Msisitizo wa somo hili ni kuandaa wanamaombi watakao simama sawasawa katika nafasi zao za maombi.
Utangulizi:
Mtu unapookoka unapata kurejeshwa
kwenye nafasi au mamlaka uliyokuwa umeipoteza hapo awali. Baadhi ya nafasi hizo
ni pamoja na unakuwa mtoto wa Mungu, kuhani kwa Mungu, mtenda kazi pamoja na
Mungu, raia wa ufalme wa Mungu, n.k.
Yohana 1 : 12 – Wote waliompokea
aliwapa uwezo wa kufanyika kuwa wana wa Mungu
Ufunuo 5 : 9 – Ukamnunulia
Mungu kwa damu yako… ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu.
Usije ukaidharau hii nafasi kwa sababu
kupatikana kwake ni kutokana na damu ya Yesu.
Nafasi ya kikuhani ni nafasi ya kimaombi. Kwa hiyo kama Mungu
ameturejeshea nafasi hiyo basi ni dhahiri kuwa anataka tuitumie, na kwa sababu
hiyo ni ya muhimu kuifahamu ili tuitumie vizuri.
Sasa leo nataka tuangalie nafasi ya kikuhani ndani ya watu wa Mungu.
-
Kuhani ni nafasi anayopewa mtu anapookoka, ili
aende mbele za Mungu kwa ajili ya kuomba juu ya nafsi yake na kwa ajili ya
wengine. Waebrania 5 : 1 - 4
-
Ni nafasi tuliyorejeshewa kwa njia ya Damu ya
Yesu iliyomwagika pale msalabani. Ufunuo
5 : 9
-
Pale msalabani si tu kwamba tulikombolewa kutoka
kwenye hali ya utumwa wa dhambi bali pia tulirejeshewa nafasi tulizokuwa
tumepoteza tangu mwanadamu alipomwasi Mungu.
-
Na kupotea kwa hizo nafasi ndani ya mwanadamu
mbele za Mungu zilikwamisha kwa kiwango kikubwa mahusiano baina ya Mungu na
mwanadamu.
-
Ukumbuke kuwa pale tu mwanadamu alipomwasi Mungu
automatically mwanadamu alipoteza nafasi zote alizokuwa nazo mbele za Mungu
(ndio maana Mungu alimuuliza Adamu “uko
wapi” [Mwanzo 3 : 9] sio kwamba
alikuwa hamuoni Adamu bali hakumuona kwenye nafasi aliyokuwa amemweka).
Nafasi ndio inayokupa hadhi (heshima) pale unapoitumia.
-
Maneno utakayoongea ukiwa na nafasi ya urais hayana
hadhi sawa na ukiyaongea maneno yale yale ukiwa nje na nafasi hiyo ya urais.
-
Kinachompa nguvu rais si yeye kama mtu bali ni
cheo cha urais alichonacho kwa wakati ule. Muda ukiisha wa yeye kuwa rais
anabaki kuwa ni mtu yule yule lakini hana tena nafasi ya urais, kwa hiyo nguvu
inayotokana na nafasi ya urais pia inaondoka. Kwa mfano: rais mstaafu Kikwete
akiongea sasa juu ya nchi, maneno yake hayana nguvu sawa na kipindi kile
alipokuwa ni raisi wa nchi, sio kwa sababu tumemdharau bali ni kwa sababu
hayuko tena katika kiti cha urais.
-
Sio watu wengi wanafuatilia pale rais mpya
anapoapishwa halafu unaona mlinzi wa rais anahama kutoka kwa rais anayemaliza
muda wake na anakwenda kwa rais aliyeingia madarakani. Hii inaonyesha kuwa
mamlaka yamehama kutoka kwa rais aliyemaliza kuja kwa rais mpya.
-
Kinacholeta heshima na uzito wa maneno si mtu
bali ni cheo au nafasi.
-
Kwa hiyo ukiwa unajua kuitumia vizuri nafasi
yako ya kikuhani basi utaona mambo makubwa Mungu atakayotenda kwa kupitia
maombi yako.
