Msisitizo: Somo hili litakusaidia kujua mambo yatakayokuza na kuchochea kipawa cha uongozi ndani yako.
Katika somo hili tutalenga zaidi juu ya
mtazamo (altitude) alionao mtu unavyoweza kumsaidia au kumuondolea kipawa cha
uongozi ndani yake.
Ipo tofauti kati ya mtu anayeongoza na mtu
anayeongozwa.
-
Kinachowatofautisha ni mtazamo (altitude)
-
Mtazamo ndio unaofichua viongozi katikati ya
kundi
-
Kiongozi anaona jambo kwa namna ya tofauti na
wale wanaoongozwa wanavyoliona jambo hilo
TUANGALIE
JAMBO HILI LA MTAZAMO WA UONGOZI KWA KUPITIA MIFANO YA HAWA VIUMBE WAWILI:
1.
Mfano
1: Ndege Tai (Eagle)
Tai ni ndege mfalme katika ndege wote
wanaoruka na wasioruka. Na ana sifa tofauti sana ukilinganisha na ndege
wengine. Sifa hizo ndio zinazompa upekee wa kujifunza kitu cha uongozi ndani
yake.
Kuna mambo ambayo ndege karibuni wote
wanafanana kama vile kupaa hewani, kutaga mayai, kujenga viota n.k lakini pia
kuna sifa walizonazo hawa ndege ambazo zinawafanya wawe na utofauti kutoka
jamii moja ya ndege na jamii nyingine.
Baadhi
ya sifa za tai zinazoonyesha sifa za uongozi ndani yake
a.
Tai
ni ndege anayeruka juu zaidi kuliko ndege wote
Tai anaruka juu zaidi kwa sababu hataki
kuchangamana na ndege wengine ambao sio level yake (viwango vyake)
-
Tai ni ndege ambaye yuko makini katika
kuchagua aina ya company au marafiki
-
Tai anaporuka juu hategemei kukutana na ndege
mwingine isipokuwa tai mwenzake. Tafsiri yake ni kwamba tai hawezi
akachangamana na marafiki wasiomsaidia (wasiokuwa level zake)
Vivyo hivyo kiongozi ni lazima na ni muhimu
kuwa makini sana katika kuchagua aina ya marafiki au watu wake wa karibu.
NB:
Kuna aina ya marafiki au watu ambao hutatakiwa kabisa kuwa nao kama watu wako
wa karibu, kwa sababu wanaweza kuharibu kile kilichopo ndani yako
1
Korintho 15 : 33 – msidanganyike, mazungumzo mabaya huharibu
tabia njema.
-
Mazungumzo mabaya yanaweza yakaletwa na
washauri au marafiki ulionao kwenye maisha yako.
-
Kuna viongozi wameshindwa kufanya mambo
makubwa, sio kwa sababu wao ni viongozi wabaya bali ni kwa sababu wana marafiki
wasiowasaidia
-
Wanasaikologia wanasema – ukitaka kujua tabia
ya mtu basi angalia aina ya marafiki wanaomzunguka huyo mtu utagundua tabia
yake
-
Viongozi wengi wana marafiki ambao ni watu
waliokata tamaa, wenye mtazamo wa kushindwa, wasioona mbali
-
Hao marafiki wa aina hiyo wana mchango mkubwa
sana katika kuharibu mtazamo wa uongozi
ndani yako.
-
Ndio maana tai huwa ana tabia ya kuruka juu
sana ambapo atakutana tu na tai wenzake – maana yake atakutana na wenye mtazamo
unaofanana na wa kwake.
b.
Tai
ni ndege anayependa dhoruba au tufani (storm)
Huyu ndege huwa anapenda sana dhoruba kwa
sababu humsaidia kwenda kwa kasi zaidi hewani
-
Tai anapokutana na dhoruba angani ndio muda
anaojiachia vizuri katika mwendo huo wa upepo wa dhoruba, na huo upepo
humsaidia aruke juu zaidi
-
Kwa hiyo hutumia dhoruba kwenda mbali zaidi
angani. Ni tofauti na wanyama au ndege wengine ambao huwa wanaogopa
wanapokutana na dhoruba lakini tai huifurahia dhoruba hiyo.
Kiongozi unatakiwa usiogope changamoto
unazokutana nazo bali uzitumie changamoto hizo kama ngazi ya mafanikio yako
-
Watu wengi waliofanikiwa si kwamba
hawakukutana na changamoto bali waliziona changamoto walizopitia kama ngazi ya
kuelekea kwenye mafanikio yao.
-
Kiongozi unapokutana na changamoto yoyote,
mtazamo unaotakiwa kuwa nao ni lazima uwe ni tofauti na wale wanaoongozwa wanapokutana
na changamoto ya namna hiyo.
