Msisitizo wa somo hili ni kujua umuhimu wa kusikiliza na kufuata maelekezo ya Mungu anayokupa Yeye kulingana na hali uliyo nayo.
Biblia
inatupa uhakika kwamba tunaoomba chochote kwa mapenzi ya Mungu yeye anajibu. Na
pia hakuna lisilowezekana kwake.
Sasa
mistari inayotuongoza kwenye hili somo ni Zaburi
32: 8 nayo inasema “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea,
nitakushauri jicho langu likikutazama.”
Biblia
inatuonyesha kuwa Mungu anaweza akakufundisha na pia anaweza akakuonyesha nini
cha kufanya. Sio tu hayo bali pia anaweza akakushauri.
Somo
hili linalenga kukuonysha namna ambavyo Mungu huwa anajibu maombi ya watu
katika namna tofauti tofauti. Mungu anaweza akakujibu maombi yako sawasawa na
vile ulivyomuomba au akakujibu kwa kukupa maelekezo yatakayokusaidia upate kile
unachokiomba.
Unajua
waombaji wengi wamekosa kuwa na nafasi ya kumsikiliza Mungu anasema nini
wanapoomba, au wanapoombea jambo Fulani. Mungu anapenda kuzungumza na watu
wake. Hii ni tabia ya kawaida ya Mungu anapojidhihirisha kama Baba kwa watoto
wake. Na anataka sio tu wewe uwe unamuomba yeye tu bale na Yeye pia upate
nafasi ya kumsikiliza asemapo.
Lakini
pia tukumbuke kuwa Mungu huwa anatumia njia tofauti tofauti katika kuzungumza
na watu wake. Hii ni kutokana na hadhi ya mausiano baina ya Mungu na mtu
binafsi. Kuna wakati Mungu anaweza akaongea nawe kupitia ndoto, maono, neno la
maarifa, sauti ya wazi, kupitia mtumishi wake au moja kwa moja kupitia Neno
lake unapolisoma.
NB: Ni lazima tukumbuke kuwaa katika
kila hali na chochote tunachopitia kuna Neno la Mungu katika hali hiyo.
Yohana 1: 1 – 3 – Vyote vilifanyika kwa
huyo, wala pasipo Yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika.
-
Hii
inamaanisha kuwa hakuna hali utakayopitia halafu Mungu asiseme na wewe.
-
Ni
vile tu kwamba Mungu anasema na wewe lakini huelewi au hujui namna ya kumsikiliza.
Kwa
hiyo ni hasara kubwa sana kutosikiliza sauti ya Mungu hata kama unatumia Muda
mwingi kuomba kwa sababu Mungu anaweza akakujibu na wewe usitambue kuwa
amekujibu. (Prayer is a kind of two ways communication). Tunapoomba mbele za
Mungu ni lazima pia tupate nafasi ya kumsikiliza anaposema nasi juu ya yale
tunayomuomba.
FAIDA ZA KUSIKILIZA NA
KUFUATA MAELEKEZO YA MUNGU
1. Mungu
ataamuru Baraka yake ikujilie au ikufuate.
Kumb 28: 1, 2
Mbaraka
wa Mungu ni Zaidi ya mafanikio ya mwanadamu. Unaweza ukafanikiwa kwenye
biashara yako kwa mfano lakini usiwe na mbaraka wa Bwana juu ya hiyo biashara.
Kwa nini?
Kwa sababu biashara inaweza
ikakupa faida nyingi lakini isikusaidie kukutoa kimaisha. Na ndio maana watu
wengi wanafanya kazi za kuajiriw lakini maisha yao ni magumu sana kana kwamba
hawana kazi lakini wana kazi. Unaweza ukajiuliza hivi hizo pesa na mishahara
yao wanapeleka wapi? Lakini ukweli ni kwamba kazi zao au biashara zao hazina
mbaraka wa Mungu ambao ungewafanikisha kimaisha.
Kwenye
mbaraka wa Mungu kun ulinzi wa Mungu, Amani ya Mungu, utoshelevu wa Kimungu,
uzidisho wa Kimungu na kibali cha Mungu.