Historia fupi ya nafsi ya kikuhani juu ya taifa la Israeli.
-
Kipindi cha torati ya Musa kulikuwa na utaratibu
wa kwamba ni lazima Kuhani mkuu tu ndiye mwenye ruhusa ya kuingia patakatifu
kwa ajili ya kupeleka dhambi zake mwenyewe na dhambi za taifa zima. Na ilikuwa
ni desturi ya jambo hilo kufanyika kila mwaka mara moja tu. Kutoka 26 : 31 – 33 na Waebrania 9 : 25.
-
Kipindi cha neema hasa kuanzia pale kusulubishwa
kwa Yesu msalabani kulileta mabadiliko ya utaratibu wa kupaingia patakatifu pa
patakatifu. Wakati yesu anasulubiwa kulitokea kupasuka kwa pazia la hekalu, hii
ilikuwa ni kuashiria kwamba sasa kila mtu anayofursa na nafasi ya kwenye mbele
za Mungu moja kwa moja kwa njia ya damu ya Yesu. Luka 23 : 45 na Waebrania 10
: 19 – 22
Kwa hiyo ni haki ya kila mtu
aliyeokoka kwenda mbele za Mungu kama kuhani na kuomba chochote.
NB: Unapokwenda mbele za Mungu kama Mwana utasikilizwa kama Mwana, na
utakapokwenda mbele za Mungu kama kuhani utasikilizwa kama kuhani. Ebrania 5 :
7 - 8
-
Mwana ni mrithi wa yote lakini Kuhani ni mpole
na mtiifu.
-
Mwana ni mtawala bali kuhani ni muombaji, mnyenyekevu
anayejua kushuka na kutii.
-
Ni muhimu ukajua unakwenda kwa nafasi gani mbele
za Mungu. Kwa sababu ile nafasi ndio inayotoa uzito wa hayo maombi unayoomba
mbele za Mungu.
Hebu fikiria
kwa mfano; raisi wa nchi Fulani anapokuja hapa nchini kwetu atapokelewa na
mwenyeji wake ambaye ni raisi wa nchi yetu, na hivyo hivyo akija Waziri wa nchi
nyingine hapa ni lazima atapokelewa na waziri wa hapa nchini kwetu.
Kinachosababisha hali hiyo ni hadhi ya nafasi walizo nazo.
-
Nguvu za sauti zao zipo kwenye nafasi zao
-
Yesu alipoomba juu ya kifo chake na namna ya
kuwakomboa wanadamu, hakwenda mbele za Mungu Baba kama Mwana bali alikwenda
kama Kuhani mkuu na ndio maana alibeba dhambi zetu pale msalabani.
-
Pale kwenye kitabu cha Waebrania 5 anaposema ”akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha
Mungu, na ingawa ni Mwana alijifunza kutii kwa mateso”= hii inaonyesha
kwamba nafasi aliyokwenda nayo Yesu mbele za Mungu si Mwana bali Kuhani mkuu.
Nafasi ya Kikuhani inakupa uhalali wa kubeba dhambi za wengine na kuzipeleka
mbele za Mungu.
Lakini pia ndani ya hii nafasi ya kikuhani kuna jambo jingine la kufahamu
ambalo ni la msingi sana.
ü Ufunuo 5 : 10 – Ukawafanya kuwa ufalme na makuhani
-
Hapa Yesu Kristo alifanya nafasi ya ufalme kama
“taifa” na nafasi ya makuhani kama “ waombaji”
ü 1 Petro 2 : 9 – Ukuhani wa kifalme
-
Nchi zinazoongozwa na wafalme, hao wafalme neno
lao ndio sheria, maana yake wanatoa maamuzi kwa maneno yao.
-
Kwa hiyo ukuhani wa kifalme ni waombaji
wanaoweza kutoa maamuzi kwa njia ya maneno wanayotamka wanapoomba.
-
Hivyo neno la mwanamaombi huyo ndio linakuwa na
maamuzi ya mwisho (final say) juu ya mahali pale unapopaombea.
