baba
mmoja aliyekuwa na watoto wawili wa kiume, na mdogo aliamua kuchukua sehemu ya
mali inayomwangukia kama urithi wake kutoka kwa babaye.
-
Na kweli tunaona baada ya muda mfupi alichukua
mali yake na kuondoka.
Sasa kwenye hii habari kuna mambo
kadha ya kujifunza, na hayo mambo nimeamua kuyaita kama masomo kwa sababu
yamechanua kwa upana wake.
-
Ni masomo ndani ya somo.
-
Unaweza ukayaelezea kama masomo kamili
yanayojitegemea moja moja.
MASOMO YALIYOJITOKEZA NI KAMA
IFUATAVYO:
1.
Kustawi
kwako kimaisha kunategemea kufuata maelekezo ya Kimungu na maonyo yake
Luka 15 : 13 - … akatapanya mali huko kwa maisha ya uasherati
Mithali 29 : 3 – apendaye hekima humfurahisha babaye bali
ashikamanaye na makahaba hutapanya mali
Hekima ni kuwa na ufahamu na
ujuzi wa namna ya kuishi ikupasavyo kuishi
-
Pia hekima ni kuwa na ujuzi na ufahamu wa namna
ya kufanya jambo Fulani .
-
Hekima inakupa muongozo wa namna jambo fulani
linavyotakiwa kufanyika
Mhubiri 7 : 12 – hekima ni ulinzi kama vile fedha ilivyo ulinzi
-
Kuna mambo duniani ambayo huwezi ukayatekeleza
na ukafanikiwa kama huna hekima ndani yako.
-
Unaweza ukawa na elimu ya darasani nzuri tu
lakini ukawa huna hekima kwa hiyo ukafeli kimaisha .
-
Matumizi sahihi ya fedha au mali uliyonayo
hayahitaji sana kwamba ni lazima uwe na elimu ya darasani baliunahitaji kuwa na
hekima ya kukusaidia kutumia vizuri mali zako.
-
Biblia inasema asiye na hekima atajishikamanisha
na makahaba, na kwa hiyo atatapanya mali
-
Ndio maana watu wengi ambao wana elimu hawajui
namna ya kutumia vipato vyao ili kuwafanikisha, kwa sababu kinachokufanikisha
si elimu uliyonayo bali nihekima uliyo nayo.
-
Elimu inaweza ikakusaidia kupata fedha bali
hekima itakusaidia kujua namna ya kutumia hizo fedha ili ufanikiwe.
-
Kwa hiyo watu wengi wana fedha au wanapata fedha
lakini hawana mafanikio. Matumizi sahihi ya fedha yako hayahitaji elimu yako
bali yanahitaji hekima.
-
Ukiwa na hekima , hiyo hekima itakulinda kwa sababu
hekima ni ulinzi
Biblia inaposema hekima ni ulinzi
maana yake ni kwamba hekima itakusaidia kufanya maamuzi sahihi ili usichague
kufanya jambo litakalokuangamiza kama vile kujishikamanisha na makahaba.
Yohana 15 : 4, 5, 7
-
Tukiwa nje ya Yesu hatutaweza kufanya jambo
lolote tukafanikiwa.
-
Ukikaa chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu
utapokea maelekezo ya kukufanikisha kimaisha.
Yakobo 3 : 17 – Hekima itokayo juu kwanza ni safi…
Kwa hiyo maisha ya Yule mwana
mpotevu yaliharibika si kwa sababu alikuwa maskini bali kwa sababu alikosa
hekima.
NB: Na ndio maana unatakiwa umuombe Mungu hekima kwanza ili milango
ya fedha inapofunguliwa mbele yako, fedha hizo zisikuangamize.
Kuna watu ambao Mungu hawezi
kuwaruhusu wakafanikiwa kwa kuwatajirisha kwa sababu anajua kwamba wakipata
fedha tu watapotea na kukengeuka.
2.
Ufahamu juu
ya kuweka akiba
Akiba ni mali au amana ya sasa
inayohifadhiwa kwa ajili ya matumizi ya baadaye (hasa zaidi wakati wa uhitaji)
Luka 15 : 14 – alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia
katika nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji.