-
Mtazamo wa anayeongozwa ukifanana na mtazamo
wa anayeongoza basi sifa ya uongozi inapotea.
1 Samweli 17 : 8 – 11, 16, 23 – 24, 31 – 37
-
Daudi alipokutana na Goliathi hakutishika na
urefu aliokuwa nao, wala ushujaa wa vita aliokuwa nao, bali mtazamo wake juu ya
ushindi katika magumu ndio uliomsaidia kupigana na Goliathi.
-
Unajua Biblia imeeleza jinsi Goliathi
alivyokuwa mrefu, silaha za vita alizokuwa nazo, ujuzi na ushujaa wa kivita
aliokuwa nao na idadi kubwa ya wanajeshi waliokuwa pamoja naye; lakini vyoote
hivyo havikumtisha Daudi asiweze kupigana naye.
-
Daudi hakuwa na uzoefu wa kupigana vita wala
kutumia silaha za vita, kwa kifupi hakuwa na sifa yoyote ya kwenda vitani na
hasa kupigana na mtu hodari kama Goliathi lakini imani aliyokuwa nayo juu ya
mtazamo wake ndivyo vilivyomsaidia kupigana.
-
Daudi alijiona anaweza akashinda ile vita hata
kama hana vigezo vya kupigana katika vita hiyo.
-
Kwa wana wa Israel, vile vita vilkuwa ni
tatizo kubwa sana kiasi kwamba walikaa karibia siku arobaini usiku na mchana bila kwenda vitani
wakimuogopa Yule Goliathi, lakini kwa Daudi vile vita vilikuwa ni fursa (mstari
wa 26).
Kiongozi ni lazima ujue kubadilisha
changamoto kuwa fursa (Leaders must know how to see challenges into
opportunities)
Watu wengi wanakwama hata kuendelea na
uongozi walionao mahali Fulani kutokana na changamoto wanazopitia.
-
Mungu hakumpitisha Daudi ili akutane na simba
au dubu ili auawe bali wamuimarishe mtazamo wake wa uongozi ndani yake ndio
maana hata alipokutana na Goliathi hakupata shida kwa sababu alikwisha pitishwa
kwenye shule ya kuimarisha msimamo wake wa kuona changamoto kuwa fursa kwake.
-
Na hapo ndipo utakapojua kuwa wakati mwingine
Mungu anaweza akaruhusu magumu yakujie kwenye maisha yako kwa ajili ya
kukutengeneza uwe kiongozi mzuri baadae.
-
Ukipitia changamoto sasa, haimanishi kuwa
hautapitia changamoto baadae bali utapitia tu changamoto zingine. Hivyo
changamoto za sasa zinatakiwa zikuimarishe na zikusaidie kupambana na
kukabiliana na changamoto utakazopitia baadae.
c.
Tai
ni ndege mwenye msimamo katika mtazamo alionao (focus)
Hapa tunongelea swala la msimamo katika
mtazamo ulionao juu ya jambo Fulani.
-
Tai huwa anatabia ya kwenda juu sana angani
na kwa sababu hiyo huwa anauwezo wa kuona vitu vingi sana vilivyo chini
ardhini. Na mara nyingi huwa anayaona mawindo yake akiwa huko angani na
kupelekea kuyakimbiza kwa kasi zaidi bila kuyumbishwa na chochote na
anahakikisha ni mpaka anayakamata.
-
Tai anapokusudia kuwinda kitu Fulani huwa
haruhusu kitu chochote kimpotezee lengo alilonalo juu ya kuwinda anachowinda.
-
Na ndio maana huwa anashuka kwa kasi kubwa
ili mawazo yake na macho yake yasitazame kitu kingine bali yatazame mawindo
yake tu.
Na kiongozi unatakiwa kuwa na msimamo katika
mtazamo ulionao juu ya mambo unayoyashughulikia kama kiongozi.
-
Kwa sababu unaweza ukaletea wazo na Roho
Mtakatifu ndani yako kwamba ufanye hiki na kile lakini wale ulionao wakaona
labda ni vigumu kwa jambo hilo kutekelezeka, hivyo wakataka kukushauri
vinginevyo. Unachopaswa kufanya ni kusimamia msimamo wako (na hili ni kama una
uhakika kwamba wazo hilo au jambo hilo ni kusudi la Bwana)
Kutoka 14 : 10 -14, 15 – 16
-
Hizi ni habari za Musa na wana wa Israel
wakati wametoka nchi ya Misri kuelekea Kaanani, walipofika kando ya bahari ya
Shamu hawakujua nini cha kufanya. Mbele yao kulikuwa na bahari, kulia na kushoto
kwao kulikuwa na milima, na nyuma yao kulikuwa na jeshi la Farao ; kwa hiyo
wakaogopa sana kiasi cha kukata tamaa na
kutaka kurudi Misri.
