Msisitizo wa somo hili ni kukusaidia kujua kwamba Mungu anataka umzalie matunda kwa kupitia karama aua huduma aliyokupa na matunda hayo yapate kukaa (maana yake yadumu)
Watumishi wengi wa Mungu wanaanzisha huduma
mbalimbali lakini baada ya muda mfupi huwasikii tena au wengine wanaacha kabisa
hata utumishi huo kutokana na changamoto mbalimbali wanazopitia.
Sio mapenzi ya Mungu waishie njiani, na
hasa zaidi kama Mungu ndiye mwanzilishi wa huduma zao.
Mungu anataka watu wake wamzalie matunda na
matunda hayo yakae maana yake yadumu. Kama ni uimbaji basi udumu, kama ni
kuhubiri au kufundisha basi udumu kwenye utumishi huo na sio leo umeinuka
halafu kesho umeanguka.
Ø Yohana 15 : 2, 6 – 8, 16
-
Na kila tawi lizaalo
hulisafisha ili lizidi kuzaa.
-
Hivyo hutukuzwa Baba kwa vile
mzaavyo sana
-
Name nikawaweka mwende mkazae
matunda na matunda yenu yapate kukaa.
Kuna
kitu kinachoitwa Mafuta ya Roho Mtakatifu ambayo ni nguvu ya Mungu ndani ya mtu
kwa ajili ya utumishi alionao.
-
Haya mafuta yanaweza yakaondoka
kama hutajua namna ya kuyatunza ili uendelee kumtumikia Mungu kwa viwango vya
Kimungu
-
Kwa lugha nyingine haya mafuta
ya Roho mtakatifu yanaitwa upako.
-
Mfano, unaweza ukaongoza
kipindi cha sifa halafu uwepo wa Mungu ukashuka watu wakaguswa na nguvu za
Mungu wakabadilishwa maisha yao. Kule kushuka kwa nguvu za Mungu wakati
unaongoza sifa ndiko kunaitwa upako. Na mara nyingi huo upako unatoka ndani ya
mtu anayetumika katika utumishi husika, inawezekuwa uimbaji, kuhubiri,
kufundisha, kuombea, n.k
SASA ZIKO SABABU ZINAZOFANYA
WATU WAPOTEZE MAFUTA YA ROHO MT NDANI MWAO
1. Kujisifia
vipawa au karama walizonazo
Yeremia
9 : 23 – 24, 25
-
Bali ajisifuye na ajisifu
kwamba anamfahamu na kumjua Mungu
-
Mwenye hekima asijisifu kwa
sababu ya hekima yake wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake.
-
Mungu anataka tusijisifu kwa
sababu ya vitu au vipawa tulivyonavyo bali tujisifu au tujivunie kwamba tunamjua
Yeye.
Ø Zaburi 20 : 7
-
Hawa wanataja magari na hawa
farasi lakini sisi tutalitaja Jina la Bwana.
-
Huu mstari unaonyesha ni nini
watu wanatumainia wanapokuwa kwenye vita lakini sisi tunatumainia Jina la Bwana
-
Imani yao ipo kwenye vitu wanavyodhani
kwamba vinaweza vikawasaidia bali Biblia inatuonyesha kwamba anayemtumainia
Mungu yeye atataja Jina la Bwana.
Ø Mika 6 : 6 – 8
-
Ee, mwanadamu yeye amekuonyesha
yaliyo mema, na Bwana anataka nini kwako ila kutenda haki, na kupenda rehema na
kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako.
-
Unajua watu wengi wanakimbilia
kwenye utumishi bila kwanza kukaa na kumfahamu Mungu zaidi na kujua anataka
wafanye nini kwenye kazi waliopewa.
-
Kwa mfano, mtu anakipaji cha
uimbaji, sasa anakimbilia kuimba bila hata ya kukaa chini ya uongozi wa Mungu
kwanza na kupokea maelekezo yake ndipo aingie kwenye huo utumishi badala yake
anatumainia uwezo wake wa sauti na ujuzi wa kuimba.
-
Na ndio maana watu wengi
wamepoteza mafuta ya Roho mtakatifu kwenye utumishi wao kwa sababu hiyo.
-
Kwa sababu ukitumia kipawa au
utumishi uliopewa bila kumjua Yeye aliyekupa basi utakuwa unafanya kwa mapenzi
yako badala ya kufanya mapenzi ya Mungu.
·
Hutoweza kumsikiliza Mungu
·
Hutoweza kumtii Mungu
·
Hutoweza kuenenda na Mungu
·
Ndani ya moyo wako utabeba huduma
badala ya kumbeba Yesu.
Mfano wa Yesu kutenda mapenzi ya Mungu na sio mapenzi yake mwenyewe.