NB: Kabla hatujaendelea, nataka ufahamu aina mbili za njaa
zinazoongelewa hapa:
a. Njaa
iliyokuwa imeingia katika nchi nzima ambayo chanzo chake ni mabadiliko ya hali
ya hewa ikasababisha mavuno kukosekana na kupelekea kukosekana kwa chakula
ndani ya nchi. Watu wote wanakutana na hiyo njaa
b. Njaa
inayompata mtu baada ya kutumia feha zake zote vibaya kwa sababu hakuweka akiba
wala hakufanya maendeleo yoyote kipindi anazo fedha. Hii ni njaa ndani ya njaa
-
Wakati watu wanalia njaa kwenye nchi kwa sababu
kuna ukame, wewe unalia njaa kwa sababu hata kama chakula kingekuwepo
usingekuwa na fedha ya kununulia chakula.
Mojawapo ya changamoto na uzembe
wanaokutana nao wapendwa ni swala la kukosa kuwa na tabia ya kuweka akiba.
-
Mtu mwenye tabia ya kuweka akiba ni mtu
anayeiona kesho yake wakati hiyo kesho haijafika.
-
Akiba ni jambo la kiroho kabla halijawa jambo la
kiuchumi.
-
Ukitaka kufanikiwa kimaisha basi kati ya mambo
ya msingi ya kuzingatia na kufahamu ni namna ya kuweka na kutumia akiba.
Akiba ina muda wake wa kuweka na
ina muda wake wa kutumia.
-
Unaweza ukapatia muda wa kuweka akiba lakini
ukakosea muda wa kuitumia hiyo akiba.
-
Ndani yako ukiwa na tabia ya kuweka akiba ni
lazima tabia ya uvumilivu ijengeke ndani mwako. Kwa sababu kuna wakati utataka
kuitumia lakini utajua kuwa matumizi hayo si sahihi kwa wakati huo, hivyo
uvumilivu na subira vinahitajika ndani mwako.
-
Akiba ili iwe akiba ni lazima ikusaidie baadae
wakati wa uhitaji. Kama akiba haikusaidii baadae basi hiyo si akiba.
Mfano: Yusufu alipoweka akiba ya chakula katika taifa la Misri
Mwanzo 41 : 33 – 36
-
Nchi nzima ya Misri kulikwa hakuna mtu mwenye
ufahamu wa kuweka akiba.
-
Akiba ilisaidia nchi ya Misri na nchi za jirani
zisiharibiwe kwa njaa
-
Yusufu alikuwa anakusanya sehemu ya tano ya
mavuno yaliyovunwa nchi nzima na wananchi wenyewe kila mwaka kwa miaka saba
lakini wananchi wenyewe hawakuwa wanaweka akiba.
-
Wananchi walijua kuzalisha chakula lakini
hawakujua namna ya kuweka akiba ya chakula.
-
Chakula kile kile alichokikusanya Yusufu wakati
wa miaka ya shibe ndicho chakula kile kile alichokuja kuwauzia wananchi kwenye
miaka ya njaa. Wananchi walijua namna ya kulima na kuvuna chakula lakini
hawakujua namna ya kuweka akiba.
Mithali 6 : 6 – 8 – Ewe mvivu mwendee chungu, zitafakari njia zake
ukapate hekima, maana yeye hujiwekea akiba ya chakula wakati wa mavuno.
-
Wanyama au wadudu wanafahamu umuhimu wa kuweka
akiba lakini wanadamu wenye akili hawajui kuweka akiba.
NB: Fahamu kuwa swala la luweka akiba ni kanuni mojawapo ya
mafanikio basi uwe na uhakika kwamba Shetani atakupiga vita sana kwamba usiweke
akiba.
Kuna:
-Akiba ya fedha/ mali
-Akiba
ya chakula
-Akiba
ya maombi
-Akiba
ya wema/ kusaidia
3.
Kutubu ni
kubadilka mtazamo
Toba maana yake ni kubadilika mtazamo.
To repent – to change your mindset
Mtu anaposema anatubu juu ya
maisha yake ya dhambi aliyokuwa akiishi- maana yake anamua kubadilisha mtazamo
wake juu ya maisha yake na kugeuka.
Toba inaanzia kwanza kwenye akili
yako.
-
Kama ulikuwa ni mwizi, ukaamua kutubu, maana
yake unaanza kubadilisha mtazamo wako wa kutotaka tena kuiba.
