Lengo la somo hili: Ni kukujengea ndani yako tabia ya kutoa zaka kwa usahihi ili kuinua kiwango chako cha kumjua Mungu na kutembea katika mapenzi yake.
Yako mambo mengi yanayoweza
yakaimarisha uhusiano wako na Mungu, lakini mojawapo kati ya hayo ni utoaji wa
zaka.
Kwa mfano: maombi, kusoma Neno la
Mungu, kushuhudia n.k ni baadhi ya mambo yanayoimarisha mahusiano yako na
Mungu. Lakini pia kuna hili jambo linaloitwa “Zaka“ ni jambo la muhimu sana
katika kujenga msingi mzuri ndani yako wa kumfahamu Mungu.
Malaki 3 : 7 – 10
“Tokea siku za baba zenu mmegeuka
upande mkayaacha maagizo yangu wala hamkuyashika….. leteni zaka kamili ghalani
….”
Ule msatari wa 10 unasema “leteni
zaka kamili ghalani…”
-
Maana yake zaka timilifu au zaka yote, na wala
sio nusu au kiasi.
-
Lakini huwezi ukauelewa huu mstari vizuri kama
hujaanzia kwenye msatari wa 7 ambao unaonyesha jinsi Mungu anavyohuzunika kwa
kuwa wana wa Israel wamegeuka na kumwacha Bwana na wala hawafuati tena maagizo
ya Bwana. Lakini wao wanamuuliza Bwana kuwa wamemuachaje? Naye anajibu kwa
kuwaagiza walete zaka iliyo kamili.
-
Wale wana wa Israel walianza tabia ya kuleta
zaka isiyo kamili mbele za Bwana na wakaona ni jambo la kawaida, lakini Mungu
hakupendezwa na hiyo tabia, ndio maana akaamua kuwaambia wajirekebishe kwa
kutengeneza kile kilichowafanya wamuache Mungu.
-
Hao watu hawakufahamu kuwa kwa tabia yao ya
kutokuleta zaka iliyo kamili iliwafanya waharibu mahusiano yao na Mungu wao,
bali wao waliona ni sawa tu.
-
Wao waliona ya kwamba kule kwenda kanisani na
kutoa sadaka kikawaida ilitosha kuimarisha ukaribu wao na Mungu wao! Hapana!
Uhusiano wako na Mungu haujengwi
tu kwa sababu unakwenda kanisani au unatoa sadaka tu kiholela holela bila
kufuata kanuni za Mungu katika utoaji, bali uhusiano wako na Mungu unajengwa
kwa kufuata maagizo yake na sheria zake katika kutimiza kusudi lake.
MAMBO YA MSINGI YA KUYAJUA KWANZA
a.
Maana ya
zaka
Zaka ni aina mojawapo ya sadaka
anayoitoa mtu kwa kutoa fungu la kumi katika mapato yake.
-
Zaka ni 10% au fungu la kumi la mapato yako
-
Mungu aliagiza mwenyewe ya kwamba tutoe zaka
katika mapato yetu yote
Ziko aina nyingi ya sadaka,
lakini sadaka nyingi ni za hiari bali sadaka ya zaka ni ya lazima
b.
Mahali unapotakiwa
upeleke sadaka yako ya zaka
-
Mungu aliagiza zaka itolewe mahali
alipoliketisha jina lake (maana yake hekaluni)
-
Hesabu 18
: 21 – 24 – zaka ni mali ya Haruni na familia yake
-
Sadaka ya zaka wanapewa makuhani, ndivyo Mungu
alivyoagiza
-
Huwezi ukaibadilisha sadaka ya zaka iwe kama
sadaka ya kawaida halafu uitoe kwa mtu yeyote tu. Hapana. Sadaka ya zaka
inakwenda moja kwa moja kwa makuhani.
c.
Zaka ya
zaka
-
Unapopeleka sadaka yako ya zaka kwa kuhani, naye
pia anatoa zaka katika hiyo zaka aliyoipokea. Hiyo ndio inaitwa zaka ya zaka.
-
Maana yake ni fungu la kumi la fungu la kumi
lililopokelewa hekaluni.
-
Kiongozi wa kanisa au mchungaji au kuhani
anayepokea zaka inambidi nay eye atoe zaka katika hiyo zaka aliyoipokea.