2. Unapata
uhakika wa ushindi
Waamuzi 7: 1-2, - 7, - 9 –
Gidioni
aliandaa jeshi kubwa sana kwa ajili ya kupigana na Wamidiani lakini Mungu
alimwambia apunguze jeshi hilo hadi kufikia wat5u 300, na kuna maelekezo alimpa
ya nini cha kufanya.
-Mungu
akikuahidi kuwa atakupigania ni kweli kwamba atakupigania. Unachotakiwa ni
kusikiliza sauti ya Mungu inayokupa maelekezo au mbinu utakayotumia kumshinda
adui.
Unaweza
ukawa unajua mbinu nyingi sana za kumshinda adui lakini Mungu anataka
umsikilize yeye kwa sababu Mungu yeye ni Bwana wa vita, anajua ni mbinu ipi
uitumie saa hiyo unapigana kwenye vita yako au kwenye hali yako.
NB: Ni muhimu sana kusikiliza
maelekezo ya Mungu anayokupa hata kama ndani mwako unajua kuwa unafahamu namna
ya kutoka kwenye shida uliyo nayo.
Haiingii
akilini jeshi la watu 300 kupambana na jeshi lenye watu kama mchanga wa
ufukweni halafu wategemee kushinda. Ni lazima Mungu mwenyewe ahusike. Njia za
Mungu si sawa na njia za mwanadamu, na mawazo ya Mungu si sawa na mawazo ya
mwanadamu.
Kwa
nini Mungu anataka umsikilize kwanza? Ni kwa sababu anafanya mambo yake yote
kwa utukufu wake- yaani anafanya hayo ili ajitwalie utukufu. Kwa hiyo ukifanya
chochote ili ujitukuze mwenyewe, utainua vita na Mungu mwenyewe ambayo hakuna
anayeweza kukusaidia. (Mungu hampi yeyote utukufu wake).
Pia
unaweza ukasoma habari za kuanguka kwa ukuta wa mji wa Yeriko katika Yoshua 6: 1 – 16
3. Unapata
kufahamu chanzo au asili ya tatizo unaloliombea.
2 Samweli 21: 1 – 2 – 14
Hapa
tunaona habari ya Mfalme Daudi katika kipindi chake kulitukia njaa ambayo
ilidumu kwa muda wa miaka mitatu, na Biblia inasema ilikuwa mwaka kwa mwaka.
Ndipo Daudi akautafuta uso Bwana na Bwana akamjibu.
Biblia
haijaweka wazi mfalme Daudi aliomba maombi ya namna gani lakini tunaona kile
alichomjibu Bwana. Bwana alimjibu “ni kwa sababu ya Sauli alivyowaua
Wagibeoni”.
-
Lile
neno “ni kwa sababu ya” linaonyesha kuwa Daudi aliomba kujua chanzo cha ile
njaa. Ni sawa na kwamba aliomba “kwa nini njaa imekuja juu ya nchi yake”.
-
Jibu
la Munngu kwa Daudi halikuondoa njaa iliyokuwa juu ya nchi bali lilimpa kujua
chanzo cha njaa ile au sababu ya kuwepo kwa njaa ile.
-
Kulikuwa
hakuna namna yoyote ile ya ile njaa kuondoka isipokuwa kushughulikia chanzo
chake.
Wakati
mwingine unaweza ukawa unaombea jambo Fulani lakini Mungu akakusemesha kitu
tofauti na jambo unaloliombea. Halafu unashangaa.
-
Kumbe
Mungu anakuonyesha chanzo cha tatizo lako na halitaondoka mpaka umeshughulika
na chanzo hicho.
-
Tusikimbilie
tu kukemea tukidhani kila tatizo tunalopitia limesababishwa na Shetani kumbe
mengine ni adhabu kutokana na kosa lililofanyika huko nyuma.
Kipindi
kile cha Daudi hakukuwa na damu ya Yesu ndio maana iliwabidi walipize kisasi
ili kuondoa chanzo cha tatizo la njaa ile lakini sisi tunayo damu ya Yesu
inayonena mema kuliko damu za watu, wanyama na hata ndege.
Hebu
fikiria Daudi kaka mwaka wa kwanza anaona njaa haiondoki, mwaka wa pili bado
tu, unafika mwaka wa tatu ndio anaamua kuutafuta uso wa Bwana.
-
Maana
yake ameacha kuomba kwamba Mungu aiondoe njaa bali anaomba kujua chanzo cha
njaa ni nini.