-
Ule mtazamo wako wa kutaka kutoendelea kuiba
tena ndio tunaita kutubu.
Luka 15 : 17 – alipozingatia moyoni mwake
-
Maana yake alipoamua kubadilika, alitafakari
namna ya kurejea kwa baba yake.
-
Alipiga gharama ya maisha anayoishi na maisha ya
watumishi wa baba yake wanavyoishi akagundua kuwa anaishi chini ya kiwango
lakini akajua kuwa kuna nafasi ipo ya yeye kurejea hata kama atarejea kama
mtumishi na si mwana.
Kutubu ni matokeo ya kujutia
dhambi ulizofanya au kujutia mfumo wa maisha uliyokuwa ukiishi na kuamua
kubadilika uishi tofauti na ulivyokuwa ukiishi awali.
-
Kule kujutia kunakufanya ubadilishe mtazamo wako
wa maisha na kuamua kugeuka ili uishi kama vile apendavyo Mungu
Pia kutubu kunakupa kuhesabu
gharama ya maisha unayoyaendea.
-
Unapiga gharama ya kwamba zamani nilikuwa
ninatumia ujanja ujanja kupata mali au fedha iliyokuwa si halali kwa ajili ya
kujikimu lakini sasa ninaokoka kwa hiyo mali ya dhuluma ninaachana nayo,
-
Au ulikuwa ni mtu unayependa kutembea na watu
zaidi ya uliyenaye kwenye ndoa lakini unapookoka unaanza kubaki na mmoja tu.
-
Kama ulikuwa ni mtu wa kujipatia mali za haraka
haraka unaamua kufanya kazi halali ili ujipatie riziki yako iliyo halali.
Kwa hiyo unapiga
gharama ya maisha ili uamue kweli kubadilika. Na unapotubu unajua kabisa kwamba
maisha yako bila kuwa na Yesu Kristo kama kiongozi wako hutoweza kufika
mbinguni.
Watu wengi wanapokosea na kutenda
dhambi huwa hawataki kurudi kuungama dhambi zao na kuomba rehema kwa Mungu bali
wengi wanaona aibu
Mithali 28 : 13 – afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeye
aziungamaye na kuziacha atapata rehema
-
Mwana mpotevu alipozingatia moyoni mwake aliamua
kurudi kwa baba yake na kutubu.
-
Hakuona aibu kwamba ataonekanaje wala hakujali
watumishi wa baba yake watamdharau au la bali alinia kurudi na kumuomba msamaha
baba yake ili maisha yake yawe salama.
4.
Msamaha wa
Mungu unakurejesha katika nafasi uliyoipoteza mbele za Mungu.
Fahamu hili, kwamba dhambi
inakutoa kwenye nafasi bali msamaha unakurejesha kwenye nafasi.
Luka 15 : 20 – 24 – (22) lakini baba aliwaambia watumwa wake
lileteni upesi vazi lililo bora mkamvike, mtieni na pete kidoleni, na viatu
miguuni.
i.
Vazi
linawakilisha utambulisho na heshima
Esta 6 : 10 – 11
Kipindi cha zamani hata cha sasa
kuna mavazi ambayo ukiyaona utajua tu huyu mtu anacheo kipi. Kwa mfano jeshini,
wanajeshi wanatambuana kwa mavazi yao yenye vyeo.
Kwa hiyo mwana mpotevu
alivalishwa vazi bora ili atambulike kama mwana na si mtumwa.
ii.
Pete
inawakilisha mamlaka
Mwanzo 41 : 41 –
43
Esta 3 : 10
Esta 8 : 2, 8
Mwana mpotevu alirejeshewa
mamlaka aliyokuwa amepoteza wakati alipoondoka katika nyumba hiyo.
iii.
Viatu
vinawakilisha utayari wa kurejea na kuanza maisha mapya. Ndani
Efeso 6 : 15
Amani inaleta utayari
Hivyo mwana mpotevu alipopata
amani moyoni mwake kwa sababu ya msamaha kutoka kwa baba yake ndipo akapata
utayari wa kuanza maisha hayo kwa upya tena.
NB: Jambo la muhimu la kufahamu
hapa ni kwamba msamaha wa Mungu kwenye maisha yetu hautokani na sisi kuomba
msamaha bali unatokana na upendo wake Mungu kwetu sisi.
