NAFASI YA KANISA KAMA NURU YA ULIMWENGU

Mathayo 5 : 14 – 16

Yohana 9 : 5 – Yesu ni nuru ya ulimwengu

(Mathayo 6 : 1- Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu kusudi mtazamwe na wao, kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni)

NB: Biblia inatufundisha mambo kadhaa hapa kutokana na hii mistari

1.       Biblia inatutambulisha sisi ni akina nani.

Ninyi ni nuru ya ulimwengu.

2.       Pia Bblia inatujulisha kazi au wajibu tulionao kutokana na utambulisho tulio nao

Nuru yenu na iangaze mbele ya watu.

3.       Na mwisho Biblia inatujulisha nini kinatokea tunaposimama kwenye nafasi zetu vizuri

Wapate kuyaona matendo mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni

Yesu Kristo katika hotuba yake ya mlimani anaweka msingi wa kanisa kama chombo muhimu cha kuuleta ufalme wa Mungu duniani.

-          Watu walidhani amekuja kutengua torati bali kumbe amekuja kutimiliza.

-          Kuna maeneo ya torati yaliwekwa kwa sababu ya ugumu wa mioyo ya waisraeli kipindi wanatoka nchi ya Misri wakielekea Kanaani.

Baadhi ya maeneo aliyoyagusia Yesu katika hotuba yake ni kama ifuatavyo:

-          Mathayo 5: 21, 22, 23

-          Mathayo 5: 27, 28

-          Mathayo 5: 33, 34

-          Mathayo 5: 38, 39

-          Mathayo 5: 43, 44 – 48

-          Na maeneo mengine

Mathayo 5 : 20

Haki yenu isipozidi haki ya mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni

-          Hii inamaanisha kwamba kuna maisha unaweza ukaishi ukidhani kuwa upo tofauti  na watu amabao hawajaokoka lakini kumbe hauna tofati nao.

-          Ndio maana anasema haki yenu lazima izidi haki ya mafarisayo

Kwa mfano, mtu akikukosea wewe uliyeokoka na mtu akimkosea mtu ambaye hajaokoka, tofauti yenu itaonekana wapi?

-          Itaonekana kwenye kupokea maudhi hayo (reaction)

-          Pia itaonekana kwenye eneo la kusamehe  (muda utakaochukua kusamehe na sababu zitakazokufanya usamehe)

No comments:

Post a Comment

Katika maisha yako usisikilize watu wanasema nini bali msikilize Mungu anasema nini, kwa sababu watu hawajui ni nini ambacho Mungu amekupang...