-
Yohana 14 : 23 – 24- nalo neon
mnalolisikia silo langu ila ni lake Baba aliyenipeleka
-
Yohana 7 : 16, 17- mafunzo yangu si
yangu mimi, ila ni yake yeye aliyenipeleka
-
Yohana 7 : 18- yeye anenaye kwa nafsi
yake tu hutafuta utukufu wake mwenyewe
Mungu anapokupa huduma au karama yoyote,
anachotaka ni ndani yako kuwe na utii na kusikiliza neno lake linasema nini juu
ya utumishi ulionao
Ø 2Korintho 10 : 17 – 18
-
Mtu mwenye kukubaliwa si yeye
ajisifuye bali ni yeye asifiwaye na Bwana
-
Watu wengi wanadhani huduma
ndizo zinawapa kibali mbele za Mungu, NO, Kumjua Bwana ndio kutakakokupa kibali
2. Kuwa na
michanganyo ya kidunia
Ufunuo
3 : 15 – 18
-
Nayajua matendo yako yakwamba
hu baridi wala hu moto, ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. Basi kwa
sababu una uvuguvugu, nitakutapika utoke katika kinywa changu
-
Kuwa vuguvugu maana yake ni
kuwa na michanganyo yaani kwa Yesu upo na kwa shetani pia upo.
-
Mtu wa michanganyo asitegemee
kabisa kuona nguvu za Mungu zikikaa ndani yake.
-
Unaweza ukabakiwa na kipawa
chako lakini upako wa Mungu haupo juu yako.
Mathayo
6 : 24
-
Hakuna mtu awezaye kutumikia
mabwana wawili. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
-
Anaposema hamwezi kumtumikia
Mungu na mali maana yake ni kwamba kuna namna mali inachukua nafasi ya Mungu
moyoni mwako na inakutumikisha.
-
Kwa hiyo hapo unakuwa na
michanganyo kwa sababu umechanganya mali na Mungu mahali pamoja.
-
Yule utakayemtumikia (Mungu au
mali) ndiye atakayeachilia nguvu zake kwako
1
Yohana 2 : 15 – 17
-
Mtu akiipenda dunia, kumpenda
Baba hakumo ndani yake.
SIFA/ VIASHIRIA (INDICATORS)
VYA WATUMISHI WA MUNGU WALIOPOTEZA MAFUTA YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAO:-
1. Hawana hofu
ya Mungu ndani yao
-
Warumi 1 : 28 – 32
-
Na kama
walivyokataa kuwa na mUngu kwenye fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao
zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa
2. Ni watu
wasiojishusha au wasiojinyenyekeza mbele za Mungu
-
Sio watu wanaotaka tena
kuongozwa na Mungu, wanataka kujiongoza wenyewe.
-
Yohana 14 : 23 – 24 –
mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu
-
1Petro 5 : 6 – Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Bwana...
3. Ni watu
wanaotii huduma zaidi kuliko kumtii Mungu
-
1 Samweli 15 : 1 – 3, 9, 10 – 11, 19 – 23
-
Mbona basi hukutii sauti ya
Bwana, bali ukazirukia nyara ukafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana?
4. Hawana muda
wa kutosha wa maombi na Mungu wao
-
Wanaamini katika uwezo wa
vipawa na huduma zao
-
Hakiwasumbui kama Mungu yupo
pamoja nao au hayupo nao kwenye utumishi wao
-
Kutoka 33 : 15 – 16
5. Hawana muda
wa kutosha wa kusoma na kutafakari neno la Mungu
-
Yoshua 1 : 8-
kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako bali utafakari mchana na
usiku, ukaangalie kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo, maana ndipo
utakapoifanikisha njia yako kasha ndipo utasitawi sana
-
Zaburi 119 : 11 –
moyoni linakaa Neno la Kristo
NB: Ukiskosa neno la Kristo ndani yako
maana yake umekosa kuwa na imani kwa sababu imani chanzo chake ni kusikia, na
kusikia kunatokana na Neno la Kristo (Rumi
10 : 17). Na kama hauna imani ndani yako huwezi ukampendeza Mungu kwa
sababu kila amwendeaye Mungu ni lazima aamini kwamba yupo (Ebrania 11 : 6). Na jambo lolote lifanyikalo bila imani hilo ni
dhambi (Rumi 14 : 23b)
-
Kwa hiyo ukikosa neno la Mungu
ndani yako ni lazima tu utatenda dhambi
6. Wanamwabudu
Mungu kwa mazoea
-
Mathayo 15 : 8
-
Wanamwabudu Mungu kwa midomo tu
bali mioyo yao ipo mbali naye
-
Maana yake wanamwabudu
kimazoea.
7. Hawana
uvumilivu ndani yao juu ya ahadi za Mungu kwenye utumishi walionao
-
1Petro 5 : 6
-
Basi nyenyekeeni chini ya mkono
wa Mungu ulio hodari ili apate kuwakweza kwa wakati wake
-
Tafsiri ya neno kuwakweza maana
yake ni kuwapandisha au kuwainua.
-
Na pia Biblia inasema apate
kuwakweza kwa wakati wake na sio kwa wakati wako.
-
Mungu anajua muda sahihi wa
wewe kuinuka kihuduma. Kuna wakati anajua kabisa kwamba ukifika level Fulani
hutaweza kusimama vizuri na Yeye kwa sababu inawezekana kuna misingi bado
hujaiweka imara kusimama kwenye level hiyo.
-
Kwa hiyo Mungu anachotaka ni
wewe uendelee kumfahamu Yeye zaidi na zaidi na zaidi ili ukue zaidi.
No comments:
Post a Comment