UMUHIMU WA IMANI KATIKA MAISHA YA WOKOVU

 DARASA LA KUUKULIA WOKOVU

Utangulizi:

a.       Maana ya Imani: Waebrania 11 : 1

-          Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

-          Lile jambo unalolitaka ukiliweka bayana, unalipa asilimia zote za kulifanikisha

b.      Chanzo cha Imani: Warumi 10 : 17

-          Imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa Neno la Kristo

-          Kwa hiyo, unaposikiliza Neno la Kristo kwa njia yoyote ile (inaweza kuwa kwa njia ya mahubiri au kwa kusoma Biblia n.k) imani inajengeka ndani yako juu ya Mungu.

-          Ndani yako kwa kupitia Neno la Mungu unapata uhakika ya kuwa Mungu yupo na anauweza wote.

-          Ili uweze kuongezeka viwango vyako vya kiroho ni lazima uinue viwango vyako vya kumtafuta Mungu kwa njia ya Neno na Maombi, na kuishi maisha masafi ndipo imani yako juu ya Mungu itaongezeka

Mfano: unaweza kuamini kuwa Mungu anaponya lakini usiamini kuwa anafufua wafu. Ni muhimu kujikita sana kwenye neno lake ukamjua Mungu zaidi

                Mithali 2 : 1 – 5

-          Ukiwa ni mtu wa kusoma Neno la Mungu na kulitafakari kila siku basi utakuwa na maisha masafi.

-          Ukijaa neno la Mungu ndani yako utaongozwa na Roho Mtakatifu katika kutenda yale yanayompendeza Mungu siku zote. Zaburi 119 : 105

-          Neno la Mungu linatupa furaha tunapopita katika taabu. Zaburi 119 : 92

c.       Kulinda imani

i.                     Dhambi inapingana na imani, maana watendao dhambi ni wa Ibilisi na Ibilisi hawezi kukuruhusu umwamini Yesu Kristo, hivyo basi ukitaka kutembea katika imani ya Kristo ni lazima ujifunze kuishi maisha matakatifu. Epuka dhambi

Yohana 8 : 44

Filipi 2 : 14 – 16

Kolosai 3 : 8 – 10

ii.                   Jitahidi kuwa muombaji kila wakati, imani yako haitayumbishwa

Mathayo 17 : 21 na Marko 9 : 29

-          Hapa maombi hayakuongezei imani bali yanaondoa hali ya kutokuamini ndani yako. Kumbuka kinachokupa imani si maombi bali ni kusikia neno la Kristo. Hivyo maombi yanashughulikia kuondoa hali ya kutoamini ndani ya moyo wako.

-          Na mara nyingi hiyo hali ya kutokuamini inasababishwa na upungufu wa Neno la Mungu ndani ya moyo wa mtu.

UMUHIMU WA IMANI

1.       Imani inatupa ushindi

Ushindi dhidi ya vita vya adui shetani, magonjwa, majaribu

Ayubu 42 : 10 – 12

Isaya 38 : 5

2.       Imani inaleta uponyaji kwa wenye magonjwa na wadhaifu

Mathayo 9 : 27 – 29

Marko 2 : 4 – 5

Marko 5 : 25 – 34

Luka 5 : 17 – 26

Isaya 38 : 1 – 6

3.       Imani inatutia nguvu-

Ukiwa na imani unapata nguvu ya kuvuka hata katika magumu. Mungu anakuvusha salama

Isaya 40 : 31 – wamngojao Bwana maana yake wenye imani kuwa Yesu atarudi tena, Mungu anawajaza nguvu za kuendelea kumtumikia kwa juhudi na kwa bidii bila kukata tamaa wakiwa katika dunia hii iliyojaa dhiki na taabu nyingi.

4.       Imani inatusaidia kuwaleta wenye dhambi kwa Yesu.

Ukiwa na imani kubwa kiasi cha kutenda miujiza basi watu watakapoona hayo watakubali kumpokea Yesu Kristo kwenye maisha yao.

Matendo 11 : 24

5.       Imani hutuletea amani.

Warumi 5 : 1

Isaya 36 : 1, 14 – 22; - 37 : 33 – 35

6.       Imani hutupa uvumilivu.

Ukiwa na imani unaweza ukavumilia na kustahimili changamoto unazopitia katika maisha yako

Yakobo 1 : 3 – 4

Ayubu 42 : 1 - 17

No comments:

Post a Comment

Katika maisha yako usisikilize watu wanasema nini bali msikilize Mungu anasema nini, kwa sababu watu hawajui ni nini ambacho Mungu amekupang...