NINI KINATOKEA UNAPOOKOKA

 DARASA LA KUUKULIA WOKOVU

Karibu tena katika darasa la kuukulia wokovu, na leo tunaangalia zaidi katika mambo yanayotokea au kufanyika mara tu unapookoka.

Tunaokolewa kwa neema ya Mungu wa si kwa matendo yetu – Waefeso 2 : 8

-          Wokovu wetu hautokani na matendo yetu mazuri wala hadhi tulizonazo katika ulimwengu huu bali ni neema ya Mungu ndiyo inayotupa nafasi ya kuokolewa.

Kuna mambo yanatokea pale tu mtu anapookoka:

1.       Unasamehewa dhambi zako zote.

Ø  Isaya 43 : 25 – Mimi ndimi niyafutaye makosa yenu kwa ajili yangu wala sitazikumbuka dhambi zenu.

Ø  1 Yohana 1 : 9 – tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote

Ø  1 Yohana 1 : 7- damu ya Yesu inatusafisha dhambi zote

Hiyo ni baadha ya mistari inayoonyesha kuwa Mungu anatusamehe dhambi zetu zote, anazifuta zote. Kwa hiyo ndani yako usije ukaanza kjikumbushia maisha yako ya kale, unaweza ukajiona kama bado hujasamehewa.

2.       Jina lako linaandikwa kwenye kitabu cha uzima kule mbinguni.

Ø  Ufunuo 20 : 15 – na iwapo mtu yeyote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto

Ø  Luka 10 : 20 – furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni

Jina lako kuandikwa mbinguni maana yake ni kwamba mbingu zinakutambua, unajulikana mbinguni.

3.       Unapata nafasi ya kuwa mwana familia katika familia ya Mungu (katika ufalme wa Mungu)

Ø  Waefeso 2 : 19 - nyinyi si wgeni wala wapitaji bali watu wa nyumbani kwake Mungu

Ø  Wakolosai 1 : 13 – akatuokoa akatuhamisha katika ufalme wa Mwana wa pendo Lake.

Hapo mwanzo ulikuwa huna ushirika na Mungu lakini baada ya kuokoka Mungu anakuwa baba yako na wewe unakuwa kwake Mwana.

Unakuwa na haki ya kuwa mtoto wa Mungu

Ø  Yohana 1 : 12 – bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu

Ø  Mathayo 6 : 9- biblia inasema “Baba ytu uliye mbinguni” haisemi Mungu wetu uliye mbinguni.

Hii inaonyesha wazi kwamba tumefanyika watoto wa Mungu.

4.       Unapata ukombozi mbali na kila kilichokufunga kwenye maisha yako.

Ø  Wakolosai 1 : 13 – Naye alituokoa kutoka katika nguvu za giza – tafsiri yake ni kwamba alituokoa kutoka kwenye vifungo na mateso ya Ibilisi.

Ø  Waefeso 1 : 7 – msamaha wa dhambi ni sawa sawa na ukombozi

Kwa hiyo unaposamehewa dhambi zako, Mungu anakuweka mbali na mateso na uonevu wa kila aina wa shetani.

5.       Unapewa mamlaka ya kiutawala katika ulimwengu war oho

Ø  Waefeso 1 : 20 – 22  & Waefeso 2 : 6 – Tumeketishwa eneo la juu sana la mamlaka katika ulimwengu wa roho. Tumeketishwa pamoja na Kristo Yesu.

Ø  Ufunuo 5 : 9 – 10 – Tulinunuliwa kwa damu ya Yesu tukafanywa kuwa wafalme na makuhani kwa Mungu

Hizo zote zinaonyesha nafasi za kiroho tunazozipata tukishaokoka.

Na kila nafasi ina majukumu yake.

6.       Mwili wako unakuwa ni hekalu la Roho Mtakatifu (pia wewe mwenyewe unakuwa mtakatifu)

Ø  1 Wakorintho 3 : 16 – 17 – miili yetu imkuwa ni hekalu la Mungu, na Roho wa Bwana anakaa ndani yetu.

Ø  1 Petro 1 14 – 16 -  mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

Tunapookoka, miili yetu inakuwa si mali yetu wenyewe bali ni mali ya Bwana, hivyo tunatakiwa tuishi kwa kuepuka uovu.

 

KWA NINI NI LAZIMA KUOKOKA?

Tunaokoka ili:

a.       Ili tupate uhakika wa kuingia katika uzima wa milele

b.       Ili tupate baraka na ahadi za Mungu katika maisha yetu

c.       Ili tusiwe watumwa wa nguvu za giza

 

No comments:

Post a Comment

Katika maisha yako usisikilize watu wanasema nini bali msikilize Mungu anasema nini, kwa sababu watu hawajui ni nini ambacho Mungu amekupang...