Msisitizo wa somo hili ni kuweka ndani yako kiu ya kutaka kupata msaada wa Kimungu kwa ajili ya kukufanikisha kwenye malengo uliyo nayo.
Uko upako
maalumu ambao tunauita upako wa maandalizi ambao kazi yake kubwa ni kumuandaa
mtu kwa ajili ya kufikia au kutimiza kusudi la Mungu alilolibeba kwenye maisha
yake.
Inawezekana
mtu huyo pia akaw amebeba kipawa cha uongozi ndani yake, hivyo akandaliwa kuwa
kiongozi wa baadae kwenye nafasi yoyote ile kama vile uongozi wa kwenye
familia, au kanisa au jamii yake au taifa.
Hivyo tambua
kwamba Mungu wetu ni wa upendo ndio maana anakupa kipindi cha maandalizi ya
kukabiliana na huo msimu mpya unaouendea.
1 Samweli 16 : 1 – 11 – 13
Kwenye hii
mistari tunaona namna nabii Samweli amekwenda kwenye nyumba ya Yese na kumpaka
mafuta Daudi kwa ajili ya kuonyesha kuwa Bwana amemchagua kuja kuwa mfalme wa
Israel baada ya mfalme aliyekuwepo wakati huo ambaye ni mfalme Sauli.
-
Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Daudi
kupakwa mafuta ili baadae aje kuwa mfalme.
Kumbuka
kwamba: Daudi alipakwa mafuta mara tatu:
i.
Mara ya kwanza: 1 Samweli 16 : 13
ii.
Mara ya pili: 2 Samweli 2 : 4
iii.
Mara ya tatu: 2 Samweli 5 : 1 – 3
Nataka tuone jambo hapa:
Daudi
alipopakwa mafuta ile mara ya pili alikuwa mfalme wa Yuda, na alipopakwa mafuta
ile mara ya tatu akawa mfalme juu ya Israel wote, swali linakuja pale
alipopakwa mafuta kwa mara ya kwanza ili kuwa ni kwa jili ya nini?
-
Alipopakwa mafuta ile mara ya kwanza Biblia
inasema Roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile.
Kwa nini roho ya Bwana ilimjia Daudi siku ile aliyopakwa mafuta
kwa mara ya kwanza?
Mithali 29 : 18a – pasipo
maono watu huacha kujizuia
-
Lile tukio la Daudi kupakwa mafuta
lilimjulisha yeye mwenyewe juu ya kile kitakachotokea baadaye kwenye maisha
yake, ya kwamba atakuja kuwa mfalme juu ya Israel. Hayo maono yakaingia moyoni
mwake.
-
Sasa ili maono hayo yatimie, ni lazima
ujifunze kujizuia. (Kujizuia maana yake
ni kufanya unachotakiwa kufanya na kutofanya usichotakiwa kufanya – self
control. Kujizuia huko kunaendana na maono uliyobeba)
-
Ndio maana ilibidi Mungu aachilie upako juu
yake wa kumsaidia kujizuia.
Na hapo
tunaona kabisa ya kwamba tangu amepakwa mafuta ile kwa mara ya kwanza ilipita
miaka mingi ndipo akaja kupakwa mafuta mara ya pili na ya tatu kwa ajili ya
kuwa mfalme wa Israel.
-
Ukisoma vizuri Biblia utagundua kuwa pale
alivyopakwa mafuta kwa mara ya kwanza hakuwa mfalme pale pale bali aliendelea
kuchunga kondoo wa baba yake.
1 Samweli 17 : 15
-
Na tunaona pia kwamba roho ya Bwana
iliyomjilia Daudi ndiye Yule yule roho ya Bwana iliyomwacha mfalme Sauli
-
Hapo ndipo utajua kuwa Mungu alikuwa
anamwandaa Daudi kwa ajili ya uongozi au utumishi uliokuwa mbele yake.
KAZI YA UPAKO WA MAANDALIZI NDANI
YA MTU
a.
Kukuandaa
kifikra juu ya mabadiliko ya kimazingira ya kazi unayokwenda kukutana nayo
Daudi
alikuwa ni mchunga kondoo wa baba yake, hivyo akili yake muda wote ilikuwa
inawaza mambo ya kondoo. Haikuwa rahisi sana kwake kubadilika kwa haraka
kimtazamo wa kuwa kiongozi juu ya watu.