-
Hesabu 18
: 25 – 26
-
Nehemia
10 : 38
d.
Mahesabu ya
zaka yalivyo.
Zaka ni sadaka
pekee ambayo ni lazima uipigie mahesabu. Unatakiwa upige asilimia kumi (10%) ya
mapato yako
Kwa mfano:
i.
Kama
ni mtu unayepokea kipato chako kwa mwezi;
Mfano, umepata
sh 100,000/= zaka yake ni sh 10,000/=
ii.
Kama
unapata kipato chako kutoka kwenye biashara
Zaka unaitoa
kwenye faida unayoipata. Mfano, biashara yako unapata kipato cha sh 20,000/=
kwa siku lakini faida pekee katika hicho kipato chako ni sh 10,000/= basi zaka
utaitoa kwenye sh 10,000/= ambayo itakuwa ni sh 1,000/=
iii.
Pia
kama ndio umeanza kufanya biashara na umekopa mtaji wa biashara hiyo
Zaka utaitoa
kwenye faida unayoipata baada ya kutoa mtaji
Mfano, mtaji wa
biashara yako ni sh 500,000/=
Na unarejesha sh
50,000/= kila mwezi, lakini kipato chako kwa mwezi kinafika sh 70,000/=
Basi, utatoa
kwanza mtaji ambao ndio rejesho kwenye hicho kipato cha mwezi halafu
kitakachobaki ndio utatoa zaka. 70,000 –
50,000 = 20,000 hivyo utatoa zaka katika sh 20,000 ambayo ni sh 2,000/=
NB: Ukishamaliza kuulipa mkopo wote,
hapo ndipo utakapokuwa unatoa zaka kwa kuipigia kwenye faida yote unayoipata
kwa kila mwezi. Kama unapata sh 70,000 kwa mwezi basi utaipigia zaka katika
hiyo fedha yote maana hakuna mkopo wa kutoa.
iv.
Kuna
zaka za mifugo na mazao au nafaka
-
Kama wewe ni mfugaji wa ng’ombe kwa mfano,
wakizaa watoto (mfano watoto 10) basi unatakiwa umtoe mtoto mmoja sadaka ya
zaka.
Au wewe unafuga
kuku na ukapata vifaranga labda tuseme 20, basi vifaranga 2 ndio zaka,
unatakiwa uipeleke kwa mchungaji.
-
Lakini pia unaweza ukawa unafuga ng’ombe au kuku
au kondoo au mbuzi na ukapata labda tuseme mtoto mmoja, basi ukimuuza mtoto
huyo utatakiwa upige asilimia kumi yake ili utoe zaka.
-
Vivyo hivyo na kwenye mazao
Kama wewe ni
mkulima na umelima mahindi kwa mfano, halafu ukavuna magunia 10 basi gunia moja
ni zaka.
NB: Zaka inayotokana na mazao au mifugo ni muhimu kwanza
uibadilishe kuwa fedha ndipo uitoe maana hiyo ndio njia rahisi nay a uhakika
katika utoaji wa zaka hiyo
-
Kumb 14 :
22 – 25
Unaweza pia ukasoma:
2 Nyakati 31 : 5 – 6
Walawi 27 : 30 – 33
Nehemia 13 : 12
Kwa hiyo, kulingana na Malaki 3 : 10, ukisoma kwenye tafsiri
za kiingereza lile neno “leteni zaka kamili” utakuta anamaanisha “leteni zaka
yote”. Mungu anataka tutoe zaka kwa utimilifu na uaminifu wote.
SABABU YA MUNGU KUAGIZA TUMTOLEE ZAKA
Ø Mungu ameagiza watu tumtolee zaka - ili
uwepo wake ukae katika kile ulichokitolea zaka.
-
Kama ni kazi basi uwepo wa Mungu ukae kwenye
hiyo kazi
-
Na kama ni biashara basi uwepo wa Mungu ukae
kwenye hiyo biashara
Unajua kuna tofauti ya uwepo wa
Mungu kukaa ndani yako wewe uliyeokoka na uwepo wa Mungu kukaa kwenye shughuli
yako unayofanya.
