Siku ya wababa duniani & kanisani
Lengo la
somo:
kukusaidia kufahamu umuhimu wa nafasi ya mwanaume kama baba na inavyotambulika
kibiblia katika kutimiza kusudi la Mungu.
Mwanaume katika Biblia ana nafasi nyingi sana.
Anaweza akatambulika kama mume, Baba, kiongozi n.k
-
Na
kila nafasi ina wajibu wake na umuhimu wake kutokana na ilivyoumbwa.
-
Aliyeziumba
hizi nafasi ni Mungu mwenyewe na ameziweka kwa makusudi yake mwenyewe.
-
Kwa
hiyo, kabla ya kuitazama nafasi yoyote kimwili kwanza ni muhimu uitazame kiroho
kwanza ili upate kujua kile kilichomsukuma Mungu kuiumba hiyo nafasi.
-
Usipojua
kusudi la hiyo nafasi basi pia hutoona thamani ya hiyo nafasi.
-
Thamani
ya kitu chochote inatokana na umuhimu wake; kama umuhimu haupo basi hata na
thamani yake haitakuwepo.
Leo nataka
tuone kwa undani kidogo juu ya nafasi ya mwanaume kama baba.
Biblia inapotujulisha nafasi ya baba kwa
mwanaume inataka kwanza tujue nafasi ya Mungu kama Baba ikoje kwa sababu yeye
ndiye Baba wa mababa, maana yake yeye ndiye asili na chanzo cha hiyo nafasi.
Unaweza ukajiuliza ni kivipi Biblia inaonyesha
Mungu anavyojifunua kama Baba!
Waefeso 3 :
14 – 15
– “kwa hiyo, nampigia Baba magoti ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni
na duniani unaitwa…”
-
Lile
neno ubaba wote maana yake familia yote
-
Ubaba
wa Mungu ambao Biblia inaelezea hapa maana yake ni asili ya vitu vyote.
-
Biblia
inaonyesha kuwa Mungu Baba ndiye asili ya mambo yote mbinguni na duniani.
Kwa hiyo, nafasi ya hii ya baba ambayo
mwanaume anapewa asili yake ni kwa Mungu Baba
Yeye ndiye “role model” wetu wanaume, ya
kwamba tukitaka kusimama vizuri inavyotupasa katika nafasi hii ya baba ni
lazima tumfuate yeye (Mungu Baba).
Na nafasi hii inaoonyesha uhusiano wa ndani
zaidi kama mahusiano ya kifamilia (baba na watoto).
-
Kuna
namna hii nafasi inakuletea picha fulani ya ukaribu na wale ambao wewe umepewa
kuwa baba kwao.
-
Ndani
yako ukipewa hii nafasi utaona kama unahusika kwa karibu zaidi juu ya maisha ya
wale uliopewa kuwahudumia kama watoto wako, kwa sababu wewe ndiye baba yao.
NB: Nafasi hii ni zaidi ya kuwa baba wa
watoto kwa maana ya kwamba umewazaa wewe bali wanakuwa ni watoto wako kwa
sababu Mungu ameweka ndani yako kitu cha kuwasaidia hao watu ili uwahudumie kwa
ukaribu ule ule kama ambavyo ungewahudumia watoto wako.
BAADHI YA TAFSIRI ZA KIBIBLIA ZINAZOONYESHA
UMUHIMU NA MAANA YA NAFASI YA BABA
Sasa fahamu ya kwamba hii nafasi ya baba ndani
yake imebeba tafsiri tofauti tofauti kulingana na Biblia inavyoeleza. Baadhi ya
tafsiri hizo ni kama ifuatavyo:
1.
Nafasi ya baba
kama mzazi wa kiume
Kwa lugha nyingine ni kwamba Yule mzazi wa
kiume anaitwa baba.
-
Kwa
hiyo, kila mwanaume mwenye uzao, kwa lugha nyepesi anapata kuwa na hii nafasi
ya kuitwa baba.
-
Hii
nafasi ni ya mwanaume pekee na sio ya mwanamke na baba ndiye aliyebeba nasaba
za uzao wake.
Nasaba ni uhusiano wa kizazi baina ya watu
kutoka katika ukoo mmoja au familia moja. Hiyo ndiyo inayoonyesha undugu,
familia, ukoo, jamaa moja n.k
-
Na
uhusiano huo ni lazima uwe uhusiano wa kizazi
-
Kumbuka
kuwa, mtoto amebeba damu ya baba yake na sio damu ya mama yake.
Nehemia 7 : 5
Ezra 2 : 59
Mbari za baba zao maana yake ni nasaba (DNA –
Deoxyribonucleic Acid)
Ndio maana hata kwenye historia ya ukoo wa
Yesu inaonyesha jinsi ambavyo uhusiano wa vizazi ulivyokuwa tangu Ibrahimu hadi
Yusufu baba mlezi wa kimwili wa Yesu.