-
Musa ndiye aliyekuwa kiongozi na wana wa
Israel walikuwa wanamlilia yeye juu ya shida yao waliyokuwa nayo. Walimwambia
kuwa wanataka kurudi Misri maana yake waende kinyume na agizo la Mungu
alilopewa Musa. Kama Musa asingisimama imara katika msimamo wake basi
wasingesonga mbele.
Kiongozi unatakiwa ujifunze kusimamia kile
unachokiona kwa sababu kile unachokiona ndicho Bwana anachotaka ukifanye.
-
Kiongozi ni mtu jasiri ambaye ana uwezo wa
kusimamia anachokiamini.
2.
Mfano
2: Simba
Simba ni mfalme katika jamii ya wanyama wa
msituni na porini.
-
Lakini tukiangalia uhalisia ni kwamba simba
sio mnyama mrefu kuliko wanyama wengine, na wala sio mzito au mnene kuliko
wanyama wengine na pia sio mnyama mwenye akili zaidi kuliko wanyama wengine
lakini ndio “king of the jungle”- mfalme wa porini.
-
Ile kwamba anakosa sifa za kuwa si mrefu
kuliko wote, si mzito kuliko wote, au sio smart kuliko wote hamzuii yeye kuwa
mfalme wa porini.
-
Kuwa kiongozi sio swala la kuwazidi watu sifa
za kimwili (urefu, unene, ujanja, ujuzi, elimu n.k) bali ni swala la mtazamo
(altitude)
-
Kwa mantiki hiyo ni kwamba simba ame-cancel visingizio
vyote (execuses) vya mtu kuwa kiongozi. Kwa hiyo mtu hawi kiongozi kwa sababu
ya sura ya nje bali kwa mtazamo alionao.
-
Mtazamo unaweza ukakufanya uwe kiongozi au
la.
¨
Hebu
tuangalie mfano huu:
Simba
anapotokea porini akimuona tembo, haogopi ukubwa wa tembo, wala haogopi nguvu za tembo bali kinachokuja akilini mwake
ni kwamba huyu tembo ni chakula.
-
Lakini pia temo naye anapomuona simba porini
haijalishi kwamba ana umbo dogo kuliko yeye, au hana nguvu kama yeye bali
kinachokuja akilini mwake ni kwamba hapa naweza kuliwa
Ø Kinacho
watofautisha hawa wanyama wawili ni mitazamo yao.
-
Mtazamo ulionao unaweza ukakufanya ujione ni
mdogo sana hata kama kiuhalisia si mdogo
Hesabu 13 : 1 -2, 25, 27 – 33
-
Waliotumwa kuipeleleza nchi ya Kaanani
walikuwa ni viongozi wa kila kabila.
-
Viongozi wawili (Yoshua na Kalebu) kati yao
ndio waliokuwa na mtazamo tofauti na wenzao. Ni kweli wote walikuwa ni viongozi
lakini walikuwa na mitazamo tofauti.
Mtazamo
unatokana na kile unachokiamini (your
altitude is produced from your belief. You can’t have altitude beyond your
belief)
-
Kile unachokiamini ndicho kinatengeneza
mtazamo ndani mwako. Kama unaamini katika kushindwa huwezi ukawa na mtazamo wa
kushinda.
-
Na unakuta wakati mwingine mtu unakuwa ni wa
kusema tu siwezi kufanya hiki, au siwezi jambo fulani, siwezi siwezi siwezi…
hali hiyo itakupelekea kutokuwa na mtazamo wa kuweza hata siku moja.
NB:
Jeshi la kondoo linaloongozwa na simba linaweza likawashinda jeshi la simba
linaloongozwa na kondoo.
-
Tofauti ya haya majeshi mawili ni viongozi
wao ambao hiyo tofauti imetokana na mitazamo yao.
Kwa mfano katika mechi ya mpira wa miguu,
timu inayofungwa mara nyingi hawalaumiwi wachezaji bali analaumiwa kocha.
Kwa nini?
-
Kwa sababu wachezaji wanacheza mpira kwa
akili za kocha wao. Na ndio maana timu inapofungwa huwa hawawafukuzi wachezaji
bali wanamfukuza kocha.
Kiongozi anaweza akafanya kundi likafanya
vizuri au vibaya.
Na ni muhimu sana kujua kwamba kiongozi
unatakiwa uone mbali zaidi ya unaowaongoza wanavyoona.
No comments:
Post a Comment