Kuwa
kiongozi ni swala la kubeba jukumu kubwa zaidi kuliko kuwa mchunga kondoo.
Ilibidi Mungu aingilie kati kwa kuachilia upako juu yake ambao utamsaidia
kubadilisha mtazamo wake.
Zaburi 78 : 70 – 72 “akamchagua
Daudi mtumishi wake, akamwondoa katika mazizi ya kondoo …., akamweka ili
awachunge wana wa Israel. ”
Kwa hiyo
upako uliokuja juu ya Daudi ulimsaidia kubadilisha mtazamo wa kuchunga kondoo
na kwenda kuchunga wana wa Israel.
-
Mungu alikuwa anajua huyu mtu anahitaji
msaada wa kufanya maandalizi mapema ili aweze kusimama katika nafasi yake kwa
uaminifu.
-
Mabadiliko ya nyakati au msimu kwenye maisha
yako yanahitaji sana mabadiliko kwenye fikra na sio kwenye roho. Hii ni kwa
sababu eneo la maamuzi ndani yako sio rohoni mwako bali ni kwenye akili yako.
-
Mchakato wa kumbadilisha Daudi kifikra
ulihitaji masaada wa nguvu za Roho Mtakatifu ndio maana akapakwa mafuta mapema
sana wakati mfalme aliyekuwa anatawala bado yuko madarakani.
-
Mungu anajua kabisa kuwa unahitaji msaada
katika hatua hiyo ya mabadiliko ndio maana anaachilia upako huo wa maandalizi
ndani yako mapema ili ukuandae kwa hatua hiyo.
Kimsingi ni
kwamba pale tu Daudi alipopakwa mafuta ili kuwa mfalme basi Yule mfalme
aliyekuwepo madarakani hakuwa na kazi tena. Ni sawa na kumchagua rais mwingine
wakati kuna rais aliyepo madarakani.
-
Lakini Mungu aliamua Daudi aendelee kujifunza
na kujijenga kifikra juu ya nafasi ya kuwa mfalme wa Israel.
-
Upako wa Roho Mt juu yake ulihakikisha Daudi
anafahamu maswala ya kiuongozi ya kitaifa ambayo ni tofauti na kuchunga kondoo
ndio maana ilibidi Mungu amtengenezee njia ya kwenda ikulu kwa mfalme Sauli
mara kwa mara.
Vijana wengi
wana imani juu ya Mungu wao kuwa anaweza akawafanikisha na kufikia katika
malengo yao lakini mitazamo yao bado haijawa tayari kukabiliana na mazingira
hayo.
-
Na ndio maana ni rahisi sana kwao kuachia
safari njiani pale wanapokutana na changamoto ngumu wakati wakielekea kutimiza
ndoto zao au maono yao.
b.
Kushughulikia
hofu inayokukwamisha kuingia msimu mpya
Mtu anaweza
akawa na hofu ya kufanya jambo fulani
jipya au hofu ya kuingia msimu mpya hivyo ukakwama kuona mabadiliko kwenye maisha
yako.
1 Samweli 17 : 1 – 2, 8 – 11, 31 – 37
Jambo la
ajabu hapa ni kwamba hivi vita vya Israeli na Wafilisti vilitokea baada ya
Daudi kupakwa mafuta ile mara ya kwanza.
-
Kila mtu kwenye taifa la Israel aliogopa
kwenda kupigana na Goliathi hata mfalme Sauli aliogopa, hata majemedari wa vita
pia waliogopa kwenda kupigana na Goliathi isipokuwa Daudi peke yake ndiye
aliyekuwa na ujasiri wa kwenda kupigana.
-
Hivi vita vinatokea mara baada ya Daudi
kupakwa mafuta. Na hii ni wazi kwamba hata Daudi mwenyewe angeogopa kwenda
kupigana na Yule Goliathi, lakini kwa sababu upako wa RohoMtakatifu ulikuwa juu
yake basi akapokea nguvu na ujasiri wa kwenda kupigana na Yule Mfilisti.
-
Hicho ndicho kilichomtofautisha Daudi na wana
wa Israel wote, ya kwamba yeye peke yake hakuwa muoga wa kwenda kupigana na
Goliathi.