-
Ukiamua paharibike basi pataharibika na ukiamua
parekebishwe basi patarekebishwa. Mfano : Ibrahimu alipopata nafasi ya kuombea
miji ya Sodoma na Gomora – Mwanzo 18: 23
– 33
Wafalme wanatawala kwa maneno
bali makuhani wanatawala kwa maombi.
ü Kutoka 19 : 5 – 6 – Ufalme wa makuhani
-
Tafsiri yake ni kwamba Mungu aliamua
ajitengenezee taifa ambao watakuwa ni waombaji. Ndio maana kila mtu anayeokoka automatically
anakuwa ni kuhani katika ufalme wa Mungu.
Kwa hiyo fahamu kuwa nafasi ya
ukuhani ni nafasi ambayo ilikuwepo kwenye mpango wa Mungu wa kumwokoa mwanadamu
kwa kupitia damu ya Yesu hivyo ina thamani kubwa sana kama tutajua namna ya
kuitumia ipasavyo.
Maombi ni sawa na chakula cha
kiroho kwa mtu yeyote aliyeokoka, hayaepukiki.
-
Ukitaka kuwa na mahusiano mazuri na Mungu wako
ni lazima uwe na tabia ya maombi maishani mwako.
-
Maombi yanajenga mahusiano mazuri kati yako na
Mungu.
-
Maombi ni mojawapo ya njia anayotumia Mungu
kuzungumza na watu wake na pia ni njia anayotumia mtu kuwasiliana na Mungu
wake.
- Lakini pia maombi ni njia mojawapo ya kutawala katika ulimwengu wa roho (Ufunuo 5 : 10 – “nao wanamiliki juu ya nchi”).
Kuna aina mbali mbali za waombaji ambao Mungu amewaweka hapa duniani.
1.
Waombaji
walinzi
Isaya 62 : 6 – 7 – tazama nimeweka walinzi juu ya kuta zako ee
Yerusalemu hawatanyamaza usiku wala mchana…
Hawa ni waombaji wenye kazi ya
kulinda kusudi la Mungu juu ya mahali Fulani wanapopaombea.
-
Wamesimama kama walinzi. Wao ndio wanaoruhusu
jambo Fulani lipite au lisipite katika ulimwengu wa roho.
-
Daniel 4
: 17 – hukumu hii imekuja kwa agizo la walinzi na amri hii kwa neno la
watakatifu…
-
kwa hiyo waombaji wa aina hii wanao uwezo wa kutoa
maamuzi juu ya maeneo yao wanayoyaombea.
2.
Waombaji
watengenezaji
Ezekiel 22 : 30 – nami nikatafuta mtu miongoni mwao
atakayelitengeneza boma na kusimama mahali palipobomoka
-
Hawa ni waombaji ambao wapo kwa ajili ya
kurejesha mahusiano yaliyoharibika kati ya Mungu na watu wa mahali Fulani.
Mfano nabii Eliya alijenga madhabahu ya Bwana iliyovunjika 1 Wafalme 18 : 30. Kipindi hiki cha nabii Eliya kulikuwa hakuna
mahusiano mazuri kati ya Mungu na taifa la Israeli kwa sababu Israeli walikuwa
wanamtumikia mungu Baali. Hivyo Eliya alikuja kwa ajili ya kurejesha mahusiano
yaliyopotea.
3.
Waombaji
wazalishaji
Wagalatia 4 : 19 – Vitoto vyangu navionea utungu mpaka Kristo
aumbike tena ndani yao.
-
Pia hawa ni wanamaombi wenye mzigo wa kuwaombea
watu ambao ni wachanga kiroho ili wakue kiroho wasitetereke na kurudi nyuma.
-
Hii inamaana kuwa sio kwamba tunaishia kuwaombea
watu waokoke halafu tunawaacha bali tunatakiwa pia tuwaombee mpaka wakue kiroho
waweze kujisimamia wenyewe.
-
Unapokwenda kumhubiria mtu aokoke kumbuka kuwa
unawajibu pia wa kumuombea ili akue kiroho.