-
Japokuwa
Yesu hakuzaliwa kutokana na baba na mama bali kwa uweza wa Roho Mtakatifu,
maana yake ni kwamba damu ya Yesu ilikuwa si damu ya kibinadamu iliyotoka kwa
baba yake bali ilikuwa ni damu halisi ya Mungu Baba mwenyewe ndiyo maana ni
damu bora zaidi kupita damu zote na ndiyo iliyoweza kutuosha dhambi zetu.
Baba ndiye mzalishaji, hivyo damu yake na ya
mtoto ni sawa.
-
Mtoto
hachukui damu ya mama bali damu ya baba yake.
-
Kitaalamu
ni wazi kabisa kwamba kwenye tumbo la uzazi la mwanamke, mtoto anachopata
kutoka kwa mama ni mfumo wa chakula bali mfumo wa damu anakuja nao kutoka
kwenye mbegu za uzazi kutoka kwa baba.
NB: Katika ulimwengu wa roho kuna eneo
la uzazi la mwanaume na eneo la uzazi la mwanamke
-
Eneo la uzazi la mwanaume linaitwa
“viunoni”
Mwanzo 35 : 11
2 Samweli 7 : 12
Mwanzo 46 : 26
Kutoka 1 : 5
-
Na eneo la uzazi la mwanamke linaitwa
“tumboni”
Mwanzo 25 : 22, 23, 24
Watoto wakashindana tumboni mwake…, Bwana
akamwambia mataifa mawili yako tumboni mwako.
Rebeka aliona watoto wawili wako tumboni mwake
bali Mungu aliona mataifa mawili yako tumboni mwake
Maana
yake ni nini? Maana yake ni kwamba Rebeka aliliona tumbo lake la kawaida
kimwili kwamba limebeba mapacha bali Mungu aliliona tumbo la Rebeka la kiroho
kwamba limebeba mataifa mawili.
Yeremia 1 : 5
Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua- maana
yake tumbo la kimwili la mama yake
Na kabla hujatoka tumboni nalikutakasa- maana
yake kabla hajatoka katika tumbo la uzazi la kiroho la mama yake alitakaswa
Tumbo – ni kimwili, tumboni ni kiroho (jifunze kujua hilo)
Zaburi 58 : 3 – wasio haki wamejitenga tangu
kuzaliwa kwao, tangu tumboni wamepotea wakisema uongo
Wanaongeaje
wakiwa kwenye tumbo? Hii inaonyesha ni kwenye tumbo la kiroho (panapoitwa
tumboni)
Nimejaribu kukuonyesha kwa kiasi tu kuwa haya
mambo ya uzazi yameanzia rohoni kwanza kabla hayajaja mwilini, hivyo ni muhimu
kuyajua ili unapoombea uzao wako ujue namna ya kuomba.
2.
Nafasi ya baba
kama tegemeo la msaada kwa ajili ya kutunza au kuhifadhi maisha ya watu.
Hii ni nafasi tofauti na ile ya baba kama
mzazi wa kiume
Biblia pia imeonyesha nafasi ya baba ambayo
mtu hupewa na Mungu kwa ajili ya watu ili kuhifadhi na kutunza maisha yao kwa
sababu ya kile kitu kilichopo ndani ya huyo mtu.
Kumbuka kwamba Mungu alipokuumba aliweka
kipawa au karam fulani ndani yako ambayo hutoitumia tu kwa ajili ya maslahi
yako peke yako bali pia kwa ajili ya wale watu ambao Mungu atakuletea
uwahudumie.
Kuna watu ambao kuishi kwao, kuendelea kwao,
au kufanikiwa kwao kunategemea uwepo wa mtu fulani, kwa sababu huyo mtu ana
kitu fulani ndani yake ambacho ni msaada kwa ajili yao.
-
Watu
wa aina hii wapo kwenye jamii zinazotuzunguka.
-
Kuna
wengine ni matajiri na wanawasaidia watu wenye uhitaji na wengine ni watu wa
kawaida lakini wanaweza kuwasaidia watu kwa njia nyingine.
Mfano 1: Yusufu
alikuwa kama baba kwa Farao
Mwanzo 45 :
7 – 8
Mungu alinipeleka mbele yenu kwa ajili ya
kuwaokoa maisha yenu na ndio maana amenifanya kuwa kama baba kwa Farao
-
Biblia
inatuonyesha jambo la ajabu sana hapa. Inaonyesha kwamba maisha ya Farao kama
mfalme wa Misri yalitegemea sana uwepo wa Yusufu katika taifa lake, katika
namna ambayo alimuona kama baba yake.