Kile kitabu
cha Matendo 1 : 8 – “mtapokea nguvu
akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu”
Wale mitume
wa Bwana Yesu kabla hawajampokea Roho Mt walikuwa hawana ujasiri wa kwenda
kuhubiri Neno la Mungu kwa watu, lakini baada ya kupokea nguvu juu yao wakapata
ujasiri, hawakuogopa tena hata kama wangepitia mateso na kuuawa.
-
Kwa hiyo hata kile kipindi cha Daudi
alipopakwa mafuta, alipokea nguvu za Roho Mt juu yake zilizoshughulikia hofu
ndani yake ambapo hizo nguvu hazikuwepo kwa Mwisrael yeyote wa kipindi kile
ndio maana bado Waisrael walikuwa na hofu ya kwenda kupigana na Goliathi lakini
Daudi peke yake akawa na ujasiri.
-
Na ukumbuke pia ya kwamba Roho ya Bwana
iliyomwacha mfalme Sauli ndiye Roho Yule yule aliyekuja juu ya Daudi, hivyo
ujasiri ukatoka ndani ya Sauli ukaenda kwa Daudi.
Na hivi
ndivyo ilivyo hata katika maisha ya vijana wengi wa sasa, wameshindwa kusonga
mbele kwa sababu ya hofu iliyopo ndani yao ya kujaribu kuanza biashara, au hofu
ya kuwa viongozi, hofu ya kusimamia misimamo ya mipango waliyonayo, na hata wengine
wana hofu ya kuoa au kuolewa wakiogopa wenzi wao wanaweza wakawaumiza kwa
kuwaacha au kuwatenda vibaya.
-
Hofu ni mojawapo ya silaha kubwa ya Shetani
anayoitumia kuwapigia watumishi wa Mungu na hasa vijana ili wasifanikishe
malengo waliyonayo.
-
Hofu ikiwepo ndani yako basi ujue kuwa imani
haipo. Ndio maana waoga watakwenda motoni kwa sababu uoga/hofu inaitoa nje
imani.
-
Wengine wameshindwa kuanzisha hata biashara
kwa sababu ya kuogopa kupata hasara
-
Kwa hiyo, kuanzia sasa usiruhu hofu ikatawala
ndani yako.
Upako wa
Roho Mtakatifu juu yako utashughulikia kuondoa hofu hiyo ndani yako.
c.
Kukusaidia
kuchagua aina ya marafiki au washauri watakaoendana na maono uliyobeba
1 Samweli 18 : 1 – 5
“roho ya
Yonathani ikaambatana na roho ya Daudi”
-
Mungu aliamua kumtengenezea Daudi aina ya
marafiki ambao wangemsaidia kufikia malengo au maono aliyokuwa nayo.
-
Tunajua ya kuwa Daudi alikuwa na marafiki
wengi alipokuwa anakaa kwa baba yake lakini hatuoni wakitajwa hata mmoja, sasa
haimaanishi walikuwa ni wabaya bali inawezekana walikuwa hawana cha kumsaidia
kufikia kwenye malengo aliyokuwa nayo. Na ndio maana Mungu aliamua kumkutanisha
na marafiki wengine watakaomsaidia kufikia hatima yake (wakina Yonathani na
watu wa vita wa mfalme Sauli)
Kuna hatua
kwenye maisha yako utafika ambapo Mungu hatokuruhusu uendelee kuwa na aina ya
marafiki ulionao, sio kwa sababu Mungu amewachukia bali ni kwa sababu hawawezi
kukusaidia kufikia maono uliyo nayo
-
Sio kila mtu utakayekutana naye anafaa kuwa
rafiki yako. Wengine wataletwa na shetani kwa ajili ya kuua maono yako. Hawana
mawazo ya kukusaidia bali wanakupa ushauri wa kukukandamiza ili ujione kuwa
huwezi kitu.
Linapofika
swala la kuchagua marafiki utakaoambatana nao sio swala la kwako kuchagua bali
ni la Mungu kukusaidia kutambua aina ya marafiki wa kuwa nawe.
-
Urafiki ni jambo la kiroho kabla ya kuwa la
kimwili. 1 Samweli 18: 1 - inasema
“roho ya Yonathani iliambatana na roho ya Daudi”
-
Tafsiri yake ni kwamba, roho zao ziliungana
kwa sababu zilipatana na kupendana.
-
Kwa hiyo urafiki wao, msingi wake haukuwa
mwilini bali rohoni.
