Mkazo wa somo: ni kukusaidia kutunza na kuimarisha imani yako kwa Yesu Kristo bila kufuata udanganyifu wa adui. Ni muhimu ukajua kuilinda imani yako uliyonayo kwa Mungu.
Yako mashambulizi yanayoletwa na hizi roho zidanganyazo juu
ya wateule wa Yesu Kristo ili wasiendelee kumwamini na kumtegemea Mungu wao.
1 Timotheo 4 : 1
Biblia inaeleza wazi ya kwamba nyakati za mwisho watu
watajitenga na imani wakisikiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
-
Lile
neno “kujitenga na imani” maana yake wataicha imani ya kweli na wataelekea
imani potofu.
-
Maana
yake ni kwamba kuna roho chafu ambazo zinatoka kwa shetani zinazoachiliwa
katika kipindi hiki cha siku za mwisho kwa ajili ya kuwapoteza watu na
kuwaondolea imani yao kwa Yesu Kristo.
-
Kikubwa
zaidi kinacholengwa hapo ni watu kupoteza mahusiano kati yao na Mungu wao.
-
Kwa
sababu imani inaleta mahusiano binafsi kati ya mtu na Mungu wake. Huwezi
ukaenda mbele za Mungu kama humwamini; ni lazima kwanza uamini kama yupo –
ndivyo kitabu cha Waebrania 11 : 6
inavyotuambia.
-
Hizi
roho za udanganyifu zinakuja kipindi hiki kabla ya Yesu kurudi mara ya pili ili
watu watetereke kiroho wasiwe imara. Unajua uongo kazi yake ni kukufanya utoke
kwenye ukweli.
Hata pale katika bustani ya Edeni, roho ya udanganyifu ilikuwepo,
ilitangulia kuja kabla ya Mungu hajashuka na kuwatembelea Adamu na Hawa siku
ile wakati wa jua kupunga.
Mwanzo 3 : 1 – 8
-
Mungu
aliposhuka aliwakuta tayari wamekwisha danganywa na nyoka kwamba wakila matunda
walioambiwa wasiyale hawatakufa, wakati Mungu aliwaambia kuwa wakila hayo
matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya watakufa. Na huo ndio ulikuwa ni
uongo wa adui ili kuharibu uhusiano uliokuwepo kati ya mtu na Mungu.
Uongo huwa unafanana na ukweli lakini sio ukweli. Uongo
utabaki kuwa ni uongo na ukweli utabaki kuwa ni ukweli. Hakuna namna yoyote
ambayo uongo utageuka na kuwa ukweli. Hakuna!
Na hivi ndivyo itakavyokuwa katika nyakati hizi za mwisho ya
kwamba roho ya udanganyifu inaachiliwa
kwa ajili ya kuwaondolea watu imani yao kwa Yesu Kristo.
Swala sio kutokuwa na imani bali wanakuwa na imani juu ya
vitu vingine au watu wengine lakini sio kwa Yesu.
Mathatyo 24 : 3 – 4
-
Hapa
wakati Bwana Yesu ameulizwa na wanafunzi wake juu ya dalili za kuja kwake mara
ya pili na ya mwisho wa dunia; Yesu aliwajibu kwa kuwataadharisha juu ya ujio
wa roho za uongo ambazo zinaweza kuonekana zinafanya kazi sawa sawa na ukweli
lakini sio za kweli.
-
Bila
kuongozwa na Roho Mt. ndani yako ni vigumu sana kutenganisha uongo katikati ya ukweli.
-
Shetani
ili ampate mtu huwa anamletea kitu kinachofanana na cha kweli lakini sio cha
kweli.
Kwa mfano: kama unatembea njiani, roho ya
udanganyifu haikuzuii kutembea bali itakuletea njia nyingine isiyo sahihi.
-
Roho
ya udanganyifu haiwezi kukuzuia usisikile mahubiri au mafundisho bali
itakuletea mafundisho yasiyo sahihi.
-
Hata
kama katika mahubiri au mafundisho hayo wanataja jina la Yesu haimaanishi kuwa
hayo ni mahubiri sahihi. Biblia inasema wengi watakuja kwa jina langu wakisema
mimi ndiye nao watadanganya wengi.
-
Na
ndio maana tunahitajika kujaa Roho Mt. wakati wote kwa sababu yeye ndiye
kiongozi wetu kutujulisha mambo yaliyojificha hata mambo ya siri yeye anayajua.
Ni hatari sana kwa wakristo wa nyakati hizi kutokujaa Roho Mt. ndani yao.
Mathayo 24 : 5, 24 – 25 – Yesu anawaonya na kuwapa angalizo
juu ya ujio wa roho za udanganyifu ambazo zitatumia jina la Yesu au mafundisho
yanayodhaniwa kuwa ni sahihi na kumbe sio sahihi. Na wengine watatoa hadi
ishara na maajabu makubwa na kuwadanganya watu kuwa ni Yesu amefanya hiyo
miujiza na kumbe sio kweli.