-
Ile kwamba umeokoka na Mungu yupo ndani yako
haimaanishi kuwa pia na Uwepo wa Mungu upo kwenye biashara yako au kazi yako.
-
Na ndio maana wapendwa wengi wana hali ngumu
kiuchumi kwa sababu wanadhani wakishaokoka basi na biashara zao au kazi zao
tayari zinakuwa na ulinzi wa kimungu. Mambo hayakwendi hivyo.
-
Unaweza ukawa umeokoka na ulinzi wa Mungu upo
juu yako lakini biashara au kazi yako haina ulinzi wa Mungu.
-
Kwa hiyo unapotoa zaka unaruhusu uwepo wa Mungu
ukae katika biashara yako au kazi yako au shughuli unayoifanya.
-
Maombi yako hayatoshi kulinda biashara yako bali
sadaka ya zaka inaweza na inamruhusu Mungu kumkemea yeye alaye au aharibuye.
Malaki 3 : 11 – 12
UMUHIMU WA KUTOA ZAKA
Kutoa sadaka ya zaka ni agizo la
Mungu kwa kila mtu kutokana na kipato chake.
-
Unajua sio kwamba Mungu ameagiza watu watoe zaka
kwa sababu ana shida na hela yako bali ni kwa ajili ya kukusaidia wewe unayetoa
hiyo zaka ili uwepo wake ukae kwenye hicho unachomtolea zaka.
-
Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana kwa kila mkristo
kujua kutoa zaka kwa ukamilifu na kwa uaminifu.
Yafuatayo ni mambo yanayotokea
unapotoa zaka:
1.
Uwepo wa
Mungu unaketi katika kazi au biashara au shughuli unayoifanya.
Malaki 3 : 11 - 12
Kutoka 25 : 1 – 2,
8
Sadaka yoyote inaleta uwepo wa
Mungu mahali ambapo unapatolea sadaka.
-
Kama unatoa sadaka kwa miungu basi unaachilia
uwepo wa miungu kuketi mahali hapo ulipopatolea sadaka. Na kama unatoa sadaka
kwa Mungu aliye hai basi unaachilia uwepo wa Mungu ukae mahali hapo ulipotoa
sadaka hiyo.
-
Kwa hiyo sadaka ya zaka, nayo pia inampa nafasi
Mungu akae katika hiyo shughuli au biashara uliyoitolea zaka.
-
Na Mungu akiketi mahali basi utapata kibali,
utapata ulinzi wa Kimungu, utapata uwezesho wa Kimungu, utapata kustawi,
utapata ushindi n.k
Wana wa Israel waliambiwa watoe
sadaka kwa moyo wa kupenda ili Mungu aketi katikati yao.
-
Sadaka inampa Mungu uhalali wa kukaa mahali
-
Na ndio maana walikuwa wanajenga madhabahu ili
watoe sadaka juu ya hizo madhabahu.
-
Kazi mojawapo ya madhabahu ni kujulisha aina ya
mungu anayemiliki hilo eneo ambalo limejengwa madhabahu. Na hakuna
madhabahuambayo hawatoe sadka juu yake.
-
Unapotoa sadaka juu ya madhabahu maana yake ni
unaonyesha uhalali wa mungu anayemiliki mahali ambapo madhabahu imejengwa. Na
ndio maana huwezi ukajenga madhabahu mbili za miungu miwili tofauti katika eneo
moja la sivyo eneo hilo litakuwa na vita vikali sana mpaka mungu mmoja mwenye
nguvu ashinde. Na kinachoipa nguvu madhabahu ni ile sadaka inayotolewa juu ya
hiyo madhabahu
Kama wewe ni mfanyabiashara, pale
unapofanyia biashara kuna watu wanakwenda kutoa sadaka kwa miungu yao ili
miungu hiyo iwafanikishe katika shughuli zao. Sasa kama na wewe hujajua namna
ya kutoa sadaka hasa ya zaka ili Mungu wako apate kukaa katika hiyo biashara
yako basi utakuwa ni mtu wa kushindwa tu siku zote.
2.
Unapata
haki ya kupata baraka kutoka kwa Bwana
Malaki 3 : 10
“mkanijaribu kwa njia hiyo muone
kama sitawafungulieni madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka”
-
Sadaka ya zaka inakupa haki au kibali cha kupata
baraka za Bwana
-
Unakuwa na uhuru wa kumdai Bwana akupe baraka
kwa sababu ni Mungu mwenyewe ndiye aliyesema tukamjaribu kwa njia ya kutoa
zaka.