-
Usifikiri
Biblia inaposema mwaka kwa mwaka kwamba Daudi alikuwa haombi, alikuwa anaomba.
Lakini alipoona hakuna mabadiliko yoyote ilibidi abadilishe prayer point.
-
Mwaka
wa kwanza Daudi anaomba lakini hatuoni Mungu akijibu chochote na mwaka wa pili
vivyo hivyo, lakini mwaka wa tatu Mungu anajibu.
NB:
Hebu kaa utafakari ni kitu gani ambacho Mungu amekuwa akikuonyesha au
akikusemesha lakini huelewi wala hujui?
-
Kwa
sababu wengi wamekwama mahali na hawajasogea mbele kwa muda mrefu wakidhani
kuwa Mungu hajawajibu maombi yao kumbe ni wao hawajamsikiliza Mungu kwa makini
ili kupata maelekezo ya kufanyia kazi.
Ukishindwa
kusikiliza sauti ya Mungu inayosema nawe ndani yako utashindwa kuvuka mahali pa
kubwa sana katika viwango vya kumjua Mungu kwenye maisha yako.
HASARA ZA KUTOISIKILIZA
SAUTI YA MUNGU
1. Kukosa
kibali mbele za Mungu.
1 Samweli 15: 1 – 9, 10 -22 – 23
Kumb:
utii ni bora kuliko dhabihu.
2. Kukosa
mbaraka wa Mungu
Kumb 28: 15 –
Laana
ni kutofikia uwezo wa nguvu zako.
NAWEZAJE KUISIKIA SAUTI
YA MUNGU?
1. Jenga
na kudumisha mahusiano mazuri na Roho mtakatifu
1Wakorinto 2:10 inasema ‘Lakini Mungu
ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu…
vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu’
2. Ongeza ufahamu wa viashiria (signal) vya mawasiliano kati
yako na Mungu
Biblia katika 1Samweli
3:9 inasema ‘… Enenda, kalale, itakauwa AKIKUITA, utasema, Nena,
BWANA; kwa kuwa mtumishi wako anasikia…’ Jambo ninalotaka ulijue hapa ni kwamba
Mungu ana njia nyingi za KUITA, naam anaweza kukuita kwa sauti itokayo kinywani
pake au KWA NJIA KUKULETEA ALAMA/VIASHIRIA VYENYE KUKUFANYA UJUE MUNGU
ANANIITA. Kama ilivyo kwa jinsi ya kibinadamu anayekuita si lazima aongee,
anaweza kutumia alama za mikono au hata maandishi nk, kukuita. Katika kukuita
kwa njia ya viashiria/alama Mungu anaweza kuleta
nguvu/msisimuko/ubaridi/maumivu fulani kwenye sehemu ya mwili wako au huzuni
moyoni mwako kama ishara/kiashiria cha uwepo wake juu yako na hivyo
KUTAFUTA/KUTAKA USIKIVU WAKO ILI ASEME NAWE. Hivyo ni lazima uwe na ufahamu na
utafute kujua kuhusu alama/namna ya kwako ambayo Mungu hutumia kutafuta usikivu
wako.
3.
Ni lazima ujue
kutofautisha sauti ya Mungu na sauti nyingine
Hili ni muhimu sana kwako kulielewa ili usije
ukaipuuza sauti ya Mungu kwa kudhani ni mawazo yako au ni ya Shetani au usije
ukatekeleza jambo ukiamini kwamba Mungu amesema nawe kumbe Shetani ndiye
alisema nawe.
Katika
1 Samweli 3:7 imeandikwa ‘Basi Samweli alikuwa hamjui BWANA
bado, na neno la BWANA lilikuwa bado halijafunuliwa kwake’. Andiko hili
linatuonyesha makosa aliyofanya kijana Samweli katika kuielewa sauti ya Mungu
akiichanganya na babu yake Kuhani Eli. Ni muhimu ukaelewa kwamba Mungu anaweza
kusema na wewe hata kama uko katikati ya mkutano wa watu wenye kelele nyingi
sana. Hii ni kwa sababu Mungu hatumii mdomo kusema nasi bali
anatumia moyo wako kuzungumza. Moyo ndio kiungo muhimu cha mawasiliano kati ya
mtu na Mungu.
No comments:
Post a Comment