NAMNA YA KUSHUGHULIKIA HOFU INAYOPUNGUZA KIWANGO CHAKO CHA KUMTEGEMEA MUNGU

Msisitizo wa somo hili ni kukujengea msingi imara wa kumtegemea Mungu katika hali zote bila kutetereka.

Somo hili litakusaidia kutengeneza msingi imara wa kumtegemea Mungu kwa kiwango kinachohitajika mbele zake  bila kujali mazingira unayopitia

Zaburi 27 : 1 – 3

“Bwana ni nuru yangu na wakovu wangu nimwogope nani?”

Kuna mambo mawili ninayoyaona katika mistari hii: (i) kuna watu wanakuwa na hofu ndani mwao japo Mungu wao ni ngome na wokovu wao (ii) kuna watu ile hofu inapotea pale wanapojua kuwa Mungu ni ngome na wokovu wao.

Mithali 3 : 5 inasema “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe”.

-          Nataka ufahamu jambo hili, kwamba unapopitia kwenye shida au mazingira yoyote magumu kwenye maisha  yako halafu ndani yako ukajawa na hofu basi ujue kiwango chako cha kumtegemea  Mungu kimepungua.

-          Kumtegemea Mungu ni jambo la imani kwa sababu imeandikwa  (Ebrania 11 : 6) kwamba amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yupo. Hivyo tunaposema kiwango chako cha kumtegemea Mungu kimepungua maana yake ni kuwa kiwango chako cha imani juu ya Mungu wako kimepungua.

Maandika yanasema tunatoka imani hata imani (Warumi 1 : 17). Hii inadhihirisha wazi kuwa imani ina viwango. Pia ina maana kuwa imani inaweza kuongezeka au kupungua.

Mfano 1: Mathayo 17 : 14 – 21 na Marko 9 : 37 – 42

Imani aliyokuwa anaiongelea Yesu sio imani ya kumjua Mungu bali ni imani ya kuwasaidia kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo.  Yesu alikuwa anawaambia kuwa kumwamini Yesu anayeweza kuwaokoa na dhambi ni tofauti na kumwamini Yesu anayeweza kuwaokoa na magonjwa.

-          Unaweza ukawa na Yesu ambaye ni Mkombozi wako lakini ukawa huna Yesu ambaye ni Mponyaji.

-          Kwa hiyo fahamu kwamba kiwango chako cha imani kikipungua basi ujue kuwa kuna aina ya changamoto ukizipitia nhutoweza kuzishinda. Hii ni kutokana na kwamba kila changamoto inayokutana nayo inahitaji level Fulani ya imani ili uishinde hiyo changamoto.

Yesu alikuwa anawaambia kuwa kilichowafanya mshindwe kutoa pepo Yule si kwa sababu hamniamini mimi bali ni kwa sababu ndani yenu kuliingia hofu ikapunguza kiwango cha imani yenu juu ya nguvu za Mungu za kuponya.

Waefeso 3 : 20 “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo makubwa mno kuliko yale tuyaombayo au tuyawazayo kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu”.

-          Neon “kwa kadiri” maana yake “kwa kiwango”. Kwa hiyo utendaji kazi wa Mungu kwenye maisha yako unategemea kiwango cha nguvuya Mungu inayotoka ndani yako, nguvu hiyo inaachiliwa kwa nia ya imani.

-          Hiyo imani ikipungua na nguvu ya Mungu inayoaachiliwa ndani yako nayo inapungua.

NB: Hofu ni adui mkubwa sana wa imai yako. Na upate kujua ya kwamba huoweza kuvuka kwenye mazingira yako kama hofu inayokuzuia haijaondoka ndani yako.

Kazi ya hofu ni ku-disconnect nguvu ya Mungu iliyopo ndani yako isishughulike na tatizo ulilonalo.

Mifano mingine zaidi:

Ukisoma Mathayo 9 : 29 – ndipo alipowagusa macho yao akasema kwa kadiri ya imani yenu mpate.

Maana yake ni kwamba unpokea kwa Bwana kwa kadiri ya imani yako.

Pia ukisoma Luka 10 : 17 – ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha wakisema hata pepo wanatutii kwa jina lako

NAMNA YA KUSHUGHULIKIA HOFU ILIYOPO NDANI YAKO

1.       Kusoma Neno la Mungu kila wakati

Kuwa na tabia ya kusoma Neno la Mungu mara kwa mara kutakusaidia kukujengea uhakika wa kumjua Mungu na nguvu zake. Hivyo utafahamu kuwa hakuna lisilowezekana kwa Bwana.

Kumb 20 : 1 – 4 – kila wakati Yesu atakuambia usiogope kwa maana yeye yuko pamoja na wewe ili akuokoe.

Kwa kupitia Neno la Mungu unaifahamu kweli ya Mungu.

2.       Kufunga na kuomba

Mathayo 17 : 21 – namna hii haitoki isipokuwa kwa kufunga na kuomba. Hapa Yesu haongelei kwamba uombe ili utoe pepo au uponye bali anatuelezea kuwa na tabia ya kuwa na maombi ya mara kwa maraitaondoa hali ya kutokuamini ndani mwako.

Kinachokwamisha watu wasione matokeo ya kile wanachokiomba sio nguvu za Mungu bali ni kiwango cha nguvu hizo za Mungu zinazotoka ndani yako.

3.       Kuhudhuria ibada mara kwa mara

1 Wathesalonike 5 : 11 na Yuda 1 : 20

Biblia inasema “Basi farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake.” Pia mahali pengine anasema “Bali ninyi wapenzi mkijijenga juu ya imani iliyo takatifu sana na kuomba katika Roho  Mtakatifu”.

Kuhudhuria katika ibada ni agizo la Bwana wetu Yesu Kristo nani njia pekee ya kujengna kiimani kwa sababu imani ni kama mkaa usiowaka moto lakini ukiuchanganya na mikaa mingine inayowaka moto basi hata ule usiowaka moto nao utawaka moto.

No comments:

Post a Comment

Katika maisha yako usisikilize watu wanasema nini bali msikilize Mungu anasema nini, kwa sababu watu hawajui ni nini ambacho Mungu amekupang...