Baraka - maana yake ni kustawi, kufanikiwa, kupata kibali,
kuongezeka n.k
-
Faida unayoipata kutoka kwenye kazi au biashara
yako, italindwa na Mungu ili uitumie kwa maendeleo, kuongeza mtaji, kufanyia
maendeleo ya familia yako.
-
Ni tofauti na Yule mtu asiyekuwa na mbaraka wa
Bwana, anaweza akapata faida kubwa lakini isimsaidie huyo mtu chochote, anakuwa
ni mtu wa kuandamwa na mabalaa na mikosi mbalimbali
3.
Zaka
inaleta roho ya kumcha Mungu ndani ya mtoaji
Kumb 14 : 22 – 23
Mtu mwenye tabia ya kutoa fungu
la kumi mara kwa mara ni lazima ndani yake ijengeke hofu ya Mungu.
-
Ndani yako mazoea yanaondoka na badala yake
inaingia tabia ya kumcha Bwana.
-
Unajua kuna wakati mwingine unaweza ukaombea
sana uamsho uje kanisani, ili watu wajifunze kumcha Bwana, halafu unashangaa
Mungu anakusisitizia juu ya kutoa zaka. Kumbe anakujulisha kuwa kwa njia ya
kutoa zaka tunaweza kujifunza kumcha Bwana.
-
Mungu hawezi kukuruhusu uendelee kumtolea zaka
na bado ukawa hujui kumcha yeye.
Matendo 10 : 1 – 4
Upo uhusiano
kati ya kutoa sadaka na kumcha Bwana. Ni vitu viwili ambavyo haviwezi
vikaachana.
4.
Zaka
inaachilia roho ya utumishi kwenye uzao wako.
Mwanzo 14 : 17 – 20 – 24
Ebrania 7 : 1 – 10
Hii ni habari ya Ibrahimu wakati
ametoka kuwapiga wale wafalme watano, Biblia inasema akakutana na mfalme
Melkizedeki ambaye alimpa sadaka ya fungu la kumi la vitu vyote alivyoviteka
nyara.
-
Kitu cha ajabu hapa ni kwamba, utoaji huu wa
zaka uliachilia roho ya utumishi kwenye kizazi chake ambapo roho hiyo ilipita
mpaka kwa Lawi na uzao wake ambao walikuja kuwa makuhani.
-
Lawi alikuwa ni mtoto wa Yakobo, maana yake ni
uzao wa tatu kutoka kwa ibrahimu
-
Katika kipindi cha Musa, kabila la Walawi ndili
kabila pekee lililopewa kuihudumia madhabahu ya Bwana na kupokea sadaka ya
fungu la kumi. Na Biblia inaweka wazi kabisa kuwa wakati Ibrahimu anatoa sadaka
ile kwa Melkizedeki na Lawi pia alikuwepo hapo japo alikuwa katika viuno vya
Ibrahimu.
-
Kwa tafsi nyingine ni kwamba kutoa sadaka kwa
babu (Ibrahimu) kuliachilia roho ya utumishi kwa kitukuu chake (Lawi).
ITIFAKI YA KUTOA SADAKA
Ni lazima unapokwenda kutoa
sadaka mbele za Mungu uwe na imani.
Ebrania 11 : 6 – “kila amwendeaye Bwana lazima aamini kuwa yupo …”
-
Imani ndio inayofanya fedha yako iitwe sadaka.
Kwa mfano, unaweza ukawa n ash 1,000/= halafu ukaamua kumtolea Mungu sadaka y
ash 500/= na wewe ubaliwe na sh 500/=. Ile 500 uliyoitoa sadaka na ile 500
uliyobakiwa nayo tofauti yake ni imani. Mia tano ya kwanza ambayo ni sadaka
imebeba imani ndani yake bali mia tano ya pili ambayo sio sadaka haina imani
ndani yake.
Mwanzo 28 : 20 – 22 & Mwanzo 31 : 10 – 13 (Yakobo aliweka nadhiri ya fungu la kumi)
No comments:
Post a Comment