SEMINA YA MKESHA WA MWAKA MPYA 2023
Msisitizo wa somo: Ni
kukujengea tabia ya kupenda kumshukuru Mungu kila wakati kwenye maisha yako.
1 Thesalonike 5 : 18
“shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika
Kristo”
-
Huu mstari uzito wake upo kwenye hii sehemu ya pili
inayosema “… maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”
-
Watu wengi huwa hatuna habari na huo mstari tukidhani
yakuwa hautuhusu lakini ukweli ni kwamba ndio uliobeba maana/uzito wa mstari
mzima.
-
Tafsiri yake ni kwamba anachokitaka Mungu kwetu sisi
ni tuwe na shukrani mbele zake katika mazingira yote hata kama ni magumu. Mungu
huwa anapenda kushukuriwa. Anapenda kuona watoto wake wakiwa wanamshukuru Yeye
katika hali zote wanazopitia.
Ukisoma kwenye Biblia ya Kiswahili
unaweza usione huo uzito lakini baadhi ya tasfiri za Biblia za kiingereza
zinaonyesha wazi jambo hilo.
Kwa mfano:
American Standard
Version-ASV
“In everything give thanks: for this is the will of God in Christ
Jesus to you-ward.”
Amplified Bible-AMP
“In every situation [no matter what the circumstances] be
thankful and continually give thanks to God; for
this is the will of God for you in Christ Jesus.”
Complete Jewish
Bible-CJB
“In everything give thanks, for this is what God wants from you
who are united with the Messiah Yeshua.”
Contemporary
English Version-CEV
“Whatever happens, keep thanking God because of Jesus Christ. This
is what God wants you to do.”
-
Hapo tunaona kwamba kutokana na hizo tafsiri
mbalimbali za Biblia, Kumshukuru Mungu ni jambo ambalo Mungu anategemea watoto
wake watakuwa wanalifanya mara kwa mara kwake.
-
Ndani mwako itaanza kutengenezeka tabia ya kumshukuru
Mungu sit u kwenye matukio maalum bali hata kwenye mambo ambayo unadhani ni ya
kawaida kwako lakini Mungu anahitaji shukrani zako.
-
Wengine wanamshukuru Mungu baada ya kuwavusha kwenye
magumu na wengine wanamshukuru Mungu baada ya kuwapatia mahitaji yao. Hayo yote
ni mema, lakini tambua kwamba kumshukuru Mungu ni kwenye mambo yote.
Jambo la muhimu la kufahamu ni
kwamba huwezi ukamshukuru Mungu wakati unapita kwenye hali ngu kama humuoni
Kristo kwenye hiyo hali.
-
Wengi tunaona kushindwa, kukata tamaa, kuvunjwa moyo, kudharauliwa,
n.k
-
Lakini ukijifunza kumuona Kristo kwenye hiyo taabu
unayopitia, basi kitakachoinuka ndani ya moyo wako ni kumshukuru Mungu.
-
Kumshukuru Mungu hakuji hivi hivi; ni lazima ujifunze
kwanza kumuona Yesu Kristo kwenye hiyo hali unayopitia ndipo utamshukuru Mungu.
-
Unajua kuna wakati mwingine unaweza ukapitia hali
ambayo ni vigumu sana kusema kwamba utamshukuru Mungu, kwa sababu moyo unakataa
kabisa kutokana na ugumu wa mazingira unayopitia. Si kwamba hujui kuwa
unatakiwa kumshukuru Mungu bali moyo unakataa kabisa. Hapo unatakiwa umuombe
Mungu akusaidie.
MAANA YA KUMSHUKURU MUNGU
Kumshukuru Mungu ni ile hali ya kuonyesha
kuwa unatambua na unathamini kazi anayoifanya Mungu kwenye maisha yako.
-
Kumbuka kuwa huwezi kuhesabu mambo ambayo Mungu
anakutendea kwenye maisha yako. Wema wa Mungu umekuzunguka muda wote na pande
zote ndio maana leo hii uko hai bila kujalisha mazingira unayopitia.
-
Sasa kule kujua kuwa wema wa Mungu umekuzunguka pande
zote na kwamba hajakuacha, yuko pamoja nawe katika hali zote, kunakupa hali ya
kuendelea kumtegemea na kumwamini, ndipo swala la kumshukuru linapokuja hapo.
Unaweza ukamshukuru Mungu kwa njia mbalimbali kama vile:-
-
Maombi ya shukrani
-
Sadaka ya shukrani
-
Nyimbo za shukrani n.k
NINI KINATOKEA UNAPOMSHUKURU MUNGU
1.
Mungu
anakufungulia msimu mpya mbele yako ambao ameachilia nguvu zake zikusaidie
kwenye huo msimu.
Mwanzo 8 : 15 – 22
Mungu alirejesha majira yaliyokuwa
yameharibiwa na gharika baada ya kusikia harufu nzuri ya sadaka iliyotolewa na
Nuhu. Tunaamini yakuwa ilikuwa ni sadaka ya shukrani kwa sababu tunaona Mungu
akirejesha kwa upya majira yaliyopotea.