-
Na ndio maana watu wengi ni rahisi sana
kuumizwa na marafiki zao, au ni rahisi sana kuwaamini marafiki zao kutokana na
misingi ya urafiki wao ambao ni rohoni.
-
Hivyo ni muhimu sana kumshirikisha Mungu
kwanza kabla hatujachagua marafiki kwenye maisha yetu.
Wagalatia 2 : 9 – mtume
Paulo alipewa mkono wa shirika na wale mitume wakubwa.
-
Maana yake ni kwamba walimpa support kwenye
huduma yake.
-
Kuna watu Mungu atakukutanisha nao ili wakupe
mkono wa shirika. Japo kuna watu wengine yamkini hata watumishi wa Mungu
utakutana nao lakini watakupinga, hawatakupa mkono wa shirika.
d.
Kukusaidia
kuwa na utulivu moyoni mwako pindi utakapopita katika mazingira magumu.
Hakuna
anayezoea au anayependa kupitia mazingira magumu kwenye maisha yake. Lakini inapotokea ukapita kwenye mazingira
hayo magumu kwa ajili ya kule unapoelekea basi ni wazi kabisa kuwa Mungu
anahitaji uwe na utulivu moyoni mwako ili umsikilize Yeye akuongoze namna ya
kuvuka kwenye hayo mazingira bila kutegemea akili zako mwenyewe.
-
Vijana wengi tunakwama njiani inapotokea
tunapitia mazingira magumu kwa sababu tunadhani mazingira yote magumu
tunayoyapitia yameletwa na adui shetani, kwa hiyo tunashughulika nayo zaidi kwa
kutumia akili zetu pekee bila kumshirikisha Mungu kwanza.
-
Upako wa maandalizi unakusaidia kutulia na
kumwacha Mungu mwenyewe akupiganie.
-
Na ndio maana mara nyingi unapopita kwenye
changamoto kama hizo unajikuta unaomba halafu badala Mungu kushughulika na
tatizo lako, Yeye anashughulika na hali ya moyo wako. Kwa sababu hali ya moyo
wako ni ya muhimu sana kukaa sawa katika kipindi hicho cha maandalizi ili
kumruhusu Mungu kukuvusha katika mazingira hayo.
Zaburi 77 : 1 – 13
Hayo ni
maombi ya Daudi wakati ule anapitia katika hali ngumu ya kumkimbia mfalme
Sauli.
-
Upako uliokuwa juu ya Daudi haukumbadilishia
mazingira aliyokuwa anayapitia bali ulimbadilisha hali ya moyo wake
anavyojitazama; yaani nguvu za Mungu zilimbadilisha namna anavyomuona Mungu.
NB: Inawezekana unapita mahali pagumu zaidi, na
Mungu anajua kuwa unapita mahali pagumu lakini Mungu anashughulika na hali ya
moyo wako na sio mazingira unayopitia kwa sababu anajua mpango alionao kwa
ajili yako ni mpango wa kukufanikisha na sio wakukukwamisha. Yeremia 29 : 11
Katika
kukupa utulivu moyoni mwako ni lazima upako huo wa maandalizi utashughulikia
tabia ya kusamehe ndani yako.
-
Ndani ya moyo wako kama ni vigumu kumsamehe
mtu aliyekukosea basi Mungu atashughulikia hali hiyo kwa sababu kutokusamehe ni
kikwazo kimojawapo cha kuwakwamisha watu wasifikie malengo yao.
-
Kutokusamehe kunamfanya mtu aache “ku-focus”
kwenye malengo yake na badala yake huyo mtu anaanza “ku-focus” namna ya
kulipiza kisasi juu ya watu waliomkosea.
Katika kila
hali unayopitia liko Neno la Bwana la kukusaidia kuvuka hapo, kwa hiyo ni
muhimu sana kukawa na utulivu moyoni mwako ili uweze kusikia kile
atakachokuambia Yesu ili ukifanye.
Biblia
inasema Imani chanzo chake ni kusikia, kusikia Neno la Kristo, hivyo ili uwe na
imani ya kushinda magumu unayopitia ni lazima ujifunze kusikia kwanza Neno la
Kristo ndipo imani ijengeke ndani mwako.
MUNGU AKUJALIE KUWEZA KUISHI KWA KUTIMIZA KUSUDI LAKE.
No comments:
Post a Comment