-
Lengo
kubwa hapo ni kuwaondolea watu imani yao waliyonayo kwa Yesu.
-
Na
ndio maana watu wengi kwa sasa wanakwenda ibadani au kanisani lakini hawana
imani na Yesu wanayemwabudu. Wako tayari kuamini vitu kama keki au maji au
mafuta ya upako lakini hawamwamini Yesu anayeweza kuwasaidia bila hivyo vitu.
Na wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kuwaamini watu na kuwategemea lakini
mioyoni mwao wamemwacha Bwana.
Sasa angalia, kinachofanya watu wasiwe na imani kwa Yesu Kristo ni mafundisho yasiyo
sahihi. Kisikutishe sana kwamba watu wanajazana katika nyumba za ibada
zenye miujiza, wengi hawamfuati Yesu mtenda miujiza bali wanafuata miujiza
yake. Na imani yao hawajaiweka kwa Yesu bali wameiweka kwenye vitu wanavyodhani
kuwa ndio vimewapa miujiza.
-
Ndio
maana Yesu akatuambia tuwe makini tusije tukadanganywa.
MOJAWAPO
YA MBINU ZINAZOTUMIWA NA ROHO ZA UDANGANYIFU KUFANYA KAZI
v Zipo mbinu nyingi ambazo zinatumiwa
na roho ya Udanganyifu katika kutenda kazi kwake. Mojawapo ya mbinu hizo ni kuwafanya wakristo wasijue na kuthamini kazi
za silaha za kiroho za Mungu tulizopewa kuzitumia (kuzijua kazi za silaha
moja moja dhidi ya shetani)
Waefeso 6 : 11 - 17
Unajua tumepewa silaha za kumpinga shetani na kazi zake. Ziko
silaha za kujilinda na silaha za kushambulia.
-
Na
mara nyingi tumekuwa tukizitumia silaha za kushambulia zaidi na tukaacha zilaha
za kujilinda.
-
Tunasahau
ya kuwa shetani naye anazo silaha zake za kutushambulia hivyo ni lazima na sisi
tuvae silaha zote ili tuweze kuizima mishale yote inayotoka kwa adui.
-
Biblia
inatuagiza tuvae silaha zote na sio baadhi – (ule mstari wa 11)
Kwa hiyo, Roho ya udanganyifu inakufanya usione umuhimu wa
kila silaha za kumpinga shetani.
-
Na
kwa sababu hiyo ni vyema ukatambua kuwa mojawapo ya hila za shetani ni hiyo
roho ya udanganyifu.
-
Ili
uzipinge hila zote za shetani basi
ni lazima uvae silaha zote za Mungu.
Hiyo ndio kanuni ya Kimungu ilivyo.
NB: Kila silaha ina kazi yake na ina
umuhimu wake, hivyo kama hutoivaa na hutojua namna ya kuitumia basi ujue kuwa
kuna mahali tu utakwama kwa sababu shetani atakushambulia, na wewe hutoweza
kumpinga.
Silaha
mojawapo ambayo watu wengi huwa hatujui na pia hatupendi kuitumia sana ni
Chapeo ya wokovu.
Chapeo maana yake ni kofia ngumu au kofia
ya chuma, na huwa inavaliwa kichwani kwa ajili ya kulinda kichwa.
Isaya 59 : 17 na 1 Thesalonike 5 : 8
-
Kichwa
ni eneo mojawapo katika mwili wa mtu ambalo ni la muhimu sana kulilinda. Kwa
mfano uko vitani; adui yako anaweza akakulenga kichwani na akawa amekumaliza kabisa
kabisa (hata ikapelekea kufa) lakini kama atakulenga sehemu nyingine za mwili
wako kama miguuni au mkononi bado kuna uwezekano wa kuwa mzima na ukaendelea na
mapambano. Kwa hiyo kichwani ni sehemu nyeti sana.
NB: Si watu wengi sana tunaojua kwamba
wokovu ni silaha mojawapo tuliyopewa na Mungu ambayo ni silaha ya kujilinda.
Tuiangalie silaha
inayoitwa chapeo ya wokovu
Hapa nataka tuangalie jambo hili kwa mtazamo huu ufuatao:
Yesu ni kichwa cha kanisa. Hivyo Yesu ndiye anayevalishwa
kofia hiyo kwa sababu yeye ndiye kichwa chetu, (ili uelewe vizuri zaidi jambo
hili, ni vyema ukatazama kwa mtazamo huu wa mtu, yaani Yesu ndiye kichwa, na
kanisa ndio mwili; kwa hiyo chapeo ya wokovu inavaliwa kichwani yaani
anavalishwa Yesu)
-
Sasa
angalia, kwa nini Yesu ambaye ndiye kichwa chetu tumvalishe kofia ambayo ni
wokovu? Tunalinda nini?