-
Na
kitu hicho Yusufu alikijua. Yusufu alijua umuhimu aliokuwa nao mbele ya Farao,
ndio maana akawaambia ndugu zake kwamba yeye amekuwa kama baba kwa Farao.
-
Na
sio tu Farao aliyemuona Yusufu kama baba bali taifa zima la Misri na mataifa
jirani pia, kwa sababu kitu alichobeba Yusufu ndani yake kiliwasaidia mataifa
yote ya kipindi kile.
-
Hivyo
tunaelewa kuwa ndoto alizoziota Yusufu akiwa mtoto hazikuwa ndoto kwa ajili yak
wake binafsi bali zilikuwa ni kwa ajili
ya kuhifadhi maisha ya watu. Mungu akamfanya Yusufu kuwa kama baba kwako.
Mfano 2:
Ayubu kama baba kwa maskini na wahitaji
Ayubu 29 :
12 – 16 – 17
Nalikuwa baba kwa mhitaji na daawa ya mtu
nisiyemjua naliichunguza.
-
Maandiko
yanaonyesha kwamba Ayubu pamoja na utajiri wake na kumcha Mungu kwake bado pia
alikuwa ni msaada na tegemeo kwa watu maskini na wenye uhitaji.
-
Hao
watu hawakuwa ndugu zake wala hakuwa anawafahamu lakini alihusika katika
kuwasaidia mambo mbalimbali kwenye maisha yao.
-
Kulikuwa
na watu kipindi cha Ayubu ambao walimtegemea Ayubu kwa kula, kuvaa, kuishi, na
hata kupata mahitaji mbalimbali
-
Ayubu
alipoanza kupita kwenye majaribu pia wale watu nao walipita kwenye hali ngumu
kwa sababu msaada wao (yaani Ayubu) hakuweza kuendelea kuwasaidia tena.
Na mara nyingi huwa hatujui namna ya kuwaombea
watu wa namna hii tulionao kwenye jamii zetu. Hivyo unakuta kama wakipata shida
yeyote, sio tu kwamba wao wenyewe ndio watateseka bali na jamii kubwa ya watu
wanaowategemea pia watapata shida.
3.
Nafasi ya baba
kama mwanzilishi na kiongozi wa kabila au ukoo au familia
Mwanzo 25 :
22 – 23
– Bwana akamwambia mataifa mawili yako tumboni mwako, na kabila mbili za watu
watafarakana tangu tumboni mwako.
-
Hawa
watoto wawili ambao ni mapacha walikuwa ni waanzilishi wa mataifa mawili
tofauti. Mmoja alikuja kuwa mwanzilishi wa taifa la Israel na mwingine taifa la
Waedomu
Mwanzo 10 : 21- Shemu ambaye ni baba wa
wana wote wa Eberi
Mwanzo 36 : 8 – 9 – Esau ndiye baba wa Edomu
wote.
Biblia inaonyesha kuwa mataifa na makabila na
jamaa na familia zimetoka kwa watu.
-
Kuna
watu ambao Mungu aliwaweka kuwa waanzilishi na waasisi wa mataifa mbalimbali au
makabila au ukoo.
-
Sasa
hao waanzilishi wanaitwa baba. Unaweza kukuta wameelezea kwa mfano baba wa
Edomu wote, au baba wa kabila la Yuda, au baba wa kabila la Manase
Hesabu 1 : 4
Mfano 1: Hesabu
17 : 1 – 3, 6
-
Hapa
tunaona mfano huu kwamba kila fimbo moja ilikuwa inawakilisha nyumba ya kila
baba ambaye ni katika wakuu wa makabila yao.
-
Sasa
angalia, kama zingekuwa ni nyumba kwa maana ya familia basi zisingekuwa fimbo
12, zingekuwa fimbo nyingi sana. Bali wale wababa wa kila nyumba walikuwa ni
viongozi wa makabila ya wana wa Israel (makabila kumi na mbili)
Makabila katika taifa la Israel yametokana na
watoto wa Yakobo, hivyo kila mtoto mmoja alikuwa ni baba wa kabila lake
-
Yeye
ndiye aliyelizaa hilo kabila
-
Yeye
ndiye mwanzilishi wa hilo kabila
-
Na
yeye ndiye aliyebeba baraka au laana za kabila zima
-
Kila
aliyezaliwa katika kabila husika alikutana na mbaraka au laana hiyo iliyotokana
na mwanzilishi wa kabila hilo – Mwanzo
49 : 1 – 28 & Hesabu 18 : 1 - 2
4.