-
Mtume Paulo aliwahubiria watu wakaokoka lakini
baada ya muda wale watu wakarudi nyuma, ikambidi aanze tena kuwaombea mpaka
Kristo aumbike tena ndani yao.
KWA NINI TUNATAKIWA KUOMBA?
a.
Mwanamaombi
ndiye mtu mwenye maamuzi ya mwisho juu ya hali ya kimwili na ya kiroho ya
mahali anapotakiwa kupaombea.
Mathayo 16 : 19; 18 : 18 – 20
-
Mbingu zinakusikiliza wewe unaomba nini.
-
Unapoombea taifa lako au kanisa lako au familia
yako, ni wewe ndiye unayeamua nini kifanyike juu ya mahali hapo unapopaombea.
-
Utakachokiomba ndicho kitakachofanyika
-
Kumbuka: Muombaji anatawala kwa njia ya neno
lake (maombi anayoomba) kama vile ilivyo kwa mfalme anavyotawala kwa njia neno
lake. Neno la mfalme ni sheria.
b.
Nguvu
za kutengeneza majibu juu ya maswali au matatizo au mazingira magumu
tunayokutana nayo hapa duniani ipo ndani yetu.
Waefeso 3 : 20
-
Unapoomba ndipo unaachilia nguvu za kutengeneza
majibu ya hayo mambo unayopitia.
-
Tafsiri yake ni kwamba usipoomba basi utaendelea
kupata shida mwenyewe wakati uwezo wa kutoka kwenye hiyo shida upo ndani yako.
c.
Maombi
yanatusaidia kutokuingia majaribuni
Mathayo 26 : 41- kesheni mwombe msije
mkaingia majaribuni
-
Kuna mazingira magumu ambayo hatupaswi tukutane
nayo kwenye maisha yetu.
-
Hayo mazingira tutayaepuka kwa njia moja tu
ambayo ni maombi, kwa sabau kwenye maombi ndipo utajulishwa na Roho mtakatifu
wapi uende na wapi usiende, au nini ufanye na nini usifanye. Mathayo 2 : 12, 13
d.
Pia
maombi yanatusaidia kupata neema ya kushinda majaribu
Waebrania 4 : 16 – na tukikaribie kiti
cha neema kwa ujasiri…, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.
-
Tafsiri yake ni kwamba kuna neema ya kumsaidia
mtu wa Mungu anapopita kwenye magumu aweze kutunza
uchaji wa Mungu ndani yake bila kumtenda Mungu dhambi
-
Watu wengi wanapopita kwenye shida Fulani kwenye
maisha yao huwa wanapoa kiroho kunakosababishwa na kushuka kwa kiwango chao cha
kumwamini na kumtegemea Mungu
-
Sasa kazi mojawapo ya maombi ni kuhakikisha
kiwango chako cha kumtegemea Mungu kinazidi kuongezeka hata kama unapita kwenye
magumu.
e.
Maombi
ni njia mojawapo anayoitumia Mungu kuwasiliana na watu wake.
Isaya 41 : 21- leteni maneno yenu…,
toeni hoja zenu zenye nguvu…
Isaya 43 : 26 – unikumbushe na
tuhojiane.
-
Unapoona mahali pameandikwa hoja au tuhojiane,
tafsiri yake ni kwamba kuna kuwa na mazungumzo baina ya pande mbili. Na kila
upande unatoa hoja zake.
-
Hayo ndiyo mawasiliano yanayotokea baina ya
pande mbili.
-
Kwa hiyo Mungu anaweza akakusemesha wew pale
unapokuwa katika hali ya maombi, lakini pia wewe unaweza ukamsemesha Mungu
unapokuwa katika maombi.
-
Ukumbuke
kuwa mawasiliano yanatengeneza mahusiano. Mawasiliano yakiwa mazuri basi na
mahusiano yatakuwa mazuri, bali mawasiliano yakiwa mabaya na mahusiano pia
yatakuwa mabaya.
NB: Mungu akusaidie kusimama vizuri
kwenye zamu yako ya maombi kwa kuwa usipoomba wewe hakuna mwingine atakayeomba
kwenye nafasi yako.
No comments:
Post a Comment