Jibu la swali hilo ni
kama ifuatavyo: Ni
lazima kwanza ujue Yesu anajifunua kama nani kwako.
Ø Yohana 14 : 6
– Yesu kwetu anajifunua kama njia, na
kweli na uzima
Kwa hiyo unamlinda Yesu kama unalinda
njia, unalinda kweli, na unalinda uzima. Ni muhimu sana ukatambua jambo hili
kwa sababu litakusaidia kuepuka mashambulizi ya roho ya udanganyifu.
a. Njia- maana
yake ni uhakika wa uelekeo wako. Wapi unaelekea?
-
Shetani
akitaka kukudanganya hakunyang’anyi njia unayoiendea bali anakuonyesha njia
nyingine isiyo sahihi. Anachokifanya shetani ni kukupoteza uelekeo wako. Hiyo
ndio maana ya kukudanganya.
-
Mtu
anapodanganywa maana yake amefuata jambo lisilo sahihi akidhani yakuwa ni
sahihi. Kama ni njia, anakuwa amkwenda kwenye njia isiyo sahihi akidhani kuwa
ni njia sahihi. Kwa hiyo maisha ya huyo mtu au mahusiano ya mtu huyo na Mungu
wake ni lazima yaharibike au yapate shida kwa sababu uelekeo wake sio sahihi.
-
Hivyo
shetani anakuwa amekupoteza kwenye uelekeo wako.
ü Hapa wokovu unalinda njia au uelekeo wako. Wokovu unakusaidia
kutokugeukia njia nyingine mbali na Yesu.
b. Kweli
-
Hapa
shetani anachokifanya ni kukuletea maneno yatakayofanana sana na kweli lakini
ni ya uongo. Anaweza akatumia mafundisho au mahubiri yaliyopotoka kwa lengo la
kukufanya usifahamu kweli ya Kristo.
-
Shetani
anaweza akapindisha maagizo uliyopewa na Mungu kuhusu jambo fulani ili
kukupoteza kwenye lengo alilolikusudia Mungu alipotoa hayo maagizo. Ni sawa na
kile kipindi katika bustani ya Edeni, nyoka alimwambia mwanamke kuwa mkila
matunda yale hamtakufa wakati Mungu alisema kuwa wakila hakika watakufa.
-
Ndio
maana Biblia inamuita shetani ni baba wa uongo (Yohana 8 : 44). Pia mahali pengine Biblia inasema kuwa shetani
anajigeuza kwa mfano wa malaika wa nuru (2
Korintho 11 : 14 - 15)
-
Maneno
ya shetani ni feki bali maneno ya Kristo ni ya kweli, nuru ya shetani ni feki
na nuru ya Kristo ni kweli.
ü Hapa wokovu unakulinda usije ukaamini kila neno linalokuja kwako au
unaloletewa kwa sababu shetani anaweza akaachilia maneno yake ya uongo na
yakavuruga uhusiano wako na Mungu.
Hivyo unatakiwa kuwa makini hata na
mafundisho unayoyasikiliza. Sio kila mafundisho ni ya kusikiliza kwa sababu
yanaweza yakakuharibu kiroho chako. Unapaswa kutulia mahali pamoja bila
kutangatanga hovyo.
c. Uzima – maana
yake ni maisha aliyoyakusudia Mungu tuishi.
Waefeso 2 : 10
– kuna aina fulani ya mfumo wa maisha ambayo Mungu ameyakusudia watoto wake
tuishi.
-
Sasa
shetani anachofanya ni kukuletea aina nyingine ya mfumo wa maisha ambayo sio
sahihi kwa mtoto wa Mungu kuishi lakini aina hiyo ya maisha inafanana sana na
ile aina ya maisha ya Kimungu. Shetani anakuletea mfumo feki.
-
Unaanza
kuona watu wa Mungu badala ya kuanza kukemea dhambi ndio wanaanza kuisifia na
kuiishi. Ukiangalia lugha zao, matendo yao kuwaza kwao hakuna tofauti na
mataifa wanavyoishi.
-
Unakuta
vijana wengi wa kikristo wanaishi maisha ya kwenda na wakati hata kama
wanamkosea Mungu, wao hawajali bali wanachojali ni kwenda na wakati.
-
Na
hiyo inapelekea hata mitindo mingi ya kimaisha ya duniani unaanza kuiona
kanisani kwa sababu ya kuiga.
ü Kwa hiyo wokovu ndani yako utakusaidia kulinda huo mfumo wa maisha ili
uishi kama apendavyo Mungu wako na sio uishi kama dunia inavyotaka uishi.
No comments:
Post a Comment