Nafasi ya baba
kama kichwa cha familia au mke
1 Wakorintho 11 : 3
Waefeso 5 : 23
-
Biblia
inaonyesha namna ambavyo Mungu amemweka mwananume kuwa kichwa cha familia yaani
kiongozi wa familia.
-
Na
siku zote, kiongozi wa familia anawajibika katika hiyo familia
Hebu
tuangalia kidogo baadhi ya wajiu na majukumu ya mwanaume mwenye nafasi hii ya
baba kama kichwa cha familia.
a.
Kuitunza na
kuilea familia yake
Waefeso 5 :
28 – 29
– ni wajibu wa kila baba kuilisha na kuitunza familia yake.
Maana yake ni kwamba baba anahusika na
maendeleo ya kila mtu aliyeko katika familia anayoitunza.
-
Usiwe
mmoja wapo wa wale wanaume wanaozikimbia familia zao kutokana na hali ngumu za
kimaisha, bali unatakiwa uwe kielelezo na mfano kwa watu wa familia yako. Ndio
maana ukaitwa kichwa cha familia.
-
Kuna
familia ambazo mke anaweza akamuona mumewe ni kama baba yake. Hii ni kutokana
na ukweli kwamba mume amesimama vizuri katika nafasi yake ya kuilea na kuijali
familia yake pamoja na mke wake.
b.
Baba ni mwalimu
katika familia
Kumb 6 : 6 – 7
Mithali 22 : 6
Ni wajibu wa kila mzazi na hasa baba wa
familia kuwafundisha watoto wako njia iwapasayo kuiendea.
-
Baba
huwezi ukafundisha watu waifuate njia iliyo sahihi wakati wewe mwenyewe hauendi
katika njia sahihi. Hivyo ni lazima uchague kwanza njia sahihi ndipo utakapojua
namna ya kuwafundisha watoto na familia yako yawapasayo kufanya. Yoshua 24 : 15
Pia baba anatakiwa ajue namna ya kuwaonya
watoto wake anaowapenda
Waebrania 12 : 6
Mithali 3 : 11 – 12
c.
Baba hutakiwi
kuwakatia tamaa watoto bali unatakiwa kuwavumilia na kuwapenda
Luka 15 : 11
– 32
Huo mfano unaonyesha namna Yule baba wa mwana
mpotevu alivyokuwa na uvumilivu na upendo mkubwa kwa mwanaye aliyedai urithi
wake mapema na kuondoka. Aliporudi alimuomba msamaha baba yake na akasamehewa.
Haijalishi mtoto wako amekukosea kiasi gani,
hutakiwi kumkatia tamaa bali unatakiwa kumuonya na kuendelea kumpenda.
Moja ya sifa ya kuwa baba bora ni kujua namna
ya kuwasamehe watoto wako waliokukusea pale wanaporudi kwako kukuomba msamaha.
d.
Baba una wajibu
wa kuweka urithi kwa ajili ya uzao wako
Mithali 13 :
22-
mtu mwema huwaachia wana wa wanaye urithi.
Mithali 19 :
14
– nyumba na mali ni urithi mtu apatao kwa babaye
Hivyo ni wajibu wa kila baba ambaye ni kichwa
cha familia kutengeneza “future” ya watoto wake (yaani kutengeneza maisha ya
baadae ya watoto wako).
-
Ni
lazima ujifunze kuona mbele zaidi kule ambako familia yako inaelekea.
Baba hutakiwi kujifikiria wewe tu peke yako
bali unatakiwa kufikiri juu ya familia yako inaishije na inauelekeo upi.
Kumbuka kuwa wako watoto wanaokutegemea wewe
na pia wako wajukuu wanategemea waishi vizuri kutokana na urithi utakao waachia
(ni haki yao kibiblia kupata urithi kutoka kwako).
Mjukuu kudai urithi kutoka kwa babu yake ni
haki yake kibiblia.
Hivyo ufahamu na akili yako ewe baba
vinatakiwa vifunguke ili uone jamii kubwa ya watu wanao kutegemea na kukufuata
nyuma yako.
Ni lazima ujifunze kuishi kwa malengo ili
uishi maisha yenye maana. Mitahli 29 :
18
Ni maombi yangu kuwa somo hili litafungua kwa
sehemu ufahamu wako na kukusaidia kuanza kuishi kama vile apendavyo Mungu wako
aliyekuokoa.
-
Kumbuka
kuwaombea na wababa wengine ili watumie nafasi zao vizuri
-
Wanaume
wengi hawajua majukumu yao kwa sababu hawajafundishwa na imepelekea kupata
kizazi ambacho kinabaki kujiita tu mimi ni kichwa cha familia lakini hajui
maana yake na wajibu wake ni nini kuwa kichwa cha familia.
No comments:
Post a Comment