Isaya 43 : 25 – Mimi ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu
mwenyewe
-
Hausamehewi kwa sababu umeomba msamaha bali
unasamehewa kwa sababu Mungu anakupenda na hataki uangamie.
-
Mungu alitupenda kabla hatujaomba msamaha – Yohana 3 : 16
-
Ndio maana Biblia inasema tunaokolewa kwa neema,
maana yake si kwa jitihada zetu wala juhudi zetu bali ni kwa pendo la Mungu
mwenyewe. Efeso 2 : 8 – 9
5.
Haki ya kuwa
mrithi
Kila anayeokoka anafanyika kuwa
mrithi kwa Mungu, kwa sababu tumepewa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu, kwa
hiyo kama tumefanyika kuwa wana basi tu warithi
Wagalatia 4 : 1 - 7
Anapoongelea mrithi kuwa mtoto
haongelei swala la umri bali swala la ukomavu wa akili unaoonyesha kwamba
mrithi anauwezo wa kusimamia na kutekeleza majukumu yake.
Katika Israel, walikuwa
wanautaratibu wakuhakikisha kijana ni mpaka afikishe miaka 30 ndipo ajulikane
kwamba ni kijana mtu mzima anayeweza hata kupewa majukumu ya familia.
-
Chini ya miaka 30 bado ulihesabiwa kama mtoto.
Uko chini ya uangalizi wa wazazi.
-
Kwa hiyo hata kama wewe ni mtoto ambaye ni
mrithi halali kwa baba yako bado ulikuwa huwezi ukakabidhiwa mali bila kuwa
chini ya usaidizi wa mtu mwingine.
Kinacholeta shida si umri bali ni
ukomavu wa akili za Yule anayerithi.
Luka 15 : 28 – 31, 12
-
Ndio maana kilimpa shida Yule kijana mkubwa
aliposikia ya kwamba mdogo wake amerudi na amefanyiwa sherehe kubwa wakati yeye
hajawahi kufanyiwa shrehe yoyote kwa baba yake.
-
Kitu ambacho baba yake alikuwa anajaribu
kumuonyesha ni kwamba wewe ndiye mrithi wa haya yote wala hauhitaji kukasirika
bali unatakiwa kufurahi.
-
Ni swala la muda tu kwamba bado uko chini ya
uangalizi wa baba lakini mali zote izo ni za kwako.
Swala la muda katika kurithi ni
swala la muhimu sana kwa sababu anayerithiwa ndiye anayepanga muda wa kurithiwa
na sio anayerithi.
Ukirejea katika ile Wagalatia 4 : 2 Biblia inasema ‘bali yu
chini ya mawakili na watunzaji hata wakati uliokwisha kuamriwa na baba’.
-
Hapa anaongelea swala la muda sahihi wa mtoto
kurithi vitu vya baba yake.
-
Mungu anajua ni muda gani sahihi wa kukupa vitu
na ni muda gani si sahihi wa kukupa kwa hiyo ni vyma ukaendelea kunyenyekea
chini yake mpaka muda alioukusudia yeye mwenyewe.
-
Kuna vitu unaweza ukapewa sasa na vikaharibu
uhusiano wako na Mungu, badala ya hivyo vitu vikusaidie na vikufainikishe,
vinakurudisha nyuma kiroho.
-
Kumbuka kila jambo lina wakati wake hivyo
usitamani upate kitu chochote kabla ya wakati ulioamriwa.
HITIMISHO
Ni matumaini yangu kuwa somo hili
litakujengea msingi mzuri na kuimarisha mahusiano yako na Mungu.
Sasa utajua kuwa hii habari ya
mwana mpotevu si tu habari ya kijana kutaka mali kwa baba yake na kuondoka bali
ni habari yenye masomo muhimu ya kujifunza ndani yake.
Unaweza ukawa upo kwenye nafasi
ya kijana mdogo aliyechukua mali na kuondoka au ukawa kwenye nafasi ya kijana
mkubwa aliyeamua kubaki kuishi kwa baba yake.
-
Kila mmoja alikwama mahali pake lakini Mungu
wetu ni wa rehema nyingi ambaye hatuachi tukaangamia.
Bwana Yesu Kristo na akubariki
sana.
No comments:
Post a Comment