Tunapoingia msimu mpya hasa huu
mwaka mpya wa 2023 ni muhimu kuwa na baraka za Bwana ambazo zitatufanikisha
katika njia tunazopitia.
Kwa wengine mwaka mpya unaweza
ukawa ni mambadiliko tu ya tarehe lakini kwenye yao hakuna chochote
kinachobadilika. Lakini kwetu sisi tunaomjua Mungu, mwaka mpya ni msimu mpya.
Maana yake ni lazima tuone baraka na uweza wa Bwana ukiwa juu yetu kwa viwango
vingine ili kutufanikisha na kutusaidia.
-
Kama ni utumishi, basi tunamuona Mungu akiinua viwango
vyetu vya kutumika mbele zake kwa utukufu na na kibali kikubwa.
-
Kama ni hali ya kiuchumi kwenye familia, basi
tunamuona Mungu akihusika kuinua uchumi wetu kwa viwango vya juu zaidi.
2.
Unampa
Mungu nafasi ya kushughulika na adui zako.
2 Nyakati 20 : 15 – 17, 21 – 22
Hawa wana wa Israel walimshukuru
Mungu kabla ya vita wakiamini kwamba Mungu atawapigania, na ndivyo ilivyokuwa
kwani Mungu aliwashindia vita bila wao kupigana.
-
Unapomshukuru Mungu katikati ya magumu unayopitia
inaonyesha ni kwa jinsi gani unamtegemea Mungu akusaidie kukuvusha katika hiyo
hali.
-
Wana wa Israel waliona vita ni vikubwa na adui zao ni
wengi kuliko wao, kwa namna yoyote ile ilikuwa ni vigumu sana kuishinda ile
vita bila msaada wa Mungu. Lakini walipotambua siri iliyopo katika shukrani
basi walishinda vita kwa kumshukuru Mungu.
Kuna wakati unaweza ukawa unapitia
hali Fulani ambayo si nyepesi kwenye maisha yako lakini ghafla ndani ya moyo
wako unakuja wimbo au nyimbo za kumshukuru na kumsifu Mungu, ujue kuwa Roho Mt
anakujulisha ni nini unachotakiwa kukifanya kwa wakati huo. Maana yake Mungu
anataka umshukuru Yeye ili Yeye ashughulikie tatizo lako.
3.
Utukufu wa
Mungu unashuka
2 Nyakati 5 : 1 – 13 – 14
Baada ya wana wa Israel kuijenga
nyumba ya Bwana, ile siku ya ufunguzi wakati wanaliingiza sanduku la agano
ndani ya hekalu, ndipo walipomsifu na kumshukuru Mungu mpaka utukufu wa Mungu
kama moshi ulishuka ukalijaza hekalu lote hata watu walishindwa kuonana.
-
Mungu alijidhihirisha kwa namna ya pekee sana ambapo
ule utukufu ulilifunika hekalu lote.
-
Kumbe, tunapomsifu na kumshukuru Mungu basi utukufu
wake unashuka kwenye maisha yetu.
-
Na utukufu wa Mungu ukikushukia hutabaki jinsi
ulivyokuwa. Ni lazima Mungu akutane na haja za moyo wako, ni lazima maisha yako
yabadilishwe, ni lazima Mungu aondoe aibu ya kudharauliwa na kuonewa katika
maisha yako.
Matendo 16 : 23 – 26
Wafilipi 4 : 6
4.
Kunampa
Mungu nafasi ya kufanya zaidi ya vile ulivyo muomba.
Luka 17 :
12 – 19
Hii ni habari ya wale wenye ukoma
kumi waliomwende Yesu wakiomba awaponye, yesu aliwaponya lakini ni mmoja wao tu
ndiye aliyekuja kushukuru kwa Yesu.
-
Bwana Yesu alishangaa kuona ni mtu mmoja tu ndiye
aliyekuja kumshukuru wakati wote waliponywa. Yesu alitegemea awaone wote wakija
kumshukuru.
-
Mungu yuko serious na swala la kushukuru.
-
Kushukuru si swala dogo mbele za Mungu, lina uzito
wake.
-
Wewe unaweza ukaona ni jambo dogo tena la kawaida
lakini mbele za Mungu ni jambo kubwa sana na Mungu huwa analifuatilia.
-
Si watu wengi wanajua kuwa Mungu akikupa kitu huwa
anafuatilia kuona kama utamshukuru.
-
Yule aliyerudi kushukuru alipewa kitu kingine ambacho
hao wenzake hawakupewa. Alipewa wokovu, maana aliambiwa imani yako imekuponya.
Wote mwanzoni waliomba kuponywa lakini aliye shukuru alipewa ziada, (imani yake
ilimwokoa).
Tunaposhindwa kumshukuru Mungu kwa
mambo tunayomuomba basi huwa tunakosa kupata hata vile ambavyo tungevipata kama
tungeshukuru.
Kuna mambo kweye maisha yako ambayo
utayapata tu endapo utamshukuru Mungu.
-
Kuna wakati Mungu atakupa upendeleo ambao huo huwezi
kuupata usipokuwa mtu wa shukrani mbele za Mungu.
No comments:
Post a Comment